• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

Waziri Jafo Aagiza Wakuu wa Mikoa Nchini Kuhamasisha Wananchi Kujiunga Mfuko wa Afya ya Jamii

Posted on: July 5th, 2018

Waziri wa Nchi  Ofisi ya Rais   Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(OR-TAMISEMI) Mhe.Selemani  Jafo amewaagiza Wakuu wa Mikoa nchini kuweka mpango mkakati wa kuwahamasisha wananchi kujiunga na Mfuko wa Afya ya Jamii (CHF) ulioboreshwa kama alivyofanya  Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe. Anthony Mtaka, ili kuwapunguzia gharama za matibabu.

Mhe. Jafo alitoa agizo hilo wilayani Busega mkoani Simiyu katika hafla ya kupokea Majengo ya wodi ya wazazi na chumba cha upasuaji  katika Kituo cha Afya NASA, ikiwa ni moja ya vituo vya Afya 38 mkoani Simiyu, pamoja na magari tisa yakiwepo magari matatu ya kubebea wagonjwa (Ambulance) na magari Sita kwa ajili ya uratibu wa huduma za Afya  yaliyopatikana chini ya ufadhili wa  UNFPA/KOICA , msaada uliogharimu jumla ya shilingi bilioni 5.52.

 “Agenda yako Mkuu wa Mkoa wa Simiyu ya kuhakikisha wananchi wote wanajiunga na Bima ya Afya, wewe utakuwa Mkuu wa Mkoa Kinara ndani ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kupitia mkutano huu niwaagize wakuu wa mikoa wote wahakikishe wanakuja na mpango wa kuwasaidia wananchi wao kupitia mikakati  watakayoibuni, kuwa kila mwananchi anakuwa na bima ya afya kupitia CHF iliyoboreshwa” alisema Jafo.

Awali akikagua  jengo la wodi ya wazazi na jengo la upasuaji katika kituo cha Nasa Waziri Jafo amepongeza viongozi wa Wilaya ya Busega na Mkoa wa Simiyu kwa kusimamia na kuhakikisha majengo hayo yanajengwa katika viwango bora kwa kutumia “Force Account” na kuwataka wananchi kuyalinda na kuyatunza majengo hayo.

Mhe. Jafo amewataka Waganga  Wakuu wa Wilaya kuhakikisha wanatoa huduma za afya vizuri katika maeneo yao kwa kuhakikisha kuwa wanakagua vituo vyao mara kwa mara badala ya kukaa ofisini.

Aidha, amewataka kuboresha mazingira ya vituo vyote vya afya nchini kuhakikisha vinakuwa visafi, huku akisisitiza  kusimamia kufungwa kwa mfumo wa Kielektroniki wa Kukusanya Mapato,   ili kuhakikisha kuwa mapato hayapotei.

Mhe. Jafo, amewataka wataalamu wa afya kuhakikisha wanakusanya na kuwa na takwimu sahihi za watoto wanaozaliwa na kufariki ili kuwezesha Serikali kuwa na takwimu sahihi zitakazowezesha kupambanana tatizo  la vifo vya akina mama na watoto.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa Anthony Mtaka amewashukuru wafadhili Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia idadi ya watu duniani (UNFPA), kwa namna walivyoshirikiana na Serikali katika kuchangia kuboresha huduma za afya mkoani humo, ikiwa ni pamoja na kujenga vituo vya kutolea huduma za afya.

Kuhusu mkakati wa Mkoa juu ya Bima ya Afya, Mtaka amesema “Tungehitaji kuwa ni mkoa ambao kila mwananchi atafaidika na huduma zinazotolewa na  Hospitali na vituo vingine vya kutolea huduma za afya kwa kuwa na bima ya afya ili waweze kupata matibabu yao vizuri” .

Naye, Mkuu wa Idara ya Afya KOICA Tanzania Kira Thomas amesema pamoja na kufadhili ujenzi wa vituo vya afya mkoani Simiyu, mkakati wao ni kuhakikisha Zahanati 31 mkoani Simiyu zinapatiwa vifaa vya dharura kwa ajili ya kutoa huduma za dharura na kuongeza damu kwa mama wajamzito wakati wa kujifungua.

Akizungumza kwa niaba ya wananchi wa Busega Mbunge wa Jimbo la Busega Dkt. Raphael Chegeni amesema uwepo wa wodi ya wazazi na chumba cha upasuaji utatatua changamoto ya huduma za afya ya muda ya wananchi kutembea umbali mrefu kutafuta huduma na akaishukuru Serikali kwa kutenga shilingi Bilioni 1.5 kwa ajili ya ujenzi wa Hospitali ya wilaya.

MWISHO

Waziri wa Nchi  Ofisi ya Rais,  Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Mhe.Selemani  Jafo akitoa maelekezo mara baada ya kukagua chumba cha upasuaji katika Kituo cha Afya cha Nasa wilayani Busega mkoani Simiyu kabla ya kukabidhiwa jengo hili lilojengwa kwa ushirikiano kati ya Serikali na Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia idadi ya watu duniani (UNFPA

Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto  Dkt. Mpoki Ulisubisya akitoa maelezo juu ya vifaa tiba vilivyowekwa katika chumba cha upasuaji cha katika Kituo cha Afya Nasa, kabla ya jengo hilo kupokelewa na Waziri wa Nchi  Ofisi ya Rais,  Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(TAMISEMI), Mhe.Selemani  Jafo.

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka akitoa salamu za mkoa katika hafla ya makabidhiano Majengo ya wodi ya wazazi na chumba cha upasuaji  katika Kituo cha Afya NASA pamoja na magari tisa yakiwepo matatu ya kubebea wagonjwa na magari Sita kwa ajili ya uratibu wa huduma za Afya,  yaliyotolewa na UNFPA chini ya ufadhili wa KOICA mkoani humo.

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka akizungumza na Mkurugenzi Mkaazi wa UNFPA Bi. Jacqueline Mahon hafla ya kupokea Majengo ya wodi ya wazazi na chumba cha upasuaji  katika Kituo cha Afya NASA pamoja na magari tisa yakiwepo matatu ya kubebea wagonjwa na magari Sita kwa ajili ya uratibu wa huduma za Afya  yaliyotolewa na UNFPA chini ya ufadhili wa KOICA kwa mkoa wa Simiyu.

Waziri wa Nchi  Ofisi ya Rais   Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Mhe.Selemani  Jafo (kulia) na Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka wakiteta katika  hafla ya kupokea Majengo ya wodi ya wazazi na chumba cha upasuaji  katika Kituo cha Afya NASA pamoja na magari tisa yakiwepo matatu ya kubebea wagonjwa na magari Sita kwa ajili ya uratibu wa huduma za Afya,  yaliyotolewa na UNFPA chini ya ufadhili wa KOICA kwa mkoani humo.

Baadhi ya wananchi wa Kijiji cha Nasa wilayani Busega Mkoani Simiyu wakisikiliza Waziri wa Nchi  Ofisi ya Rais   Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Mhe.Selemani  Jafo(hayupo pichani) katika  hafla ya kupokea Majengo ya wodi ya wazazi na chumba cha upasuaji  katika Kituo cha Afya NASA pamoja na magari tisa yakiwepo matatu ya kubebea wagonjwa na magari Sita kwa ajili ya uratibu wa huduma za Afya,  yaliyotolewa na UNFPA chini ya ufadhili wa KOICA kwa mkoani humo

Waziri wa Nchi  Ofisi ya Rais   Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe.Selemani  Jafo (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa wizara ya Afya, TAMISEMI, mashirika na wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wa Simiyu baada ya kupokea Majengo ya wodi ya wazazi na chumba cha upasuaji  katika Kituo cha Afya NASA pamoja na magari tisa yakiwepo matatu ya kubebea wagonjwa na magari Sita kwa ajili ya uratibu wa huduma za Afya,  yaliyotolewa na UNFPA chini ya ufadhili wa KOICA kwa mkoani humo


Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa