• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

Wananchi Simiyu Waipongeza Serikali Kuwajengea Mahakama

Posted on: June 23rd, 2020

Wananchi wa Wilaya ya Bariadi Mkoani Simiyu wameipongeza Serikali kwa kuwajengea mahakama ya Wilaya ya Bariadi na Mahakama ya Hakimu Mkazi Simiyu jambo ambalo limewapunguzia adha ya kutumia gharama na muda mrefu kwenda kufuata huduma za mahakama katika mkoa wa Shinyanga kama ilivyokuwa awali.

Akizungumza katika hafla ya uzinduzi wa jengo la mahakama ya Hakimu Mkazi Simiyu na Mahakama ya Wilaya ya Bariadi ambayo ilifanyika Juni 22, 2020 Mjini Bariadi, Bw. Zengila Nyoni mkazi wa Bariadi ameomba watumishi wa mahakama kutoa huduma kwa kuzingatia misingi ya haki ili umuhimu wa uwepo wa mahakama uonekane kwa wananchi.

“Tunaishukuru Serikali kutujenge jengo zuri la mahakama, sasa hivi hatutasafiri kwenda Shinyanga kufuata huduma za mahakama ya hakimu mkazi ni hapa hapa tu; niwaombe mahakimu na majaji kutoa haki kwa wananchi ili tufurahie uwepo wa jengo hili zuri, maana haitakuwa na faida kama tumejengewa jengo zuri halafu huduma zisiwe nzuri,”alisema Nyoni.

Awali akizungumza katika uzinduzi huo Jaji kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Dkt. Eliezer Feleshi amewashauri Wakuu wa Wilaya na Mikoa nchini  kutumia kamati za maadili za wilaya  na mikoa ambazo wao ni wenyeviti wa kamati hizo kuwajadili mahakimu ambao wanaenda kinyume na maadili ya utumishi wa Umma.

“ Ni aibu kwa Mkuu wa Wilaya au Mkuu wa Mkoa kusema kuwa hamtaki hakimu fulani kwenye eneo lake wakati  yeye ndiyo mwenyekiti wa kamati ya maadili ya wilaya au mkoa, mahakimu wasio waadilifu wafikisheni kwenye kamati za maadili, zile kamati zinajuimisha watu wengi wazuri; niendelee kuwasihi watumishi wa Mahakama kujiepusha na vitendo vilivyo kinyume na maadili,” alisema Jaji Feleshi.

Katika hatua nyingine Jaji Kiongozi amewaomba wakuu wa mikoa nchini kusaidia  Magereza mikoani mwao kupata vifaa vya TEHAMA ili kuunga mkono jitihada zinazofanywa na Mahakama ya Tanzania za kusikiliza mashauri kwa njia ya mtandao, ambapo amebainisha kuwa tayari vifaa vya TEHAMA vimeshawekwa kwenye mikoa mbalimbali nchini na endapo wadau hao wa Mahakama wataziwezesha Magereza, kazi hiyo itafanyika kwa urahisi.

Kwa upande wake Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Shinyanga, Mhe. Gerson Mdemu amesema ujenzi wa jengo la  mahakama ya wilaya ya Bariadi na Mahakama ya Hakimu Mkazi Simiyu, utasaidia kuokoa fedha iliyokuwa ikitumika kulipa pango na itatumika kutoa huduma katika maeneo mengine.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Mhe. Festo Kiswaga akitoa salamu kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka amesisitiza uadilifu kwa watumishi wa mahakama, huku akibainisha kuwa kujenga kwa mahakama kutawasaidia wananchi kupata huduma karibu na kuokoa rasilimali fedha na muda waliokuwa wakitumia kufuata huduma mkoa wa Shinyanga.

Akitoa taarifa ya ujenzi wa mahakama ya wilaya ya Bariadi na Mhakama ya Hakimu Mkazi Simiyu, Mtendaji wa Mahakama Mkoa wa Simiyu, Leonald Maufi amesema ujenzi umegharimu zaidi ya shilingi milioni 800.

MWISHO

KUPATA PICHA ZAIDI FUNGUA KIUNGANISHI HIKI:-https://simiyuregion.blogspot.com/2020/06/wananchi-waipongea-serikali-kuwahjengea.html

Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa