• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

Wadau wa Elimu Wakiri Kambi za Kitaaluma Kuchangia Simiyu Kuingia Kumi Bora Matokeo Kidato cha Sita 2018

Posted on: July 24th, 2018

Wadau wa Elimu mkoani Simiyu wamekiri kuwa kambi za kitaaluma zimekuwa na mchango mkubwa katika kuuwezesha mkoani huo kushika nafasi ya kumi Kitaifa katika matokeo ya Mtihani wa Taifa wa Kidato cha Sita mwaka 2018, kutoka nafasi ya 26 mwaka 2017.

Hayo yamebainishwa katika kikao cha tathmini ya Matokeo ya Mtihani wa Taifa wa Kidato cha Sita mwaka 2018 kilichofanyika Julai 24, Mjini Bariadi ambapo pia walimu wa Kidato cha Sita waliowezesha wanafunzi kufaulu kwa alama A na B katika masomo yao wamepongezwa na kupewa zawadi ya fedha taslimu na vyeti.

Kikao hiki  kimewashirikisha  viongozi na Watendaji wa Serikali ngazi ya Mkoa na Wilaya, Wakuu wa Shule na walimu wa shule za Sekondari za kidato cha tano na sita, wadhibiti ubora, Maafisa Elimu Wilaya na Kata, Wenyeviti wa Bodi za Shule, Viongozi wa Dini, Viongozi wa Chama cha Walimu na wadau wengine.

Baadhi ya wadau waliochangia katika tathimini hiyo wamempongeza Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka kwa kuanzisha wazo la kuwa kambi za kitaaluma ambazo zimeleta mafanikio makubwa na kutoa maoni ya namna ya kuboresha na kuzifanya kambi hizi kuwa mkakati endelevu katika kuinua ubora wa elimu mkoani Simiyu.

“Nampongeza sana mkuu wetu wa Mkoa kuja na wazo hili la kuwa na kambi za Kitaaluma na Mkuu wa Mkoa amesema ni agenda ya kudumu katika mkoa , kama walimu, wazazi, wanafunzi, sisi viongozi na wadau wengine wa elimu katika Mkoa wetu tukiendelea kushirikiana, kambi hizi zitabadilisha mfumo wa elimu na kuufanya mkoa ung’are katika sekta ya elimu” Mkuu wa Wilaya ya Maswa, Dkt. Seif Shekalaghe.

“Kambi za Kitaaluma zimechangia kuufikisha mkoa kwenye nafasi ya 10 Kitaifa lakini nashauri iundwe kamati ya ndogo ya Maafisa Taaluma kutathmini mazuri na changamoto za kambi za kitaaluma ili tuweze kuboresha zaidi na kuufanya mkoa kufanya vizuri zaidi” Mwl.Baraka Owawa Katibu Chama cha Walimu Wilaya ya Bariadi.

Nao viongozi wa madhehebu ya dini walioshiriki katika kikao  hicho cha tathmini wamesema wanaunga mkono juhudi za Serikali katika maendeleo ya elimu na wakaahidi kushirikiana na Serikali kwa kuwa hata vitabu vya dini navyo vinahimiza kupenda na kuthamini Elimu.

Afisa Taaluma wa Mkoa wa Simiyu, Mwl. Onesmo Simime akitoa tathmini ya matokeo ya Mtihani wa Taifa wa Kidato cha Sita mwaka 2018 amesema idadi ya wanafunzi waliopata daraja la I imeongezeka kutoka wanafunzi 43 mwaka 2017 na kufikia 119, daraja la II imeongezeka kutoka 304 mwaka 2017 hadi 451, daraja III toka 325  mwaka 2017 hadi 381.

Aidha, amesema idadi ya wanafunzi waliopata daraja sifuri imepungua kutoka kutoka wanafunzi 29 mwaka 2017 hadi wanafunzi 14 mwaka 2018 ambapo amebainisha kuwa shule sita kati ya 11 mkoani humo zimefanikiwa kuondoa daraja sifuri mwaka 2018.

 Amesema pamoja na kambi za Kitaaluma mkoa uliweka mikakati ambayo pia imechangia kuongeza ufaulu kuutoa kwenye nafasi ya 26 mwaka 2017  hadi 10 Kitaifa mwaka 2018, ambayo ni kuhakikisha walimu wanafundisha vipindi vyote na kufidia vilivyopotea na kufanya mtihani wa utimilifu (Mock) wa Mkoa na kanda uliowasaidia walimu kubaini mada zenye changamoto na kufanya mapitiao ya mada hizo.

Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe. Anthony Mtaka amewapongeza walimu,wazazi wanafunzi  na wadau wote wa elimu waliofanikisha mkoa kufanya vizuri katika Mtihani wa Taifa wa Kidato cha Sita mwaka 2018, huku akisisitiza kuendelea kuweka mikakati ya kuboresha uendeshaji wa kambi za kitaaluma ili waweze kufikia lengo walilojiwekea la kufikia ‘single digit’ nafasi ya 1-9.

Katika kikao hicho pia Mtaka ameagiza kuwa muda wa  wanafunzi wa madarasa ya mtihani katika Shule za Sekondari za Serikali(Kidato cha nne na cha sita)kuzimiwa taa utakuwa saa sita usiku siyo saa nne usiku, hivyo akiwataka walimu kuweka utaratibu wa viongozi wa wanafunzi kuendelea na ratiba kwa niaba yao baada ya ratiba ya walimu inayoishia saa nne usiku.

Wanafunzi wa kidato cha sita mwaka 2018 walikaa katika kambi za Kitaaluma kwa muda wa siku 10 mwezi Aprili, aidha wanafunzi wa Kidato cha nne na Darsa la saba wa mwaka 2018 waliwekwa katika kambi za kitaaluma mwezi Juni kwa siku 21 kwa ajili ya kujiandaa na mitihani yao ya Taifa.

MWISHO

KUPATA PICHA ZAIDI ZA TUKIO HILI FUNGUA KIUNGANISHI HIKI:-https://simiyuregion.blogspot.com/2018/07/wadau-wa-elimu-wakiri-kambi-za.html

Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa