• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

Wadau wa Kilimo Simiyu Wajadili Mwongozo wa Kilimo cha Mkonge

Posted on: September 12th, 2020

Bodi ya Mkonge Tanzania imekutana na uongozi wa mkoa wa Simiyu na baadhi ya watendaji na wataalam wa kilimo kwa lengo la kujadili mwongozo wa kilimo cha mkonge mkoani hapa lengo likiwa ni kuhakikisha mkulima anazalisha mkonge bora na wenye thamani katika soko.


Akikabidhi mwongozo huo kwa katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu, Bi. Miriam Mmbaga na baadaye akawakabidhi maafisa Kilimo, Mratibu mkuu wa utafiti na masoko, Bw Hassan Kibarua amesema ni vema wataalam wa kilimo wakatoa elimu kwa wakulima wa mkonge juu ya kuzingatia ubora kuanzia uzalishaji ili usipungue thamani.

"Mkonge unatakiwa kuchakatwa si zaidi ya masaa 48 tangu kukatwa lakini kuna wakati mkulima anachakata mkonge uliokatwa zaidi ya siku tano, unakuwa umepungua ubora na unapofika sokoni unakuwa haupo kwenye daraja la ubora wa 3L ambalo lina bei ya juu, " alisema Kibarua.

KIbarua ameongeza kuwa pia wakulima inabidi waelekezwe namna ya kuchakata na kusafisha mkonge ili wasipeleke sokoni mkonge wenye uchafu (maganda) kwani makosa kidogo yanapelekea kushuka kwa thamani ya zao hilo.

Ameongeza kuwa  mkonge unasoko la uhakika ndani na nje ya nchi kutokana na kuongezeka kwa matumizi kutoka kwenye yale ya awali ya kutengeneza kamba na magunia; sehemu ya matumizi mengine ni kutengeneza mapambo ya nyumba, mabaki yake kutengeneza gesi na chakula cha mifugo


Akizungumzia  umuhimu wa kupima afya ya udongo ili kuongeza uzalishaji wa mkonge, mratibu wa utafiti wa udongoTanzania kutoka TARI- Mlingano Dkt. Sibaway Mwango, amesema ni vema maafisa ugani wakatimiza wajibu wao na wawaunganishe watafiti na wakulima ili wakulima waweze kulima kwa tija.


"Kila mmea una aina fulani ya udongo ambao unahitaji na kiasi fulani cha tindikali kisichozidi , hivyo ni muhimu wakulima kupima afya ya udongo kabla ya kupanda mazao  ili kujua aina ya virubishi vilivyopo na aina ya mbolea inayotumika Afya ya udongo ni muhimu zaidi kwa kilimo chenye tija," alisema Dr Mwango.

Aidha amesema, afya ya udongo ni lazima ilindwe kwa kupanda mazao ya mikunde katika mashamba ya mkonge, kuepuka matumizi ya mbolea yasiyo sahihi yanayo sababisha kuharibu udongo, ambapo alibainisha kuwa hali hiyo inachangia wakulima kutopata mavuno mengi na yenye ubora uliokusudiwa .

Katika mkoa wa Simiyu zao la mkonge tayari limeanza kulimwa katika baadhi ya maeneo hasa katika wilaya ya Meatu na Maswa ambapo wakulima wanaojishughulisha na kilimo hicho wametoa wito kwa wakulima wenzao kuchangamkia fursa hiyo kwa kuwa zao hilo linalimwa wakati wowote na  linastahimili katika hali zote.

"Kilimo cha mkonge hakimtupi mtu maana mkonge haubagui ukame wala mvua nyingi kwa hali yoyote ni lazima uvune na kizuri zaidi ninachanganya na mazao mengine yaliyoko kweye msimu na sijaona shida yoyote,” alisema Bw. Mabula Mipawa

"Ukiangalia uchumi wangu wa sasa na hapo awali kuna mabadiliko sana sasa ninalima kilimo ambacho kinaniingizia pesa muda wowote hadi nimefikia hatua ya kuweza kupeleka watoto wangu shule na kuwa na uchumi mzuri,"alisema Mizwazwa Kidia mkulima wa mkonge kata ya Mwasengela.
MWISHO

KUPATA PICHA ZAIDI TAFADHALI FUNGUA KIUNGANISHI HIKI:-https://simiyuregion.blogspot.com/2020/09/wadau-wa-kilimo-simiyu-wajadili.html

Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa