• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

Wanufaika wa TASAF watakiwa kubuni Miradi kujiongezea Kipato

Posted on: April 11th, 2017

Wanufaika wa Mpango wa kunusuru kaya maskini TASAF III wametakiwa kubuni miradi midogo midogo kwa kutumia fedha wanazopata ili kujiongezea kipato.

Wito huo umetolewa na Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu, Ndg. Jumanne Sagini wakati wa ziara yake wilayani Itilima ya kukagua visima vya maji ambavyo ni miongoni mwa miradi  ya kutoa ajira za muda kwa walengwa wa Mpango wa kunusuru kaya Maskini TASAF III.

Sagini amesema wanufaika wa TASAF ikiwa ni pamoja na waliopata ajira za muda katika uchimbaji wa Visima na kulipwa ujira  kidogo watumie fedha hizo kujikimu na kuanzisha miradi midogo midogo ikiwemo ya biashara ndogo ndogo na ufugaji wa kuku, bata, mbuzi na kondoo.

“ Mradi huu hautadumu milele nawashauri katika kidogo mnachokipata mkitumie vizuri,  anzisheni miradi midogo midogo itakayowasaidia kuboresha kipato katika kaya zenu, wenye uwezo wa kufuga wafuge, wenye uwezo wa kufanya biashara ndogo ndogo wafanye”

Mwenyekiti wa kijiji cha Nanga Dismas Lyang’ombe amesema baadhi ya wanufaika wa mradi wa TASAF waliohusika katika ujenzi wa visima vinne vilivyojengwa na Serikali kupitia Mradi wa TASAF kwa kushirikiana na wananchi na kupewa ujira wa shilingi 2300 kwa siku, wameonesha mabadiliko katika kaya zao tofauti na ilivyokuwa awali, ikiwa ni pamoja na kufuga kuku, mbuzi na kuezeka nyumba zao kwa bati.

Aidha,  Lyang’ombe ameishukuru Serikali kwa kujenga visima hivyo kwa kuwa vimewasaidia wananchi wake kupata huduma ya maji katika umbali mfupi

Kwa upande wao wananchi wa vijiji vya Nguno, Nanga na Laini B vyote vya Wilaya ya Itilima alivyovitembelea Katibu Tawala Mkoa Simiyu, wameomba Serikali hiyo kutibu maji yanayopatikana katika visima hivyo ili wapate maji safi na salama.

Akijibu hoja hiyo, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Itilima, Ndg. Mariano Mwanyigu amesema  Halmashauri yake itaandaa utaratibu mzuri wa kitaalam  kupitia wahandisi wa maji kuhakikisha maji yanatibiwa na wananchi wanapata maji safi na salama.

 Miradi ya ajira za muda kwa wanufaika wa Mradi wa TASAF  hutekelezwa katika kipindi kigumu kiuchumi ili kuwasiadia wanufaika hao na katika wilaya ya Itilima imeanza kutekelezwa mwezi Disemba 2016 hadi Machi   2017.

Jumla ya miradi 161 imeibuliwa katika vijiji 65 vilivyo kwenye mpamgo, katika kipindi cha kwanza cha utekelezaji wa miradi ya kutoa ujira ni visima 161 vinavyotakiwa kukamilishwa  na visima 95 vimekamilika vinatoa maji, 66 viko katika hatua ya kufunikwa na vinatoa maji.

Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa