• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

Wananchi wahimizwa kwenda Kushuhudia Mashindano ya Baiskeli na Ngoma za Asili Agosti 06

Posted on: August 5th, 2017

Wananchi Mkoani Simiyu wamehimizwa kwenda kushuhudia mashindano ya Baiskeli na Ngoma za Asili yatakayofanyika kesho Jumapili katika Uwanja wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi.

Akizungumza na Waandishi wa Habari Mratibu wa Mashindano hayo yanayotambulika kama Simiyu Jambo Festival ambayo yanadhaminiwa na Kampuni ya Jambo Food Products, Ndg.Kulwa Mtebe amesema washiriki wa mbio za baiskeli kutoka mikoa mbalimbali wameshawasili Mjini Bariadi na wamejiandaa vizuri kwa ajili mashindano.

Aidha, amesema Mgeni Rasmi katika tukio hilo(Simiyu Jambo Festival) la Kihistoria Mkoani Simiyu ambaye ni Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe.Dkt.Tulia Ackson ameshawasili Mkoani kwa ajili ya mashindano hayo.

Mkuu wa Usalama Barabarani Mkoa wa Simiyu, Edson Mwakihaba amesema Jeshi la Polisi Kikosi cha Usalama Barabarani limejipanga kikamilifu kuhakikisha kwamba watumiaji wa barabara wanazingatia sheria za usalama barabarani na askari watakuwepo katika vituo vyote ambavyo washiriki wa mbio za baiskeli watapita.

Rais wa Chama cha Baiskeli Taifa Godfrey Mhagama amesema Chama hicho kupitia kamati yake ya Ufundi kitakahikisha kanuni na taratibu za mchezo wa mbio za baiskeli zinasimamiwa na kufuatwa katika mashindano hayo.

Mhagama ameongeza kuwa Wachezaji wahakikishe wanacheza katika viwango vinavyotakiwa kwa kuwa vigezo vyote vitavyozingatiwa ikiwa ni pamoja na kasi ya mchezaji na muda anaoutumia katika kukamilisha mbio kwa umbali uliopangwa, ambayo pia itakuwa ni njia ya kupata wachezaji wanaoweza kuwakilisha Taifa katika Mashindano ya Olimpiki.

Kwa upande wake Meneja Masoko wa Kampuni ya Jambo Food Products Anthony Paul amewahakikishia washiriki kuwa zawadi zote zilizopangwa kwa washindi katika makundi yote matatu (wanaume, wanawake, walemavu) ziko tayari ambayo ni pikipiki itakayotolewa kwa mshindi wa kwanza(wanaume) na fedha taslimu zaidi ya shilingi Milioni nane zitakazotolewa kwa washindi wengine.

Naye Emmanuel Mollel mshiriki wa mashindano ya mbio za Baiskeli kutoka mkoa wa Arusha amesema washiri kutoka katika mkoa huo wamejipanga kikamilifu na kiushindani kuhakikisha wanapata ushindi.

Tatu Malulu mshiriki wa mbio za Kilometa 80 kutoka katika Mkoa wa Mwanza amesema amekuwa akifanya mazoezi siku zote ambayo yamemuimarisha hivyo akathibitisha kuwa kutokana na maandalizi hayo anatarajia ushindi na ametoa wito kwa Wachezaji kujenga utamaduni wa kufanya mazoezi siku zote maana ndio siri ya kufanikiwa kwao.

Zaidi ya washiriki 160 kutoka katika mikoa ya Simiyu, Shinyanga, Mwanza, Geita na Arusha wanatarajia kushiriki mashindano hayo ambayo yatagawanyika katika makundi matatu; wanaume Kilometa 200, wanawake Kilometa 80 na Watu wenye Uemavu Kilometa 05.

Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa