• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

Waziri Kairuki Atoa Wito kwa Wawekezaji Wazawa Kuchangamkia Fursa Za Uwekezaji Zilizopo na Kusajili Miradi ya Uwekezaji

Posted on: April 21st, 2019

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Uwekezaji, Mhe.  Angela Kairuki ametoa wito kwa chama cha wanataaluma na wajasiriamali wa Kanisa la Waadventista Wasabato  Tanzania (ATAPE) na wawekezaji wengine wazawa kuchangamkia fursa mbalimbali za uwekezaji zilizopo nchini na kusajili miradi  yao ya Uwekezaji katika Tume ya uwekezaji ya Taifa (TIC).

Kairuki ameyasema hayo wakati akifunga Mkutano wa 20 wa chama cha wanataaluma na wajasiriamali wa Kanisa la Waadventista Wasabato  Tanzania (ATAPE) Mjini Bariadi, ambapo amebainisha kuwa kwa mwaka huu 2019 wawekezaji wazawa zaidi ya asilimia 72 wamesajili miradi yao ya uwekezaji TIC.

“ Kwa mwaka huu peke yake tumepata wawekezaji wazawa waliosajili miradi yao ya uwekezaji TIC zaidi ya asilimia 72, hii inanipa faraja sana kama waziri wa nchi ninayesimamia uwekezaji ninapoona Watanzania wenzangu wanachangamkia fursa”

"Naomba mchangamkie fursa hizo kwa sababu wawekezaji wa nje tunapenda waje tu endapo watakuja kuungana nasi kwenye mtaji, kubadilishana nasi ujuzi na uzoefu " alisema Kairuki.

Ameongeza kuwa Serikali imeendelea kuboresha mazingira ya biashara, uwekezaji na kuweka vipaumbele kwa ajili ya kuvutia wawekezaji katika sekta ambazo zitakuwana athari na tija kubwa kiuchumi kwa wananchi, ili kuimarisha minyororo ya thamani katika kilimo,uvuvi, na mifugo ambayo ni maeneo yanayoajiri Watanzania wengi zaidi.

Aidha, Waziri Kairuki amezitaja sekta nyingine za kipaumbele kuwa ni  uzalishaji wa mafuta ya kula kwa kutumia mbegu zinazozalishwa nchini, uzalishaji wa sukari, uzalishaji wa dawa za binadamu, vifaa tiba na kemikali, ujenzi wa miundombinu ya uvuvi wa kisasa, viwanda vya kuchakata samaki, kusindika nyama, viwanda vya kubangua korosho, viwanda vitakavyotumia pamba na viwanda vya  pembejeo na mbolea.

Katika hatua nyingine Waziri Kairuki ameipongeza ATAPE kwa jinsi inavyoshirikiana na Serikali katika kutoa huduma mbalimbali za kijamii ikiwemo sekta ya afya, elimu, maji pamoja na huduma nyingine.

Kairuki amesema serikali pekee haiwezi kutatua changamoto zote hivyo kwa kushirikiana na wadau ikiwemo taasisi za dini wanaweza kuwahudumia wananchi na kuleta mabadiliko chanya ikiwa ni pamoja na kuhubiri amani, huku akisisitiza kuwa masomo ya ujasiriamali yanayotolewa kwa wana ATAPE wayatumie kwa manufaa ya kanisa na jamii kwa ujumla.

Awali akimkatibisha waziri Kairuki, mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka amesema mkutano huo umewasaidia watu wa Simiyu kukutana na watu wa maeneo mengine hatua iliyopelekea kubadilishana uzoefu sambamba na kuongeza na kupata masoko mapya .

‘’watu wetu wameongeza wigo wa masoko, mmebadilishana uzoefu ....huu ni mkoa wa kibiashara na ni mkoa wenye fursa nyingi;  tunajenga tawi la chuo cha usimamizi wa fedha (IFM) hivyo ninawaalika wafanyabiashara na Watanzania wote kuja kuwekeza ujenzi wa hosteli eneo lile linalojengwa tawi hilo"alisisitiza Mtaka.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa ATAPE Freddie Manento amesema kwa miaka mitatu ATAPE imewekeza miradi ya bilioni 1.2 katika miradi yenye manufaa kwa kanisa, wanajamii na wana ATAPE.

Alisema wamewekeza kwenye miradi ya maji kwenye maeneo yenye uhitaji mkubwa, miradi ya miti ya matund), korosho na miradi ya mashamba ya mihogo kwa kutengeneza ajira na faida katika vijiji walivyolima mashamba yao.

‘’Wana ATAPE wamejitoa kwelikweli na wameitikia dhana yetu ya kutumia vipaji na rasilimali zetu kwa ajili ya kazi ya MUNGU, hii iko katika mathayo 28;19, 20…hii ndio dhana yao’’ alisema Manento.

Mkutano wa Wanataaluma na Wajasiriamali (ATAPE) kutoka kanisa la Waadventista Wasabato umefanyika mkoani Simiyu kwa muda wa siku sita ambapo umehudhuriwa na wananchama zaidi ya 1500.

.....MWISHO....

KUPATA PICHA ZAIDI FUNGUA KIUNGANISHI HIKI:https://simiyuregion.blogspot.com/2019/04/waziri-kairuki-atoa-wito-kwa-wawekezaji.html

Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa