• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

Waziri Mkuu Majaliwa Aitaka SIDO Kupanua Wigo Kuwafikia Wajasiliamali Kuanzia Ngazi ya Chini

Posted on: October 23rd, 2018

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ameliagiza Shirika la viwanda vidogo nchini SIDO  kuweka mikakati ya kupanua wigo wa shughuli zake kwa kuanzisha vituo katika ngazi ya halmashauri za wilaya ili kuwafikia wajasiliamali wengi zaidi, kuwajengea uwezo, kuwapa miongozo bora ya namna ya kuendesha shughuli zao kwa tija na kuwaunganisha na taasisi za fedha  waweze kupata mikopo.

Waziri mkuu Majaliwa ametoa kauli hiyo katika ufunguzi wa maonesho ya SIDO Kitaifa yanayofanyika katika viwanja vya Nyakabindi Wilayani Bariadi Mkoani Simiyu ambapo amesema umefika wakati kwa SIDO kutilia mkazo sekta ya viwanda na hivyo kuifanya jukwaa la kuwakutanisha wabunifu pia kuwapa fursa ya kuonyesha uwezo wao katika matumizi ya teknolojia rafiki na rahisi zitakazoharakisha maendeleo ya viwanda nchini.

Pia Waziri Mkuu Majaliwa amesema SIDO inapaswa kujielekeza katika kubuni mashine , mitambo na teknolojia rahisi zitakazotumika kuongeza thamani ya bidhaa na kusisitiza kuwa  kutokana na umuhimu wa sekta ya viwanda nchini katika kukuza ajira na kuongeza pato la taifa serikali itaendelea kuweka miundombinu wezeshi itakayoharakisha kasi ya ukuaji wa viwanda.

“ Bila shaka nyote mnafahamu tumedhamiria kufikia uchumi wa kati kufikia mwaka 2025, ninaamini tunao uwezo wa kulifikia lengo hili, sasa tunachotakiwa kufanya kuhakikisha halmashauri zetu zote zinatenga maeneo maalumu kwa ajili shughuli za viwanda kama mlivyofanya hapa Simiyu, lakini pia lazima mhakikishe mnawajengea uwezo wajasiliamali ili waweze kuingia katika soko la ushindani, alisisitiza Waziri Mkuu Majaliwa”.

Waziri Mkuu Majaliwa  amewasisitiza SIDO waendelee kubuni mikakati itakayoleta mabadiliko katika sekta ya viwanda huku akiwataka wananchi kuthamini bidhaa zinazotengenezwa hapa nchini ambazo tayari zimeonyesha kukidhi mahitaji ya soko.

Halikadhalika waziri Mkuu Majaliwa ameziagiza halmashauri za wilaya nchini kuendelea kutekeleza agizo la kutenga 10%  ya mapato yake ya ndani kwa ajili ya mikopo ya wanaweke, vijana na walemavu huku  akiwasisitiza madiwani katika halmashauri zote nchini kuhakikisha wanasimamia utekelezaji wa agizo hilo.

Katika hatua nyingine Waziri Mkuu Majaliwa ameupongeza uongozi wa mkoa wa Simiyu kwa kujenga mahusiano mema na wananchi, viongozi  wa kisiasa pamoja na taasisi mbalimbali jambo ambalo amesema ni chachu ya kuharakisha maendeleo ya kiuchumi na kijamii mkoani Simiyu.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Kuhudumia Viwanda vidogo(SIDO), Prof. Sylvester Mpanduji amesema Shirika hilo litaendelea kutoa mafunzo kwa wajasriamali ili kuwajengea uwezo zaidi, ambapo amebainisha kuwa katika mwaka wa fedha 2017/2018 SIDO imetoa mafunzo kwa wajasiriamali 16,900.

Aidha, Prof. Mpanduji ameishukuru Serikali kwa kutenga shilingi bilioni 29 katika mwaka wa fedha 2018/2019 ambazo zitasaidia kutatua changamoto mbalimbali za wajasiriamali ikiwemo upatikanaji wa mashine mpya zitakazotumika katika vituo vya SIDO vya kuendeleza viwanda, kukopesha wajasiriamali mitaji na kujenga miuondombinu mingi ya viwanda katika sehemu hapa nchini.

Naye Mkuu wa Mkoa  wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka amemhakikishia Waziri mkuu  kuwa  Mkoa huo utahakikisha unaendelea kutekeleza maagizo ya serikali ikiwemo agenda ya kitaifa ya Uchumi wa Viwanda kupitia Falsafa ya Wilaya Moja Bidhaa Moja.

“Simiyu ni Mkoa wenye ajenda na kazi yetu ni kutekeleza maelekezo na miongozo yote ya Serikali, tunatekeleza Sera ya Viwanda chini ya Falsafa ya Wilaya Moja Bidhaa Moja na sasa tunaenda kwenye utekelezaji wa Kijiji Kimoja Bidhaa Moja na sisi tunaamini Mapinduzi ya Viwanda yanaanza na SIDO” alisema Mtaka.

Maonesho hayo ya SIDO ambayo yanafanyika kwa mara ya kwanza mkoani Simiyu yamehudhuriwa na wajasiliamali zaidi ya 500  kutoka mikoa mbalimbali hapa nchini ambayo yanatarajiwa kuhitimishwa Oktoba 28, 2018.

MWISHO

KUPATA PICHA ZAIDI KUHUSU HABARI FUGUA KIUNGANISHI HIKI:-https://simiyuregion.blogspot.com/2018/10/waziri-mkuu-majaliwa-aitaka-sido.html

Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa