• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

Washindi wa Simiyu Jambo Festival Mwaka 2018 hawa Hapa

Posted on: July 8th, 2018

NAIBU spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Tulia Ackson, ametoa medali na pesa taslimu takribani milioni 25 kwa washindi wa mashindano ya mbio za baiskeli, mbio fupi, mashindano ya ngoma za asili (Wagika na Wagalu) na uandishi wa insha kwa shule za Sekondari katika Tamasha la Simiyu Jambo Festival lililofanyika katika Uwanja wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi Mkoani Simiyu

Katika mashindano ya baiskeli wanaume (kilometa 150) Richard Laizer kutoka Arusha aliibuka kidedea na kuwa  mshindi wa kwanza na kujinyakulia kitita cha shilingi 1,200,000/= , huku upande wa wanawake(KM 100 ) Laulensia Ruzuba wa Mwanza aliyekimbia km 100 na kujishindia  kiasi cha shilingi 1,000,000/=.

Mshindi wa pili (wanaume)Hamisi Hussein kutoka Arusha aliyekimbia Kilometa 150 kwa saa 4:56:51 alijishindia kiasi cha Sh. Milioni 1,000,000/= ambapo mshindi wa tatu Hamisi Hatari ambaye alikimbia kwa saa 4:56:52 alipata  sh.800,000.

Aidha, kwa upande wa wanawake  Elizabeth Mwinamila kutoka Mkoa wa Simiyu ambaye alikimbia Km 100 kwa saa 3:10:58 alipata kiasi cha Sh. 800,000 akifuatiwa na Sophia Adson kutoka Arusha ambaye alikimbia kwa saa 3:15:47.

Kwa upande wa mbio za baiskeli walemavu washindi wote walitoka Mkoa wa Simiyu,majina yao na zawadi zikiwa kwenye mabano ni Saguda Ngulima(500,000), Emmanuel John (400,000) na Saguda Sospeter (300,000) na Mpingi Ngolo (150,000).

Katika mbio fupi kilometa 10 zilizoshirikisha  wachezaji kutoka  Tanzania na nchi jirani  ya Kenya mshindi wa kwanza Joseph Mbatha wa  Kenya alikimbia Km 10 alipata kiasi cha Sh.Milioni 1,000,000/= na medali ya dhahabu.

Nafasi ya pili ilikwenda kwa Tanzania kwa Fabian Sulle ambaye alijinyakulia Sh.800,000 wa tatu alitoka Kenya Abraham Atoo ambaye alipewa Sh. 700,000.

Kwa upande wa wanawake nafasi ya kwanza mbio fupi za  Km. 10 ilikwenda pia nchini Kenya kwa Esther Chesenga ambaye alijipatia  kiasi cha Milioni 1, nafasi ya pili ilikwenda Tanzania kwa Failuna Matanga ambaye  alipata medali na kiasi cha sh. 800,000, nafasi ya tatu ilikwenda kwa Faith Kipsun kutoka Kenya..

Kwa upande wa wanafunzi ambao walikimbia Km 2.5  nafasi ya kwanza ilichukuliwa na Saimon Marco kutoka Mkoa wa Mara ambaye alipata Sh.50,000 Lucia Mochemba kutoka Mara aliyepata pia sh. 50,000.

Nafasi ya pili ilikwenda Mkoa wa Simiyu kwa  Kundi Gambo na Juma Benjamini na kupata Sh.40,000 washindi wa tatu walitoka Mkoa wa Mara kwa Veronica Samweli na Karebo Joseph, wao walipata Sh.30,000.

 Kwa upande wa mbio za Km 5 washindi Mkoa wa Simiyu ulionekana kufanya vizuri zaidi  ambapo nafasi ya kwanza ilishikwa na Maganda John(50,000) , Masanja Saguda(40,000) na Masaba Lameck (30,000) wasichana ni Anastazia Mkama(50,000), Asha Daniel (40,000) na Lugendo (30,000) wa Mkoa wa Mara.

Katika mashindano ya uandishi wa insha ambayo yalishirikisha shule tano za Mjini Bariadi ambazo ni Kidinda, Mahaha, Bariadi, Biashara na Simiyu mshindi wa kwanza alikuwa ni Magese Mahega(Simiyu), wa pili Liku Mayombo na wa tatu akiwa Mathias Peter.

Washiriki wa mashindano ya mbio fupi Kilometa Tano wakianza mbio hizo katika eneo la Salunda mjini Bariadi wakati wa Tamasha la SIMIYU JAMBO FESTIVAL Mjini Bariadi, ambalo limehusisha mashindano ya ngoma za asili (Wagika na Wagalu), mbio za baiskeli(Kilomita 150 wanaume na kilomita 100 wanawake), mbio fupi(Kilomita 10 na Kilometa tano), uandishi wa insha, likiwa limeshirikisha washiriki kutoka  mikoa mbalimbali hapa nchini, nchi jirani ya Kenya.

Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa