• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

World Vision Yakabidhi Zahanati, Vifaa Vya Kujikinga na Corona Simiyu

Posted on: May 9th, 2020

Shirika lisilo la kiserikali la World Vision limekabidhi msaada wa vifaa vya kujikinga na maambukizi ya Virusi vya Corona pamoja na Jengo la zahanati kwa uongozi wa mkoa wa Simiyu vyote vikiwa na thamani ya shilingi milioni 95.7.

Akikabidhi msaada huo jana Mei 08, 2020 kwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu, Bw. Jumanne Sagini katika kijiji cha Wigelekelo wilayani Maswa, Meneja wa World Vision Kanda ya Ziwa, Bw. John Massenza amesema pamoja na zahanati wamekabidhi mipira ya kuvaa mikononi, vitakasa mikono,vipaza sauti, barako na mavazi maalum ya wataalam wa afya.

"Pamoja na zahanati leo tunakabidhi mipira ya kuvaa mikononi boksi 500,vitakasa mikono lita 200,vipaza sauti 26 kwa wahudumu wa afya ngazi za jamii na mavazi ya kujikinga na maambukizi 60 na barakoa aina ya N95, vyote vikiwa na thamani ya shilingi 95,755,000/=, "alisema Massenza.

Aidha, ameongeza kuwa shirika hilo kwa kushirikiana na ofisi ya mganga mkuu wa mkoa wa Simiyu na waganga wakuu wa wilaya litaendelea kutoa misaada ya vifaa , vitendea kazi, kutoa mafunzo kwa watumishi wa afya na kuhakikisha wanasambaza elimu ya kujikinga na ugonjwa wa homa ya mapafu (COVID 19) inayosababishwa na virusi vya Corona. .

" Shirika limeendelea kutoa elimu ya kujikinga na ugonjwa wa homa ya mapafu kwa njia ya matangazo na tumewezesha mafunzo kwenye makundi tofauti ya watu ambayo yatasambaza elimu hii kwa jamii mfano wa makundi hayo ni viongozi wa dini,wahudumu wa afya ,viongozi wa serikali,  "alisema Massenza.

Akipokea vifaa hivyo pamoja na zahanati Katibu Tawala Mkoa wa Simiyu, Bw Jumanne Sagini ameishukuru World Vision kwa msaada huo ambao umetolewa kwa Halmashauri zote sita pamoja na kuwa shirika hilo linafanya kazi na halmashauri ya wilaya ya Maswa na Itilima; huku akibainisha kuwa vifaa kinga hivyo vitawajengea ujasiri watoa huduma za afya kuwahudumia watakaobainika kuwa na maambukizi ya Virusi vya Corona.

Naye mganga mkuu wa mkoa wa Simiyu,Dkt.Festo Dugange amesema wamekuwa wakitekeleza afua mbalimbali za kuhakikisha wananchi wanakuwa salama dhidi ya ugonjwa wa COVID 19  kwa kutoa elimu ya namna ya kujikinga, huku akiongeza kuwa mkoa upo vizuri na tayari umeshatenga vituo endapo watapatikana washukiwa wa ugonjwa huo.

Akiongea kwa niaba ya wakurugenzi wa halmashauri mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya Maswa, Dkt. Frederick Sagamiko amelishukuru shirika hilo kwa kuwa msaada mkubwa kwenye shughuli za maendeleo mkoani hapo hususani katika wilaya ya Itilima na Maswa ambapo kwa Maswa mbali na kuwajengea zahanati pia limesaidia katika ujenzi wa kiwanda cha viazi lishe na wilaya ya Itilima kiwanda cha sabuni.

Kwa upande wao wananchi wa kijiji cha Wigelekelo wakiwemo Mbuke Kemakema na Mashauri Ngeme wamelipongeza shirika hilo kwa ujenzi wa zahanati ambayo itawasaidia kupata huduma za afya karibu  kwani awali walikuwa wakitembea umbali mrefu kufuata huduma za afya.

MWISHO

KUPATA PICHA ZAIDI FUNGUA LINKI HII:-https://simiyuregion.blogspot.com/2020/05/world-vision-yakabidhi-vifaa-vya.html

Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa