• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

Wastaafu Wawaasa Watumishi Kufanya Kazi kwa Kujituma

Posted on: April 14th, 2021

Watumishi waliostaafu wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wamewaasa watumishi wa Umma kufanya kazi kwa bidii, uaminifu na kujituma ili waweze kutekeleza majukumu yao vizuri na kumaliza salama safari yao ya utumishi wa Umma.

Rai hiyo imetolewa kwa nyakati tofauti katika hafla ya kuwaaga iliyoandaliwa na Katibu Tawala wa Mkoa ambayo iliyofanyika Aprili 13, 2021 Mjini Bariadi.

“Nawasihi Watumishi wenzangu mfanye kazi kwa kujituma na muwe makini katika utendaji kazi wenu ili mtoe huduma inayotakiwa kwa watu mnaowahudumia,” alisema Dkt. Mugune Maeka ambaye alistaafu utumishi wa Umma akiwa Daktari msaidizi Mkuu

“Ninawashukuru kwa ushirikiano mlionionesha siku zote nilizofanya kazi nanyi, nawaomba watumishi mtimize wajibu wenu na muwe na subira mnapokutana na changamoto mbalimbali katika utumishi wao,” alisema Gamitwe Mahaza ambaye amestaafu utumishi wa Umma akiwa Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Uchumi na uzalishaji

“Ninawashukuru sana viongozi wetu kuona umuhimu wa kutuaga baada ya kukoma kwa utumishi wetu, niwaombe watumishi mfanye kazi kwa utii na uaminifu ili muweze kumaliza vema safari yenu ya Utumishi wa Umma,” alisema Joseph Milando ambaye amestaafu watumishi wa umma akiwa Mlinzi.

Kwa upande wake Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Utawala na Rasilimali watu, Bw. Ekwabi Mujungu amewapongeza wastaafu hao kwa utumishi wao uliotukuka kwa kuwa wakati wakiwa watumishi hawajawahi kuwa rekodi yoyote ya utovu wa nidhamu wala tuhuma zozote na kuwataka watumishi wengine kuiga mfano wao.

Naye Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa, Bw. Donatus Weginah amewashukuru wastaafu hao kwa kuwa na mchango mkubwa katika kufikia ndoto ya mkoa huku akiwapongeza kwa kuwa watumishi wa mfano wenye utumishi uliotukuka.

Wastaafu hao ni pamoja na Bw. Rauden Mwamwaja ambaye amekuwa mtumishi wa Umma kwa miaka 38 amestaafu akiwa dereva mwandamizi, Dkt. Mugune Maeka amekuwa mtumishi wa Umma kwa miaka 37 amestaafu akiwa Daktari Mkuu msaidizi, Dkt. Gamitwe Mahaza ametumikia Umma kwa miaka 36 amestaafu akiwa Katibu Tawala msaidizi Sehemu ya Uchumi na Uzalishaji, Bw. Joseph Milando ametumika miaka 21 kama mlinzi na Bw. Leonard Malulu ambaye amefanya kazi kwa miaka 34 na amestaafu akiwa Msaidizi wa Ofisi Mwandamizi.

Katika hafla hiyo kila mstaafu alikabidhiwa cheti cha utumishi uliotukuka pamoja na fedha taslimu shilingi milioni moja (1,000,000/=), zawadi ambazo zimetolewa na Katibu Tawala wa Mkoa kwa lengo la kuwapongeza na kutambua mchango wao wakati wa utumishi wao.

MWISHO

KUPATA PICHA ZAIDI KUHUSU TUKIO HILI FUNGUA KIUNGANISHI HIKI:-https://simiyuregion.blogspot.com/2021/04/wastaafu-wawaasa-watumishi-kufanya-kazi.html

Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa