• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

Waziri wa Mifugo Aongoza Waombolezaji Meatu Mazishi ya Diwani Shukia Aliyefariki kwa Ajali

Posted on: July 17th, 2018

Waziri wa mifugo na Uvuvi, Mhe. Luhaga Mpina amewaongoza wakazi wa Wilaya ya Meatu na Mkoa wa Simiyu katika mazishi ya aliyekuwa Diwani wa Kata ya Mwanhuzi wilayani Meatu Elias Shukia aliyefariki katika ajali ya gari Mkoani Singida akitokea Dodoma na kusababisha kifo chake na dereva na kusababisha watu wengine watano kujeruhiwa.

Ajali hiyo imetokea Julai 14 eneo la Mkiwa Wilaya ya Ikungi Mkoa wa Singida ,baada ya gari walilokuwa wakisafiria aina Toyota landcluser DFPA 0148 la Halmashauri ya Meatu kupasuka tairi na kupinduka mara tatu na kusababisha vifo hivyo viwili,huku majeruhi wa ajali hiyo Mkurugenzi Mtendaji, Mwenyekiti wa Halmashauri na Maafisa wa Halmashauri hiyo walipata majeruhi.

Mpina ametoa pole kwa familia, wananchi, Chama Cha Mapinduzi na Halmashauri ya Wilaya ya Meatu na kuwataka kuwa wavumilivu katika kipindi hiki kigumu kwa kuondokewa na madiwani watatu na dereva katika matukio mawili tofauti ya ajali na akawaomba wasifikiri kitu kingine tofauti juu ya kutokea kwa ajali hizo badala yake wajue kuwa ni mapenzi ya Mungu.

“ Kuna watu wanaweza wasiamini kuwa ajali zinaweza zikatokea Meatu kwa muda fupi hivi kama ilivyotokea kwetu, naomba ndugu zangu wananchi, viongozi tusiingie kwenye mtego huo tujue tu kuwa haya ni mapenzi ya Mungu kama walivyosema viongozi wetu wa dini kuwa Mungu ndiye anayejua hatma ya maisha yetu” alisema Mpina.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka ametoa pole kwa familia, chama na wananchi kwa msiba huo na  amewaagiza Viongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Meatu kuhakikisha stahili zote za marehemu zinalipwa kwa wakati kwa familia ya marehemu.

Aidha, amewaomba viongozi wa dini kufanya maombi kwa ajili ya  wilaya ya Meatu na Mkoa wa Simiyu kwa ujumla kuomba Mwenyezi Mungu kuwaepusha viongozi na wananchi na mitihani ya ajali iliyotokea mfululizo.

“Wakati tunawaaga madiwani wetu wale wawili waliofariki kwenye ajali ya kwanza,  Mwenyekiti wa Halmashauri na madiwani wengine walikuwa kwenye matibabu kwa sababu ya ajali, leo tunamuaga Mhe. Shukia Mkurugezi na Mwenyekiti wako kwenye matibabu kwa sababu ya majeraha waliyoyapata katika ajali, sisi kama wanadamu tunaamini kwenye ulimwengu wa roho tuna nafasi ya kuomba, niwaombe viongozi wa dini tumwombe Mungu atuepushe na mitihani hii” alisema

Mbunge wa Jimbo la Meatu Salum Khamis amesema kifo cha mhe. Shukia  ni pigo kubwa kwa kata ya Mwanhuzi na Meatu kwa ujumla kwa kuwa marehemu Shukia enzi za uhai wake alikuwa mtetezi ndani ya Chama Cha Mapinduzi na wananchi katika shughuli za maendeleo.

Akitoa mahubiri wakati wa ibada ya Mazishi, Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania, Dayosisi ya Kusini Mashariki ya Ziwa Victoria, Dkt. Emmanuel Makala aliwakumbusha waombolezaji wote kuishi wakimtegemea Mungu, kwa kuwa kila mtu hapa duniani anaishi kwa neema ya Mwenyezi Mungu, hivyo wanapaswa kuishi maisha ya kumpendeza Mungu.

Marehemu Shukia ameacha mke na watoto wanne, BWANA ALITOA , BWANA AMETWAA JINA LA BWANA LIHIMIDIWE. AMINA!

MWISHO

KUPATA PICHA ZAIDI FUNGUA KIUNGANISHI HIKI:-https://simiyuregion.blogspot.com/2018/07/waziri-wa-mifugo-aongoza-waombolezaji.html

Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa