• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
OFISI YA MKUU WA MKOA WA SIMIYU
OFISI YA MKUU WA MKOA WA SIMIYU

.JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA .OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA OFISI YA MKUU WA MKOA WA SIMIYU

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Idara na vitengo
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Kitengo cha Uhasibu na Fedha
      • Kitengo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano(TEHAMA)
      • Kitengo cha Ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Huduma za Sheria
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Fursa za Uwekezaji
  • Sekta ya Afya
    • Hospitali ya Rufaa ya Mkoa
    • Huduma za Afya Mkoa
  • Sekta ya Elimu
  • Sekta ya Kilimo
    • Sekta ya Mifugo
    • Sekta ya Uvuvi
    • Sekta ya Maliasili na Mazingira
    • Sekta ya Ushirika
  • Sekta Utalii
  • Kituo cha Habari

Bilioni 440 kumaliza changamoto ya Maji Chumvi Simiyu, RC Dkt.Nawanda amshukuru Rais Samia,Aahidi kuulinda Mradi kama mboni ya Jicho, Asisitiza ajira kwa Wazawa wakati wa utekelezaji Mradi.

Posted on: May 27th, 2023

Pichani:Waziri wa Maji Mhe.Jumaa Awesu pamoja na Viongozi mbalimbali wa Chama na Serikali wakishuhudia utiaji saini mkataba wa utekelezaji Ujenzi wa Miundombinu ya Maji,Mradi wa kukabiliana na mabadiliko ya Tabia Nchi Mkoani Simiyu 27 Mei 2023 katika eneo la Stendi ya Zamani ya Mji wa Bariadi.


Na IO.Simiyu

Wakazi wapatao 494,000 wa Mkoa wa Simiyu watanufaika kupitia Mradi wa kukabiliana na mabadiliko ya Tabia Nchi unaohusisha Ujenzi wa mradi mkubwa wa kutoa Maji Ziwa Viktoria na kuyapeleka katika Wilaya za Busega, Bariadi, Lagangabilili, Maswa na Meatu na vijiji vilivyoko pembezoni mwa bomba kuu utakapopita mradi huo.

Tarehe 27 Mei 2023 Wizara ya Maji ilisaini mkataba wa ujenzi wa miundombinu ya maji, mradi wa kukabiliana na mabadiliko ya Tabianchi mkoani Simiyu ambapo Katibu Mkuu Wizara ya Maji Mhandishi Nadhifa Kemikimba na Kampuni ya M/S China Civil Engineering Construction Cooperation CCECC LTD kutoka China ambayo imewakilishwa na Mkurugenzi Msaidizi wa kampuni hiyo Bw. Wu Zegang walisaini Mkataba huo huku Waziri wa Maji Nchini Mhe.Jumaa aweso akishuhudia utiaji Saini wa Mkataba huo.

Waziri wa Maji Mheshimiwa Jumaa Aweso (Mb)  katika hotuba yake aliwahakikishia Wananchi wa mkoa wa Simiyu kuwa mradi huo utakamilika kwa wakati ili kutimiza adhma ya Serikali  kuhakikisha Wananchi wanapata huduma bora  ya maji safi na salama.

 Alisema mkataba unamtaka mkandarasi atekeleze mradi huo kwa miaka minne hadi Agosti 2025, hivyo Wizara itahakikisha inamsimamia kwa ukaribu ili kazi hiyo ikamilike kwa wakati.

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe.Dkt.Nawanda alipowahutubia Wananchi wa Mkoa wa Simiyu alimshukuru Mhe.Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kuwajali Wananchi wa Mkoa wa Simiyu ambapo ameeleza kuwa hatua ya Serikali kutia saini mkataba wa Bilioni 440 wa Ujenzi wa Mradi huo utaondoa kabisa changamoto ya uhaba wa Maji Mkoani Simiyu.

Aidha RC Dkt.Nawanda amemhakikishia Waziri wa Maji Mhe.Juma Aweso na Wananchi kwa ujumla kuwa Serikali Mkoani Simiyu itashirikiana bega kwa bega na Wananchi katika kuhakikisha kuwa miundombinu ya mradi huo inalindwa kwa nguvu zote.

Katika hatua nyingine Mhe.Dkt Nawanda emetoa rai kwa Kampuni itakayotekeleza Ujenzi wa Mradi huo kutoa kipaumbele kwa Watanzania hususani Wazawa ili kusudi mradi huo uwe chachu ya Wananchi kujipatia kipato na ajira wakati wa utekelezaji wake.

Fedha za Mradi wa kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi Mkoani Simiyu zimechangiwa na wadau mbalimbali ambapo serikali ya Tanzania inatoa Euro milioni 40.7, sawa na shilingi za Tanzania Bilioni 105.8. Serikali ya Ujerumani Euro milioni 26.1 sawa na shilingi za kitanzania Bilioni 67.9, Shirikika la kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (GCF) Euro milioni 102.7 sawa na shilingi za Tanzania Bilioni 267. Mchango wa wananchi kupitia nguvu zao unatarajiwa kugharimu Euro milioni 1.5 sawa na shilingi za Tanzania bilioni 3.9


MATUKIO MBALMBALI KATIKA PICHA WAKATI WA HAFLA YA UTIAJI SAINI MIKATABA YA UJENZI WA MIUNDOMBINU YA MAJI,MRADI WA KUKABILIANA NA MABADILIKO YA TABIA NCHI 

Picha 1.Waziri wa Mji Mhe.Juma Aweso akivalishwa Skafu na Skauti mara baada ya kuwasili katika eneo la Stendi ya Zamani kushuhudia tukio la utiaji saini Mkataba wa Ujenzi wa miundombinu ya Mji,Mradi wa kukabiliana na mabadiliko ya Tabia Nchi 27 Mei 2023.



Matangazo

  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 01, 2025
  • Fungua

Habari Mpya

  • MASHINDANO YA UMISETA NA UMITASHUMTA YAZINDULIWA KIMKOA MASWA. DC NGATUMBURA ASISITIZA NIDHAMU NA BIDII ILI KUPATA USHINDI KATIKA NGAZI YA TAIFA.

    May 30, 2025
  • SIMIYU RS WAHAMIA JENGO JIPYA LA UTAWALA NYAUMATA

    June 03, 2024
  • RC NAWANDA ARIDHISHWA NA UJENZI MRADI WA MAJI MWABUMA/MWASHATA MEATU.

    May 30, 2024
  • RC SIMIYU ARIDHISHWA NA MAENDELEO UJENZI WA MRADI WA USAMBAZAJI MAJI WA VIJIJI VYA SUNZULA, MWAMNEMA NA NGESHA WILAYANI ITILIMA,

    May 29, 2024
  • Fungua

Video

MIAKA MINNE YA RAIS DKT.SAMIA SULUHU HASSAN MKOANI SIMIYU
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • TUME YA RAIS UKUSANYAJI MAONI MABORESHO YA KODI YATUA SIMIYU
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii
  • SIMIYU- RS TV

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Video

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa