• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

Wazazi Wenye Watoto Walio Madarasa ya Mitihani Wapunguzieni Kazi Wajisomee: RC Mtaka

Posted on: May 7th, 2021

Mkuu wa mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka ametoa rai kwa wazazi na walezi wenye watoto walio katika madarasa ya mitihani ya Taifa kuwapunguzia kazi ili wanafunzi hao waweze kupata muda wa kujiandaa na mitihani hiyo na hatimaye waweze kufanya vizuri katika mitihani yao.

Mtaka ameyasema hayo Mei 06, 2021 Mjini Bariadi wakati wa futari maalum iliyoandaliwa na ofisi yake kwa ajili ya waumini wa dini na Kiislamu walio katika mwezi mtukufu wa Ramadhani ambayo pia iliwahusisha viongozi na watendaji mbalimbali wa Serikali mkoani  Simiyu.

“Matarajio yangu ni kuhakikisha kuwa mkoa huu unabaki kuwa miongoni mwa mikoa mitano inayofanya vizuri kwenye elimu nchini, kwenye malengo yetu ya mwaka huu ni kuona tunatoka kwenye nafasi ya tano, kwenda nafasi ya tatu na kufikia nafasi ya kwanza ili kufikia hapo tuna kazi ya kufanya; niwaombe wazazi na walezi wote wa mkoa wa Simiyu wenye watoto wa madarasa ya mitihani wawapunguzie kazi ili wapate muda wa kujisomea na kufanya matayarisho ya mitihani yao ya Taifa,” alisema Mtaka.

Aidha, Mtaka amewataka wazazi kutowaruhusu wanafunzi kwenda katika minada kufanya biashara badala yake wahakikishe wanafunzi wote wanahudhuria masomo, “ Hii habari ya kuona watoto (wanafunzi) minadani hapana, kila mmoja awe mzazi na mlezi minada ni kwa ajili ya wazazi kufanya biashara siyo mahala kwa watoto kupeleka bidhaa maana minada yetu mingi inafanyika siku za kazi”

Kwa upande wake Sheikh wa Mkoa wa Simiyu Mahamudu Kalokola amemshukuru Mkuu wa Mkoa wa Simiyu kwa futari na kushiriki katika shughuli mbalimbali zinasowahusu Waislamu ikiwa ni pamoja na kushiriki katika ujenzi wa msikiti mkuu wa Bariadi , huku akiwataka Waislamu wote mkoani Simiyu kuendelea kuiombea nchi na kudumisha amani iliyopo.

Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Amani ya mkoa wa Simiyu,Askofu Marco Maduhu ametoa rai kwa wananchi mkoani Simiyu kuendelea kushirikiana na kuthaminiana bila kujali tofauti za dini zao.

Naye Katibu wa CCM mkoa wa Simiyu, Bi. Haula Kachwamba amewatakia heri Waislamu wote walio katika mfungo wa mwezi mtukufu wa Ramadhani na kuwaombea waweze kumaliza mfungo huo salama.

MWISHO

 KUPATA PICHA ZAIDI FUNGUA KIUNGANISHI HIKI:-https://simiyuregion.blogspot.com/2021/05/wazazi-wenye-watoto-walio-madarasa-ya.html

Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa