• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

Usimamizi wa TMDA, Elimu Kwa Umma Zatajwa Kusaidia Kupunguza Bidhaa Bandia Sokoni

Posted on: May 7th, 2021

Usimamizi shirikishi, elimu kwa umma zimetajwa kuwa ni miongozi mwa sababu zilizochangia kupunguza uwepo wa dawa bandia katika mikoa ya kanda ya ziwa, jambo ambalo limechangia soko la bidhaa hizo (dawa) kuwa soko salama.

Hayo yamebainishwa na Kaimu Meneja wa Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba, Bi. Sophia Mziray Mei 06, 2021 wakati akizungumza katika ufunguzi wa kikao kazi cha wataalam wa afya na mifugo pamoja na wakaguzi wa dawa , kilichofanyika Mjini Bariadi Mkoani Simiyu.

“Tumeza kulisimamia vizuri soko hili la kanda ya ziwa siyo kama miaka ile ya nyuma kwa sasa hivi soko hili naweza kusema ni soko salama kwa bidhaa hizi, hata zikikutwa sokoni ni chache sana, pamoja na hilo tunawaeleimisha wananchi, suala la udhibiti siyo la taasisi tu, hata wananchi ni wadau wakubwa katika udhibiti na huwa tunapata taarifa kutoka kwa rai wema juu ya wafanyabiashara wasio waaminifu wanaofanya biashara haramu za dawa, tumewabaini na tumewachukulia hatua,” alisema Mziray.

Akifungua kikao kazi hicho Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa, Bw. Ekwabi Mujungu amesema kufanya kazi bila taarifa (kumbukumbu) ni tatizo ambalo linahitaji ufumbuzi wa haraka huku akiwataka kupitia kikao kazi hicho kuja na suluhisho la kudumu.

“Mnaohusika si lazima mpaka watu  watoke Dar es salaam kuja kuona dawa bandia fanyeni kazi kwa viapo vyenu,” alisema Mujungu

Kwa upande wao baadhi ya washiriki wa kikao kazi hicho wameishukuru TMDA kutoa mafunzo ambayo yatawaongezea maarifa na kuwawezesha kutekeleza majukumu yao hususani ya ukaguzi kwa ufanisi.

“Elimu niliyoipata leo itanisaidia sana katika kufanya kaguzi mbalimbali pia imenisaidia kujua kuwa ni jukumu letu wataalam kuwapa elimu wamiliki wa maduka ili wauze bidhaa zilizosajiliwa na wajenge utamaduni wa kukagua bidhaa zao (dawa) na kubaini dawa zilizoisha muda wake ili watumiaji wa mwisho au walaji wasiumizwe kwa kuuziwa dawa zisizofaa” alisema Linah Kirumbi Daktari wa Mifugo Halmashauri ya Mji wa Bariadi.

MWISHO

KUPATA PICHA ZAIDI FUNGUA KIUNGANISHI HIKI:-https://simiyuregion.blogspot.com/2021/05/usimamizi-wa-tmda-elimu-kwa-umma.html

Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa