• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

Wakulima Wakiwezeshwa Zana Bora za Kilimo Watalima kwa Tija Zaidi: Kiongozi wa Mbio za Mwenge

Posted on: May 23rd, 2019

Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa mwaka 2019, Ndg. Mzee Mkongea Ali ametoa wito kwa viongozi wilayani Meatu kuwasaidia wakulima wa pamba  kupata zana bora za kilimo ili kuongeza tija  katika uzalishaji  na wilaya hiyo iendelee kuwa kinara katika uzalishaji wa zao la pamba nchini.

Ndg. Ali ameyasema hayo wakati Mwenge wa Uhuru ulipopita na kukagua  Shamba la Mbegu bora ya pamba lenye ukubwa wa ekari 13 katika Kijiji cha Mwabusalu ambapo alimpongeza mkulima Jidayi Charles na kumtunuku cheti cha kumtambua kama mkulima bora.

“Ninampongeza sana Bwana Jidayi maana ni wazee wachache sana wanaojihusisha na kilimo ni vizuri mkachukua jitihada za makusudi kumsaidia apate zana za kisasa, kama analima ekari 13 akiwa hana trekta nina uhakika akiwezeshwa atafanya vizuri zaidi, kama mmeshaanza utaratibu wa kumpatia mkopo uharakishwe ili kiwango cha uzalishaji kiweze kuongeza zaidi” alisema Mzee  Mkongea Ali.

Mkuu wa Wilaya ya Meatu, Dkt. Joseph Chilongani amesema wilaya ya Meatu ndiyo wilaya kinara katika uzalishaji wa pamba nchini ambapo amebainisha kuwa katika msimu wa mwaka 2018/2019 ilizalisha takribani kilo milioni 31 za pamba na akaeleza kuwa mkakati wa wilaya ni kuendelea kuwasaidia wakulima kwa utaalam na mikopo za kununua zana bora ili waweze kuzalisha kwa tija  zaidi.

Akitoa taarifa ya mradi wa shamba hilo, Afisa Kilimo wa Wilaya ya Meatu, Bw.Thomas Shilabu amesema uzalishaji wa zao la pamba unakabiliwa na changamoto ya baadhi ya wakulima kulima wa kilimo cha mazoea kwa kusia mbegu na kupalilia maotea.

Kwa upande wake Bw. Jidayi Charles amesema kwa sasa anatumia trekta ya kukodi kulima shamba lake lenye ukubwa wa ekari 13 ambalo linachangia kuchelewesha uandaaji wa shamba kwa kuwa linatumiwa na wakulima wengi, lakini endapo atakapata trekta lake litamrahisishia kuandaa shamba mapema na kwa urahisi zaidi.

Pamoja na kutembelea mradi wa shamba za kuzalisha mbegu bora za pamba, Mwenge wa Uhuru ukiwa Wilayani Meatu umezindua vyumba viwili vya maabara shule ya Sekondari Mwandoya, kutembelea mradi wa maji wa SangaItiinje na kupanda miti katika Chanzo cha maji, kukagua klabu ya wanafunzi ya wapinga RUSHWA na Klabu ya wanafunzi ya kupambana na mimba za utotoni shule ya msingi Isengwa.

Wakati mwenge wa uhuru ulipopita kuona shughuli za klabu ya mapambano dhidi ya mimba za utotoni, Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru ameupongeza uongozi wa wilaya ya Meatu kuanzisha klabu hizo shuleni na akatoa wito kwa wataalam wa Ustawi wa Jamii na Dawati la jinsia na vyombo vya dola kutowahurumia wote wanaobanika kusababisha mimba za utotoni.

Aidha, ulifungua Nyumba ya kulala wageni TS Lodge, kukagua shughuli za kikundi cha vijana wajasiriamali, kukagua shughuli za mapambano dhidi ya rushwa, mapambano dhidi ya mimba za utotoni na mapambano dhidi ya malaria.

MWISHO

KUPATA PICHA ZAIDI KUHUSU MBIO ZA MWENGE WA UHURU MEATU FUNGUA KIUNGANISHI HIKI:-https://simiyuregion.blogspot.com/2019/05/wakulima-wakiwezeshwa-zana-bora-za.html

Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa