• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

Wafanyabiashara Mkoani Simiyu Waunga Mkono Serikali Ujenzi wa Shule ya Sekondari ya Mkoa

Posted on: April 18th, 2018

Wafanyabiashara wa Mkoa wa Simiyu wamekubali kuunga mkono Serikali katika Ujenzi wa Shule ya Sekondari ya Mkoa wa Simiyu inayotarajiwa kuanza kujengwa mwezi Juni mwaka huu.

Kauli hiyo ilitolewa na Wafanyabiashara hao katika kikao chao na Mkuu wa Mkoa kilichofanyika jana Mjini Bariadi, ambacho kilifanyika kwa lengo la kuzungumzia fursa za biashara na uwekezaji zilizopo mkoani humo, changamoto zinazowakabili na utatuzi wake.

Awali akifungua kikao hicho, Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka amesema Serikali mkoani humo imekusudia kuwa na shule kubwa itakayoweza kuchukua wanafunzi 1000 ambayo itakayopatikana kwa kujenga upya shule ya Sekondari Simiyu (Kidato cha kwanza hadi cha Nne), ambapo aliahidi kuwa ofisi yake itatoa fedha kiasi na akawaomba wafanyabiasha wazawa kuchangia Ujenzi wa shule hiyo kwa ajili ya maendeleo ya Mkoa.

Amesema  pamoja na kujenga upya Shule ya Sekondari Simiyu, katika shule hiyo kutajengwa mabweni kwa ajili ya wanafunzi wa kike ili wanafunzi wote wa kike wasome wakiwa wanafunzi wa bweni(boarding).

Ameongeza kuwa shule hiyo itakuwa ikichukua wanafunzi watakaofanya vizuri kutoka katika wilaya nyingine ili waandaliwe vema na kuimarisha shule za Kidato cha Tano na Sita na kuwa katika uwezo wa kushindana na wenzao kutoka mikoa mingine.

Aidha, amesema mara baada ya kukamilisha kuimarisha Shule ya Sekondari ya Simiyu Mkoa huo umedhamiria kuwa na Shule ya Sekondari ya Wasichana Simiyu na Shule ya Sekondari ya Wavulana Simiyu,  ambazo zitapatikana kwa Kujenga Upya au kubadili zilizopo kwa kibali maalumu cha Wizara yenye dhamana na Elimu, ili kuwa na shule mbili za mkoa moja ya wasichana na nyingine ya wavulana.

"Hatuwezi kuwa Makao Makuu ya Mkoa ambayo elimu yote inaishia Shule za Kata, ni lazima tutengeneze shule ambayo watoto wetu wakifanya vizuri katika wilaya zetu wanakuja kusoma hapa; hatuwaweza kushindana na kufanya mambo yote mazuri tuliyojadili hapa ya viwanda na mengine kama hatutaelimisha watu wetu" alisema.

Mwenyekiti wa Chama cha Wafanyabiashara Mkoa wa Simiyu Bw. Njalu Silanga amesema Wafanyabiashara wako tayari kuunga mkono juhudi za Serikali katika ujenzi wa Shule ya Mkoa jambo ambalo litakuwa mwendelezo wa kile kilichowahi kufanyika miaka iliyopita ambapo wafanyabiashara hao walijenga shule ya Sekondari Biashara na kuikabidhi kwa Serikali.

“Sisi wana Simiyu tunapenda maendeleo, tumewahi kukusanywa kama hivi leo tukakubaliana tukajenga Shule ya Sekondari Biashara tukaikabidhi Serikali, pia wapo watu hapa kwenye maeneo yao wamejenga madarasa tena ya viwango wakaikabidhi Serikali, kujenga Shule ya Sekondari ya Mkoa inawezekana” alisema  Njalu.

Wakati huo huo wafanyabiashara hao wameahidi kuwashirikisha Wafanyabiashara wengine ambao ni wazaliwa wa Mkoa wa Simiyu wanaofanya biashara zao katika mikoa mingine ili washirikiane katika kufanikisha Ujenzi wa Shule ya Sekondari Mkoa wa Simiyu.

KUPATA PICHA ZAIDI KUHUSU HABARI HII FUNGUA HAPA:-https://simiyuregion.blogspot.com/2018/04/wafanyabiashara-mkoani-simiyu-waunga.html

Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa