• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

Wachimbaji Uhai Wenu ni Muhimu Kuliko Madini, Fuateni Taratibu- RC Kafulila

Posted on: February 17th, 2022

Mhe.Kafulila ameyasema hayo leo, wakati alipotembela mgodi wa EMJ, Dutwa wilayani Bariadi. Mhe kafulila amefanya ziara hiyo ili kukutana na kutatua kero za wachimbaji. Wakizungumzia kero zao, Wachimbaji hao wametaja kero hizo kuwa ni pamoja na kukatazwa kuchimba kwenye baadhi ya maeneo, uwepo wa  mwekezaji mchina ambaye ameanza kujenga uzio na hivyo kuhofia uhuru wao wa kuchimba madini kwenye eneo hilo na Maduara yaliyotelekezwa kurudishwa kwa mwenye leseni, huku  wao wakitafuta nguvu zaidi za kuendelea na uchimbaji.

Akijibu hoja hizo Mhe. Kafulila alimtaka Mwakilishi  toka ofisi ya Madini bwana Lucas Mwakulo, kujibu kero hizo na kueleza sheria inasemaje kuhusu maduara yaliyotelekezwa. Bw.Mwaluko  alieleza kuwa ni kweli kwamba kuna eneo ambalo ofisi ya Madini imekataza uchimbaji wa madini na hiyo ni  kwa sababu za kiusalama. Suala la kiusalama lipo juu ya kila kitu. Hairuhusiwi mchimbaji yeyote kuchimba katika eneo ambalo ni hatarishi.Aidha Serikali imetoa maelekezo kuwa mchimbaji anaweza kupewa kibali cha siku 30 ili apumzike na kukusanya nguvu, siku hizo zikipita shimo linarudishwa kwa mwenye leseni.

Nae katibu wa wachimbaji Bw. Ramadhani Faida, alieleza kuwa ni kweli kwamba kuna duara 5 zilizosimamishwa uchimbaji na duara hizo ni 286A, 203A,190,101B  na duara namba 237B. Akizungumzia sababu ya kufungwa mashimo hayo mkaguzi Mkuu (chief Inspector) Bw. Charles Lyaganga  alizitaja sababu hizo kuwa ni Changamoto ya maji na ajali za gesi.“Sisi ndio tunatoa mapendekezo ofisi ya Madini kuwa shimo gani lifungwe baada ya ukaguzi. Tarehe 16/01/2022 tulitangaza maduara 11 kuwa hatarishi”. Amesema Lyaganga.

 Mhe. Kafulila ameitaka ofisi ya madini kwa kushirikiana na Mkaguzi ,kubainisha Maduara yaliyotekelezwa kama yapo, na endapo yapo basi mabango yakawekwe kwenye maduara hayo mara moja na baada ya siku 30 yarejeshwe kwa mwenye leseni.  “Yale maeneo ambayo ni hatarishi,kimsingi kwenye hayo maeneo uchimbaji usiendelee, usimamishwe,kwani uhai wenu ni muhimu kuliko madini.Hayo maeneo msiende kama mnaenda basi muende kwa kibali cha afisa madini.Mpate ridhaa ya afisa madini”. Ameagiza Mhe. Kafulila.

 Aidha Mhe. Kafulila ametoa ruhusa kwa wachimbaji kuendelea na uchimbaji madini kwenye maeneo yaliyo salama ili mradi wazingatie, kanuni, sheria na taratibu.Mkuu wa Mkoa amemwelekeza inspekta Lyaganga kufanya kazi kwa umakini na kwa ukaribu na ofisi ya madini. “Wachimbaji fuateni taratibu, sio mnaacha maduara yenu bila kufuata taratibu halafu baadae mnavizia fidia. Kwa maeneo ambayo yapo nje ya maeneo hatarishi endeleeni na uchimbaji ”.Amesema Kafulila.

Akizungumzia suala la uwepo wa Wachina, Mhe. Kafulila alieleza kuwa uwepo wa Wachina  hao ni makubaliano kati ya mwenye leseni na  Wachina, ili waweze kufanya utafiti na kuona ni kwa jinsi gani  na kwa kutumia teknologia ya juu wanaweza kupata madini zaidi, kwani wachina hao ni wazoefu na wamefanya kazi katika migodi mingine kama vile Geita.

Aidha ujenzi wa uzio kwenye eneo hilo ni kwa sababu za kiusalama, kama ilivyoelezwa na mwakilishi kutoka ofisi ya madini ambaye alieleza kuwa maelekezo yalishatolewa kuwa kwenye kila mgodi  ni lazima kuwe na uzio ili kuepuka uvamizi na wizi mgodini (Manyani). Mhe.Kafulila alisisitiza kuwa, pamoja na uwepo wa uzio huo wachimbaji, wataruhusiwa kuendelea na uchimbaji madini.Mwisho.

Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa