• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

Wanafunzi 18,306 Wachaguliwa Kidato cha Kwanza Mwaka 2019 Simiyu

Posted on: December 6th, 2019

Jumla ya wanafunzi 18,306 sawa na asilimia 73.5 kati ya 24,915 waliofanya mtihani wa darasa la saba mwaka 2019 wamechaguliwa kujiunga Kidato cha Kwanza katika awamu ya kwanza mwaka 2020 katika shule za Serikali za Bweni na Kutwa.

Akitangaza matokeo hayo Desemba 06, 2019 Mjini Bariadi Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu, Bw. Jumanne Sagini amesema idadi ya waliochaguliwa kujiunga kidato cha kwanza mwaka 2020 imeongezeka kwa wanafunzi 5900 sawa na asilimia 23.8 ikilinganishwa na wanafunzi 12,399 waliochaguliwa mwaka 2019.

Aidha, Sagini amezitaka Halmashauri mkoani Simiyu kukamilisha miundombinu inayohitajika ili wanafunzi 6609 watakaochaguliwa awamu ya pili waweze kuripoti shuleni kabla ya 15 Februari, 2020.

“Halmashauri kamilisheni miundombinu inayohitajika ili wanafunzi watakaochaguliwa awamu ya pili waweze kuripoti shule kabla ya tarehe 15 Februari 2020; nawasihi  wazazi na walezi wa wanafunzi 6609 waliokosa nafasi awamu ya kwanza kuwa wavumilivu wakati halmashauri zinaendelea kukamilisha miundombinu inayohitajika,” alisema Sagini.

Katika hatua nyingine Sagini amewapongeza wanafunzi wote waliopata nafasi ya kuchaguliwa kidato cha kwanza na kuwaasa wasifanye anasa watumie fursa hiyo kujifunza na hatimaye wakamilishe safari ya elimu, huku akiwashukuru wadau wote wa elimu wakiwemo wazazi na walimu kwa namna walivyochangia katika uendeshaji na utoaji wa elimu bora.

Ameongeza kuwa wanafunzi wote waliochaguliwa kidato cha kwanza wanapaswa kuripoti shuleni tarehe 06 Januari, 2019 huku akiwasisitiza wazazi, walezi na jamii kwa kushirikiana na viongozi wa wilaya kuhakikisha wanfunzi woe waliochaguliwa wanaripoti shuleni na kubaki shuleni mpaka watakapohitimu elimu ya kidato cha nne.

Naye Afisa elimu wa Mkoa, Mwl. Ernest Hinju amesema matokeo ya mwaka 2019 kwa darasa la saba mkoa umepata zaidi ya asilimia 86 na kuufanya mkoa kushika nafasi ya nane Kitaifa ikilinganishwa na mwaka jana ambapo mkoa ulishika nafasi ya 22 Kitaifa, jambo ambalo limeufanya mkoa kuwa miongoni mwa mikoa iliyofanya vizuri na kuwa katika nafasi 10 bora kitaifa kwa mitihani yote mikubwa mtihani wa darasa la saba, kidato cha nne(nafasi ya 9) na kidato cha sita (nafasi ya 10).

Nao baadhi ya wajumbe walitoa maoni yao kuhusu namna ya kuboresha elimu na kuwasaidia wanafunzi ambao hawajapata nafasi ya kujiunga na elimu ya sekondari ambapo walishauri ujenzi wa vyuo vya ufundi na kuongea jitihada katika michezo.

“ “Ninashauri  kila Halmashauri iweke mkakati wa kuwa na vyuo ufundi ili waanfunzi wanaokosa nafasi kujiunga na elimu ya sekondari wapate fursa ya kujifunza ufundi na waweze kujiajiri na kujikwamua kimaisha,’ alisema Afisa Elimu Taaluma Halmashauri ya Wilaya ya Itilima, Mwl. Juma Athuman.

“Moja ya sababu zinazochangia kushusha kiwango cha ufaulu kwa wanafunzi ni utoro, napendekeza kuwa ili kukabiliana na tatizo la utoro Halmashauri zione haja ya kuimarisha miundombinu ya michezo; wanafunzi wengi wanaopenda michezo wanajituma pia na darasani ushahidi ninao, wanamihezo wanaofanya vizuri kwenye riadha ndani ya mkoa wetu wanafanya vizuri kitaaluma,” alisema Yohana Misese.

MWISHO

KUPATA PICHA ZAIDI FUNGUA KIUNGANISHI HIKI:-https://simiyuregion.blogspot.com/2019/12/wanafunzi-18306-wachaguliwa-kidato-cha.html

Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa