• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

Waziri wa Afya Aitaka TBA Kurejesha Fedha za Ujenzi wa Mradi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Simiyu

Posted on: January 22nd, 2019

Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto Ummy Mwalimu ameagiza Wakala wa Majengo nchini TBA kurejesha fedha ilizokabidhiwa na wizara yake kwenye ofisi za TBA mjini Bariadi ili zitumike kukamilisha mradi wa ujenzi wa hospitali ya rufaa ya mkoa wa Simiyu ambao kasi ya ujenzi wake kwa sasa hairidhishi.

Waziri Ummy ametoa kauli hiyo katika ziara yake ya siku moja mjini Bariadi, mkoani Simiyu kukagua ujenzi wa jengo litakalotumika kutoa huduma za maabara, upasuaji na mionzi na kusema kuwa serikali imejiwekea malengo ifikapo Julai  Mosi wananchi waanze kupata huduma kwani tayari fedha zote za mradi huo zimekwishalipwa.

 “Wizara tayari imeshalipa zaidi ya shilingi bilioni moja kwa TBA lakini cha ajabu wao wameleta shilingi milioni 430 tu, na matokeo yake ndio haya, ukiangalia muda tuliopewa kukamilisha kazi hii si rafiki, sasa ninawaagiza TBA walete hiyo pesa site ili kazi iendelee”.

“ Hivi jamani kwa kasi hii kweli tunaweza kuendelea kuweka matumaini kwa hawa ndugu zetu, ukiangalia mheshimiwa Rais ametupatia shilingi bilioni 2.5 tujenge jengo la mama na mtoto sasa kwa utaratibu huu wa kusuasua mnadhani tutafika kweli, mimi nadhani umefika wakati tutumie force account kwenye mradi huu, Bariadi kuna mafundi wengi wazawa wenye uwezo mkubwa wa kutufanyia kazi hii”, alisisitiza Waziri Ummy.

Kuhusu mpango wa serikali wa kuboresha huduma za rufaa katika hospitali zote za mkoa nchini, Waziri Ummy amesema wizara imedaa utaratibu ambapo kila hospitali itapata madaktari bingwa 16 katika fani 8 yaani madaktari 2 kila fani wakiwemo madaktari bingwa wa akina mama, watoto, Mishipa ya fahamu, mifupa, njia ya mkojo, dawa za usingizi na mionzi.

“ Tunataka tuwe na maabara kubwa za kisasa pamoja na jengo la mionzi kama tunalojenga hapa Simiyu katika kila hospitali ya rufaa ya mkoa, tunamshukuru sana mheshimiwa rais kwa kutupatia shilingi bilioni 3.5 kwa ajili ya ujenzi wa jengo uchunguzi, ninaomba kila mmoja wenu kwa nafasi yake ahakikishe miradi yote inayotumia fedha za serikali inatekelezwa kwa ufanisi”, aliongeza Waziri Ummy.

Akijibu maombi ya viongozi wa chama na serikali wa mkoa wa Simiyu kuhusu tatizo la usafiri kwa watumishi watakaopangiwa kufanya kazi katika hospitali ya rufaa ambayo kwa sasa haina nyumba za watumishi, Waziri Ummy amewahakikishia kuwa Wizara itaangalia uwezekano wa kuipatia hospitali hiyo basi maalumu la watumishi halikadhalika itaweka bajeti ya ujenzi wa nyumba za watumishi katika mwaka wa fedha ujao.

Akiwa katika hospitali ya wilaya ya Bariadi ya Somanda, Waziri Ummy alielezea kutoridhiswa na utaratibu wa kutoa huduma katika wodi ya wazazi na kumwagiza mganga mkuu wa mkoa kuzifanyia marekebisho kasoro zote zilizobainika ili huduma zinazotolewa ziendane ni miongozo ya wizara.

Kwa upande wake mkuu wa mkoa wa Simiyu Anthony Mtaka amemhakikishia Waziri Ummy kuwa,  mkoa utasimamia kikamilifu utakelezaji wa mradi huo na kusisitiza kuwa pale ambapo pamebainika kuwa na dosari atahakikisha zinarekebishwa ili kuongeza ufanisi katika mradi huo.

“Mhe Waziri mimi nina amini kukamilika kwa hospitali hii ni mkombozi kwa maelfu ya wananchi wetu wa mkoa wa Simiyu,  sasa wajiandae kupata huduma bora zikiwemo za bima ya afya ambazo zimeboreshwa kwa kiwango kikubwa, kwa ujumla tunaamini zitawahamasisha watu wengi zaidi kujiunga na  huduma hiyo”, alisisitiza RC Mtaka.  

Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto Ummy Mwalimu amekamilisha ziara yake mkoani Simiyu na Kuelekea katika mikoa ya Geita na Shinyanga.

Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa