• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

Tigo Simiyu Yatoa Msaada wa Karatasi Maandalizi Mtihani wa Taifa Kidato Cha Nne

Posted on: November 7th, 2020

Kampuni ya Simu za Mkononi ya TIGO Mkoa wa Simiyu imetoa msaada wa karatasi kwa ajili ya maandalizi ya mtihani wa Taifa wa Kidato cha nne mkoani hapa, unaotarajia kufanyika kuanzia tarehe 23 Novemba, 2020.

Akikabidhi msaada huo jana kwa niaba ya Meneja wa TIGO Mkoa wa Simiyu, msimamizi wa Duka la TIGO Bariadi Mjini Bi. Anna Kazimoto amesema msaada huo ni mwendelezo wa ushirikiano uliopo kati ya kampuni hiyo na Mkoa wa Simiyu huku akitoa rai kwa wanafunzi kusoma kwa bidii ili waweze kufikia malengo yao.

“Tumetoa msaada huu ili ninyi ndugu zetu msome msiwe na uhaba wa karatasi kwa ajili ya kuchapisha mitihani na majaribio kwa ajili ya kujiandaa na mtihani wa Taifa wa Kidato cha nne, tumetoa rimu 45 zenye thamani ya shilingi 450,000/=” alisema Bi. Anna Kazimoto.

Akizungumza kwa niaba ya Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu, Afisa Elimu Taaluma Mkoa wa Simiyu, Mwl. Onesmo Simime ameishukuru kampuni ya simu ya Tigo na kuahidi kutumia msaada huo kwa matumizi yaliyokusudiwa.

Nao wanafunzi wa Shule ya Sekondari Simiyu wameishukuru Tigo kwa msaada huo na kuahidi kuwa msaada huo utawasaidia kufikia malengo yao ikiwa ni pamoja na kujiandaa vema na mtihani waTaifa kwa kuwawezesha kupata karatasi kwa ajili ya kujibia majaribiao ya mara kwa mara kuelekea Mtihani wa Taifa wa kidato cha nne.

“Mitihani inahitaji maandalizi msaada huu utawasaidia sana kidato cha nne kuondokana na uhaba wa karatasi kwa ajili ya kufanya mitihani na majaribio, tunawashukuru sana Tigo na tunaamini dada zetu na kaka zetu watafanya vizuri na hiyo itakuwa ni sehemu ya shukrani kwa Tigo,” alisema Kuyala Lameck kutoka Shule ya sekondari Simiyu.

Kwa upande wake Mwalimu Kulwa Mtanzania ameishukuru Kampuni ya Simu za Mkononi ya Tigo kwa msaada huo na kutoa wito kwa kampuni hiyo kuendelea kuwa mdau muhimu wa elimu wa mkoa wa Simiyu.

MWISHO

KUPATA PICHA ZAIDI FUNGUA KIUNGANISHI HIKI:-https://simiyuregion.blogspot.com/2020/11/blog-post_7.html

Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa