• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

Waziri Jafo Aagiza Hospitali Za Wilaya Kukamilika Julai 30, 2019

Posted on: July 14th, 2019

Waziri wa nchi ,Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Seleman Jafo ametoa agizo kuwa ifikapo Julai 30, 2019  hospitali zote za wilaya zinazojengwa nchini ziwe zimekamilika .

Jafo ameyasema hayo akiwa kwenye ziara ya siku moja mkoani Simiyu ambapo alitembelea miradi mbalimbali ukiwemo wa ujenzi wa  hospitali ya wilaya ya Itilima,. ujenzi wa barabara ,ujenzi wa kiwanda cha chaki na ujenzi wa kituo cha mabasi(stendi) cha kisasa, huku akipongeza ujenzi wa hospitali ya wilaya ya Itilima kwa kizingatia viwango, mahitaji na ubora katika ujenzi.

Aidha amesema kuwa hakuna sababu za fedha kuongezwa kiasi kilichotolewa awali kwa ajili ya ujenzi wa majengo saba ya awali kinatosha kukamilisha huku akitolea mifano ya hospitali ambazo zimeshakamilika kwa kiasi hicho kilichotolewa awali.

Akiwa wilaya za Meatu na Maswa waziri Jafo amekagua na kuridhishwa na ujenzi wa barabara zilizojengwa na mkandarasi CHICO kwa kiwango cha lami ikiwa ni utekelezaji wa ahadi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt John Pombe Magufuli aliyoitoa akiwa ziarani mkoani hapo zenye urefu wa kilometa tatu( kilometa moja na nusu kwa kila wilaya)

“Nikupongeze sana mratibu wa TARURA Mhandisi Dkt Philimon Msomba kwa kazi hii nzuri kikubwa wananchi  muutunze mradi huu ,kwanza nimefarijika sana kukuta hadi taa za barabarani zipo hongereni sana ”alisema waziri Jafo.

Kwa upande wake Mbunge wa Maswa Mashariki ambaye pia ni Naibu Waziri wa Madini Mhe.Stanslaus Nyongo amemuomba Waziri Jafo kabla mkandarasi hajaondoa vifaa vyake eneo la ujenzi wa barabara ni bora ukafanyika mchakato wa kuongeza kiasi kingine cha pesa kwa ajili ya kilometa 1.5 zilizobaki.

Katika hatua nyingine akiwa Mjini Bariadi Waziri Jafo ameridhishwa na ujenzi wa kituo cha mabasi kinajengwa Mjini hapo na kumtaka mkandarasi Kampuni ya Halem and Kings Builders Co Ltd kutoka Dar es salaam kukamilisha ujenzi  ifikapo Septemba 2, 2019 ambapo kwa sasa umefikia asilimia 87 na mpaka kukamilika kwake ujenzi utagharimu kiasi cha shilingi bilioni 7.2

Pamoja na hayo waziri Jafo alitembelea ujenzi wa kiwanda cha chaki na kiwanda cha vifungashio unaoendelea wilayani Maswa na kupata taarifa ya ujenzi huo ambao ulipaswa kukamilika Augost 7 lakini mkandarasi SUMA JKT kaomba kuongezewa muda hadi sept 22 ,2019 kwa kile alichodai awali walipata changamoto zilizopelekea kuchelewa kuanza .

“kwenye taarifa yenu ujenzi huu ulipaswa kukamilika lakini hapa mnasema muongezewe muda ,mradi una lengo maalum na mkakati kiwanda kikamilike kianze kutoa products(bidhaa), mimi niwahakikishie ntakuja hapa tarehe 22 au 23 kujihakikishia kama kweli ujenzi huo umekamilika ” alisema waziri Jafo

Wakiongea kwa niaba ya wananchi Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinguzi (CCM) wilaya ya Maswa Mhandisi. Paul Jidayi na Mkuu wa Wilaya ya Meatu Dkt. Joseph Chilongani wameishukuru Serikali kutoa fedha kwa ajili ya kutekeleza ahadi ya Mhe. Rais na kubainisha kuwa watashirikiana na wananchi kuhakikisha kuwa miundombinu hiyo inatunzwa.

MWISHO

KUPATA PICHA ZAIDI FUNGUA KIUNGANISHI HIKI:-https://simiyuregion.blogspot.com/2019/07/waziri-jafo-aagiza-hospitali-za-wilaya.html

Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa