• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

Zaidi ya Milioni 138 Zatolewa Mikopo kwa Wanawake Simiyu

Posted on: March 8th, 2021

Katika mwaka wa fedha 2019/2020 Halmashauri sita za Mkoa wa Simiyu zimetoa shilingi 138,030,500/= kwa vikundi 122 vya wanawake kama mikopo kutoka katika asilimia nne ya mapato ya ndani ya halmashauri, kwa ajili ya kuwapatia mitaji ya kuanzisha na kuendeleza shughuli zao za kiuchumi.

Hayo yamesemwa na Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu, Bi. Miriam Mmbaga kupitia hotuba yake iliyosomwa kwa naiba yake na Mwanasheria wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Bi, Manahamisi Kawega wakati wa maadhimisho ya siku ya wanawake Duniani Machi 08, 2021 ambayo kimkoa yamefanyika Wilayani Maswa.

“Halmashauri ya Mji wa Bariadi, imetoa shilingi 10,000,000/= kwa vikundi 25, Halmashauri wilaya ya Bariadi shilingi 48,000,000/= vikundi 37, Busega shilingi 16,000,000/=kwa vikundi 16, Itilima shilingi 12,000,000/= vikundi 12, Maswa shilingi 39,200,000/= vikundi 18 na Meatu shilingi 12,830,500 kwa vikundi 14,” alisema.

Aidha, Mmbaga amewaagiza Wakurugenzi wa Mamalaka za Serikali za Mitaa kuendelea kutenga na kupeleka fedha asilimia nne kwa ajili ya kutoa mikopo kwa vikundi vya wanawake kwani haina riba kuliko mikopo kutoka taasisi nyingine za kifedha.

Vile vile Mmbaga amesema kauli mbiu ya siku ya wanawake mwaka 2021 “ Wanawake katika Uongozi:Chachu ya kufikia Dunia yenye Usawa” itumike kuwawezesha wanawake kwenye nafasi za uongozi katika mkoa wa Simiyu kwa kuwa jamii bado haijatambua umuhimu wa kumuwezesha mwanamke nafasi za uongozi tunapoelekea kwenye Dunia ya usawa.

Naye Katibu wa CCM Mkoa wa Simiyu, Bi. Haula Kachwamba ametoa wito kwa viongozi wanawake kufanya kazi kulingana na matarajio ya wanawake huku akisisitiza wahakikishe wanatafuta ufumbuzi wa changamoto za wanawake.

Mkuu wa Wilaya ya Busega, Mhe. Tano Mwera amewataka wanawake kujiamini na  kujitokeza katika fursa mbalimbali za uongozi katika jamii kwa kuwa viongozi wanawake ni wachache, hivyo kila fursa inapopatikana wasisite kujitokeza ili kuwe na viongozi wengi wanawake katika kuelekea dunia yenye usawa.

Maadhimisho ya siku ya wanawake Duniani Kimkoa yaliambatana na maonesho ya shughuli za wanawake wajasiriamali, uchangiaji damu, kutoa misaada kwa wagonjwa ambapo chama cha Wafanyakazi wa Afya na Serikali (TUGHE) walitoa msaada wa mashuka 30 kwenye wodi ya wazazi katika Hospitali ya Wilaya ya Maswa.

MWISHO

KUPATA PICHA ZAIDI FUNGUA KUNGANISHI HIKI:-https://simiyuregion.blogspot.com/2021/03/zaidi-ya-milioni-138-zatolewa-mikopo.html

Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa