• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

Tuzo ya Serengeti Hifadhi Bora Afrika Yatambulishwa kwa Wananchi Simiyu na Mara

Posted on: June 19th, 2019

Tuzo ya Serengeti Hifadhi Bora zaidi Afrika imetambulishwa rasmi kwa wananchi wa mikoa ya Simiyu na Mara kutoka katika maeneo yanayoizunguka Hifadhi ya Taifa ya Serengeti.

Akiitambulisha tuzo hiyo Waziri wa Maliasili na Utalii, Dkt. Hamisi Kigwangalla Juni 18, 2019 katika Kijiji cha Robanda wilaya ya Serengeti Mkoani Mara, amesema tuzo hii iwe chachu kwa wahifadhi, viongozi na wananchi wote kwa ujumla kuendelea kuimarisha shughuli za uhifadhi hapa nchini.

“Tuzo tuliyoipata ya Serengeti Hifadhi Bora zaidi Afrika iwe chachu ya kutufanya tuendelee kuitangaza zaidi Hifadhi ya Taifa ya Serengeti ili tuweze kushinda tuzo ya Kimataifa; Tuzo hii iwe chachu kwetu wahifadhi, viongozi na wananchi wote kwa ujumla kuendelea kuimarisha shughuli za uhifadhi hapa nchini” alisema Kigwangalla.

Ameongeza kuwa Sekta ya uhifadhi ina faida kubwa zaidi ya utalii ambazo ni pamoja na kutoa hewa ya oksjeni kutoka kwenye misitu, kukamilisha mzunguko wa mvua, kutoa mahali pa wanyamapori kuishi na kusaidia zoezi la uchavushaji kwa mimea unaopelekea kuwepo chakula, hivyo shughuli za uhifadhi ziimarishwe zaidi kwa manufaa ya vizazi vya sasa na vijavyo.

Naye Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka ameipongeza Mamlaka ya Hifadhi za Taifa Tanzania TANAPA kwa kazi kubwa ya uhifadhi wanayoifanya jambo ambalo limeifanya Mamlaka hiyo kutoa msaada kwa jamii, ambapo alibainisha kuwa TANAPA imechangia jumla ya shilingi milioni 100 katika ujenzi wa shule ya sekondari Simiyu maalum kwa ajili ya michezo.

Aidha, Mtaka amesema Mkoa wa Simiyu ni wadau wakubwa wa uhifadhi na unaunga mkono juhuda zote za uhifadhi zinazofanywa na wizara na wadau mbalimbali wa uhifadhi.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Mara, Mhe. Adam Malima amepongeza Kamati za Ulinzi na Usalama ya Mikoa ya Simiyu na Mara kwa kazi kubwa wanayofanya ya kuhakikisha kuwa zinapambana na uharibifu wowote katika Hifadhi ya Taifa ya Serengeti hali iliyochangia hifadhi hii kuonekana bora zaidi katika Bara la Afrika.

Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Mhe. Festo Kiswaga ambaye pia ni mhifadhi amesema tuzo hiyo I matunda ya juhudi za Serikali na wananchi katika kukomesha ujangili na uwindaji haramu na kupitia tuzo hii itachochea watalii wengi kuingia nchini.

Naye Shawezi Silas mkazi wa Kata ya Ikoma wilaya ya Serengeti amesema tuzo hiyo wananchi wameipokea kwa furaha kubwa sana  na imewasaidia kuilewa maana ya uhifadhi na umuhimu wa kuzilinda rasilimali za Taifa ikiwemo wanyamapori.

MWISHO

KUPATA PICHA ZAIDI FUNGUA KIUNGANISHI HIKI:-https://simiyuregion.blogspot.com/2019/06/tuzo-ya-serengeti-hifadhi-bora-afrika.html

Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa