• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

Vongozi Waaswa kuzungumza Lugha moja kuhusu Haki za Wananchi, Kukomesha Dhuluma

Posted on: June 9th, 2018

Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana UVCCM Taifa Kheri James  amewaasa  viongozi wa dini ,chama na Serikali kutotofautiana lugha kuhusu haki za wananchi katika kukomesha dhuluma na pia wawakemee wanaokwamisha juhudi za Serikali katika kuwaletea maendeleo wananchi.

James amesema hayo katika futari iliyoandaliwa na Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Anthony Mtaka katika viwanja vya ofisi ya mkoa, na kuhudhuriwa na waumini wa Dini ya Kiislamu wakiongozwa na Shekh Mahamudu Kalokola ,viongozi wa madhehebu mbalimbali na viongozi wa chama na serikali ,ikiwa ni desturi yake kila mwaka kujumuika pamoja katika kipindi cha mfungo mtukufu wa Ramadhan.

“Maendeleo yanayofanywa sasa ni kwa ajili ya watu wote sisi kama viongozi tunao wajibu wa kushiriki ili tuweze kuhakikisha kuwa yanafikiwa kwa wakati, viongozi wa dini, chama na Serikali tusitofautiane lugha katika kutetea haki za wananchi, tuhakikishe tunasimamia wananchi wetu wanapata haki na dhuluma inakomeshwa” alisema James.

James amesema viongozi wa madhehebu ya dini wana mchango mkubwa kwa  Serikali katika kuhimiza maendeleo kupitia makanisa na misikiti ,hivyo ni vema kuendelea kuliombea taifa kudumisha amani pasipo kutofautiana na chama na Serikali.

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe.Anthony Mtaka amewashukuru viongozi wa dini kwa namna wanavyoshirikiana na Serikali katika masuala mbalimbali , huku akiwaomba kuendelea kusaidia katika malezi ya watoto hasa katika mkakati wa mkoa wa kuinua kiwango cha ufaulu madarasa la mitihani,  ambapo Kidato cha nne na darasa la saba wapo katika kambi za Kitaaluma.

“Watoto wetu wa kidato cha nne na darasa la saba wako katika kambi za kitaaluma kwa ajili ya kujiandaa na mitihani ya Taifa, sisi kama Serikali tumetoa nafasi ya kama nusu saa kwa watoto kushiriki ibada kila siku katika kambi hizo, tunaomba viongozi wetu wa dini mfike kwa ajili ya kuwausia na kuwasisitiza kusoma kwa kuwa tunahitaji watoto wetu wafanye vizuri “ alisema.

Shekhe  wa Mkoa wa Simiyu Mahamudu Kalokola ameishukuru Viongozi wa Serikali Mkoani humo wakiongozwa na Mkuu wa Mkoa, Mhe. Anthony Mtaka kwa namna wanavyoshirikiana na Madhehebu yote ya dini naye akaahidi kuendelea kushirikiana na  Serikali katika Nyanja mbalimbali za maendeleo.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Kongwa Mhe. Deo Ndejembi ambaye yupo SIMIYU na viongozi wa vikundi vya vijana Kongwa kwa lengo la kujifunza Simiyu ilivyofanikiwa kwa miradi ya vijana, akiwa katika futari hiyo amesema Simiyu  imejipambanua vema katika masuala ya vijana hususani katika uzalishaji mdogo mdogo jambo ambalo liwawafanya waje kujifunza ili waweze kuwasaidia vijana wa Kongwa kuanzisha miradi endelevu na yenye tija.

MWISHO

KUPATA PICHA ZAIDI KATIKA TUKIO HILI FUNGUA KIUNGANISHI HIKI:-https://simiyuregion.blogspot.com/2018/06/viongozi-mkoani-simiyu-waaswa.html

Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa