• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

Wakurugenzi Watakiwa Kusimamia Idara ya Ardhi Kuhakikisha Inapima Maeneo na Kutoa Hati

Posted on: August 24th, 2017

Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe.Angelina Mabula  amewataka Wakurugenzi wa Halmashauri Mkoani Simiyu  kuwasimamia watumishi wa Idara ya Ardhi na kuhakikisha wanapima maeneo  na kutoa hati miliki kwa wananchi.

Mhe.Mabula ameyasema hayo wakati wa ziara yake Mkoani Simiyu ambayo imelenga kufuatilia utekelezaji wa maelekezo mbalimbali aliyoyatoa wakati wa ziara yake Novemba 2017, mwenendo wa ukusanyaji wa kodi za ardhi na  kukagua Jengo la Kanda ya Ardhi Simiyu itakayohudumia Mikoa ya Simiyu,Shinyanga na Mara,

“Mtumishi aliyeajiriwa kama surveyor (mpima ardhi) hana sababu za kukaa ofisini kuanzia saa 1:30 asubuhi mpaka saa 9:30 alasiri wakati kazi zake nyingi ziko uwandani; Mwisho atajikuta amepima viwanja 58 mwaka mzima, maana yake ni kwamba atakuwa hajajua wajibu wake, wakurugenzi badilikeni katika kuwasimamia watumishi wa sekta ya ardhi” amesema Mabula

Amesema ikiwa Watumishi wa Idara ya Ardhi wakitimiza wajibu wao Ardhi ikapimwa, wananchi wakapewa hati miliki ya maeneo yao ya viwanja na mashamba;  migogoro itapungua, Serikali itakusanya maduhuli kupitia kodi ya Ardhi na uendelezaji wa miji utafanyika katika mpango mzuri

Pamoja na kupima maeneo na kutoa hati miliki, Mhe.Naibu Waziri amesema Idara ya Ardhi inapaswa kuhakikisha wananchi waliomilikishwa maeneo wanajenga kwa kuzingatia sheria Namba 8 ya mwaka 2007 ya Mipango Miji, ili kuepukana na ujenzi holela unaopelekea kuwa na miji isiyopangwa.

Aidha, Mhe.Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, amesisitiza maeneo yote ya Taasisi za Serikali yapimwe na kutolewa hati miliki ili kuyalinda na uvamizi.

Sanjali na hilo, Mhe.Naibu Waziri amewataka wataalam wa Ardhi kukusanya maduhuli ya Serikali yatokanayo na kodi za ardhi kwa kutumia mifumo ya Kielektroniki iliyowekwa katika kufuatilia na kuhakikisha wananchi wote wanaostahli kulipa kodi ya ardhi wanalipa kwa wakati.

Naibu Waziri ameelekeza Kamati za Halmashauri zinazosimamia Ardhi zihakikishe zinaifanya agenda ya Makusanyo ya maduhuli kuwa ya kudumu katika vikao vyao vya kila robo, ili kila wanapokutana itolewe taarifa ya hali ya makusanyo, wananchi waliopewa notisi na wale wanaotakiwa kupelekwa katika mabaraza ya Ardhi ya Wilaya kwa kushindwa kulipa kodi ya ardhi kwa wakati.

Akiwasilisha taarifa ya Wilaya ya Bariadi Mkuu wa Wilaya hiyo, Mhe.Festo Kiswaga amesema Halmashauri zote mbili zinazounda Wilaya ya Bariadi zinaendelea na kuhamasisha wananchi kupima maeneo yao na kupata hati miliki ili kuongeza ukusanyaji wa maduhuli ya Serikali kupitia kodi ya Ardhi, ambapo Halmashauri ya Wilaya Bariadi pekee kwa mwaka 2017/2018 inatarajia kupima viwanja 2400 katika Vituo vya Kibiashara vya Nkololo,Dutwa na Ngulyati.

Naye Kaimu Kamishna wa Ardhi Msaidizi wa Kanda, Makwasa Biswalo amesema Mtalaam kutoka Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi amefika Mkoani Simiyu kwa ajili ya kutoa mafunzo ya mfumo wa ukusanyaji wa kodi za Ardhi,  kwa watumishi wa Halmashauri zote ambao utawawezesha kutengeneza ankara (bill) ya makusanyo ya kodi na tozo zote.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka ameshukuru Wizara ya Ardhi kwa kuona Umuhimu wa kuanzisha Kanda ya Ardhi ya Simiyu na akaomba Wizara ifanye utaratibu wa kumleta Mwenyekiti wa Baraza la Ardhi la Maswa kutokana na aliyekuwepo kasimamishwa kazi, hali iliyopelekea mashauri mengi kutofanyiwa kazi.

Msajili Msaidizi wa Baraza la Ardhi Kanda ya Ziwa, Dorothy Moses amesema kuanzia mwezi Septemba 2017 atakuwepo Mwenyekiti wa Baraza la Ardhi na Nyumba la Maswa  ambaye atasikiliza kesi, ambapo pia ameleeza kuwa Wizara ina mpango wa kuanzisha mabaraza mawili ya Ardhi na Nyumba katika Wilaya ya Bariadi na Busega ambayo yataanzishwa muda wowote baada ya kupatikana majengo kwa ajili ya Ofisi.

Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe.Angelina Mabula(Mb) yuko katika ziara ya siku mbili Mkoani Simiyu ambapo akiwa Mjini Bariadi amefanya kikao na  Viongozi, wataalam wa Ardhi na Watendaji wa Kata,Mitaa na Vijiji wa Halmashauri ya Mji Bariadi na Halmashauri ya Wilaya Bariadi kilichofanyika Mjini Bariadi.

Baadhi ya watumishi wa Idara ya Ardhi Mkoa na Wilaya na Watendaji wa Kata, Mitaa na Vijiji wa Wilaya ya Bariadi wakimsikiliza Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi , Mhe.Angelina Mabula(Mb) (hayupo pichani) katika kikao kilichofanyika Mjini Bariadi wakati wa ziara yake Mkoani Simiyu.

Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Mhe.Festo Kiswaga akiwaasilisha taarifa ya Wilaya hiyo kwa Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi , Mhe.Angelina Mabula(Mb)(wa tatu kushoto)wakati akiwa katika Ziara ya siku Mbili Mkoani Simiyu.

Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Mhe.Festo Kiswaga akiwaasilisha taarifa ya Wilaya hiyo kwa Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi , Mhe.Angelina Mabula(Mb)(wa tatu kushoto)wakati akiwa katika Ziara ya siku Mbili Mkoani Simiyu.

Mkurugenzi wa Wilaya ya Bariadi(kushoto) akitoa maelezo kwa Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi , Mhe.Angelina Mabula(Mb)(kulia) kuhusu jengo lililoandaliwa kwa ajili ya Ofisi ya Ardhi Kanda ya Simiyu ambayo inatarajia kuanza kazi hivi karibuni, ambayo itahudumia mikoa ya Simiyu, Mara na Shinyanga.

Mkurugenzi wa mji wa Bariadi, Ndg.Melkizedek Humbe akitoa maelekezo kwa Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi , Mhe.Angelina Mabula(Mb) wakati alipotembelea Ofisi ya Idara ya Ardhi ya Halmashauri hiyo kujionea namna inavyokusanya mapato yatokanayo na Ardhi, wakati wa ziara yake Mkoani Simiyu.


Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa