• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

Wananchi Zaidi ya 300,000 Kunufaika na Ujenzi la Hospitali ya Wilaya

Posted on: May 25th, 2019

Jumla ya wakazi 346,365 wa Wilaya ya Itilima na maeneo ya jirani wanatarajia kunufaika na ujenzi wa mradi wa hospitali ya Wilaya ya Itilima inayotarajiwa kukamilika Juni 30 mwaka 2019.

Mradi huo wenye lengo la kuimarisha upatikanaji wa huduma za afya na kusogeza karibu huduma hiyo kwa wananchi ,hadi kukamilika kwake unatarajia kutumia kiasi cha sh bil 1 .5.

Akisoma taarifa ya mradi wa Ujenzi wa Hospital ya Wilaya ya Itilima kwa kiongozi wa mbio za mwenge wa Uhuru mwaka 2019,Mzee Mkongea Ali ,mganga mkuu wa Wilaya hiyo Dk Anorld Charles amesema kuwa kukamilika kwa mradi huo kutarahisisha huduma za wananchi wa Wilaya humo.

Dk Charles ameeleza kuwa wananchi wengi wa Wilaya hiyo wamekuwa wakitembea umbali mrefu wa wastani wa kilometa 45 hadi 50 kufuata huduma za afya katika hospitali ya Bariadi.

Amesema kutokana na hali hiyo ya kutembea umbali mrefu,wengi wao hupoteza maisha kwa kukosa huduma stahiki za haraka hususani akinamama wajawazito ambao wengi wao hupoteza damu nyingi njiani.

Ameongeza kuwa endapo hospitali hiyo itakamilika kwa muda muafaka,itasaidia sana kupunguza vifo vya akinamama wajawazito wanaopoteza damu nyingi pindi wawapo njiani kuelekeza katika hospitali ya wilaya ya Bariadi.

Amesema kwa mwaka 2018 (Jan hadi Dec) pekee jumla ya akinamama 5 walipoteza maisha kwa kuvuja damu nyingi kwa kucheleweshwa kufika mapema katika zahanati na hospitali zilizo karibu nao.

Naye kiongozi wa mbio za mwenge wa Uhuru kitaifa mwaka 2019 Ndg. Mzee Mkongea Ali alisema kuwa jitihada za Ukamilishaji wa hospitali hiyo zinatakiwa ziwe za haraka iwezekanapo kabla ya kuisha mwaka wa fedha, kwani endapo wakishindwa kukamilisha kwa muda husika hawataweza kupata fedha za ukamilishaji huo.

" napenda kuwashauri kuwa ukamilishaji wa hospitali hiyo unatakiwa uwe Juni 30 mwaka huu kama ilivyoelekezwa hivyo ni lazima ujenzi uende kwa haraka usiku na mchana...la sivyo mwaka ya fedha 2018/2019 utakapomalizika itakuwa vigumu kupata fedha hizo zilizokuwa zimetengwa katika bajeti ya 2018/2019.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Itilima, Mhe. Benson Kilangi amesemaViongozi wilayani humo watahakikisha Hospitali hiyo inakamilika kabla ya juni 30, 2019 kama ilivyoelekezwa na Waziri wa nchi, Ofisi ya Rai TAMISEMI.

Marangwa Maduhu mkazi wa kijiji cha Nguno Wilayani humo,amesema uwepo wa hospitali hiyo itawasaidia sana kupunguza gharama za usafiri walizokuwa wakizitumia kufuata matibabu Wilayani Bariadi.

Mpaka sasa ujenzi wa hospitali ya Wilaya ya Itilima tayari imeshatumia kiasi cha sh bil 1.2 sawa na asilimia 81 ya utekelezaji wake

Katika hatua nyingine kiongozi wa mbio za mwenge wa Uhuru kitaifa mwaka 2019 Ndg. Mzee Mkongea Ali ametoa wito kwa wananchi kutunza vyanzo vya maji kwa kupanda miti rafiki katika vyanzo vya maji na kusisitiza wale wote ambao watakiuka sheria wachukuliwe hatua.

MWISHO

KUPATA PICHA ZAIDI FUNGUA KIUNGANISHI HIKI:-https://simiyuregion.blogspot.com/2019/05/wananchi-zaidi-ya-300000-kunufaika-na.html

 

 

Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa