• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

TACAIDS Yakabidhi Masanduku 10 ya Kuchangia Fedha za Kuboresha Huduma za VVU / UKIMWI SIMIYU

Posted on: July 22nd, 2020

Tume ya Taifa ya Kudhibiti UKIMWI imekabidhi masanduku 10 kutoka Mfuko wa Udhamini wa Kudhibiti Ukimwi kwa Mkoa wa Simiyu ili yatumike kwa ajili ya kuhamasisha uchangiaji wa fedha kwa ajili ya kuboresha huduma za VVU na UKIMWI.

Akikabidhi masanduku hayo Mkurugenzi wa TACAIDS Dkt. Leonard Maboko amesema karibuni Wafadhili wamepunguza kwa kiasi kikubwa ufadhili katika masuala ya Ukimwi ni  vema zikatumika  fedha zetu wenyewe (wadau wa ndani)  badala ya kutegemea Wafadhili

“ Ili Kuchangia fedha hizo Mfuko umebuni Masanduku ambayo Wananchi wanaweza kutoa michango kwa Fedha taslim, tumeleta masanduku haya 10 ikiwa ni maagizo ya Waziri wa nchi ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Vijana,Ajira na Wenye Ulemavu Mhe.Jenista Mhagama ambaye alikuwa mgeni rasmi akimwakilisha Mhe. Kassim Majaliwa Waziri Mkuu,wakati wa maadhimisho ya siku ya ukimwi duniani yaliyofanyika kitaifa mkoani Mwanza 2019”

“ Katika maadhimisho hayo kila mkoa uliagizwa kuwa na masanduku hayo na kuhamasisha wananchi kuchangia jitihada hizi, Siku ya Ukimwi Duniani 2020 kila mkoa utatakiwa kutoa taarifa kuwa umechangia Serikali kiasi gani kupitia Mfuko wa Udhamini wa kudhibiti Ukimwi, alisema Dkt. Maboko.

Aidha, Dkt. Maboko amesema michango hiyo inaweza kuwakilishwa kwa kuchangia Moja kwa moja au kupitia AIrtel Money +255 684 909090 au kwa Viongozi kuchukua masanduku na kuhamasisha wananchi kuchangia katika ziara na matukio mbalimbali ambayo wao wanayaongoza huku akibainisha kuwa mpaka sasa fuko umeshaipatia Serikali kiasi cha shilingi 660.

Katika hatua nyingine Dkt. Maboko amefafanua kuwa katika fedha zote zinazokusanywa katika mfuko huu, asilimia 60 hutumika kwenye ununuzi wa dawa/vitendanishi,  asilimia 25 hutumika kwenye kinga na asilimia 15 kwenye shughuli za bodi na Utawala.

Akipokea msaada huo kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa Wa Simiyu, Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu,  Mhandisi.Mashaka Luhamba ameshukuru TACAIDS kwa kutimiza ahadi ya kuleta masanduku hayo kama walivyoahidi kwa Mhe. Mkuu wa Mkoa huku akiwahakikishia TACAIDS kuwa mkoa utatumia kila fursa kuhakikisha kuwa unawahamasisha Wananchi wa Simiyu kuchangia katika Mfuko huu.

Akieleza hali ya maambukizi ya VVU/UKIMWI katika Mkoa wa Simiyu, Mratibu wa Kudhibiti UKIMWI Simiyu, Dkt.Khamis Kulemba amesema kutokana na utafiti wa Mwaka 2016-2017 ushamiri wa maambuziki ya VVU Mkoani Simiyu umefikia kiwango cha 3.9% ambayo ni chini ya 4.7% ikiwa ni kiwango cha kitaifa

“ Tunaendelea na kazi ya kuzuia maambukizi mapya kwa kuwezesha asilimia 90 watu wanatambua hali za afya zao,  asilimia 90% ya wagonjwa wanatumia dawa na asilimia 90 nyingine kushusha kiwango cha virusi vya UKIMWI katika damu ya Mgonjwa ( Viral suppression)

Dkt. Kulemba ameongeza kuwa Mkoani Simiyu asilimia 91 ya watu wanaoishi na Virusi vya UKIMWI wanatumia dawa za kufubaza makali ya VVU na kiwango cha maambukizi katika damu zao kimeshuka, huku akitoa wito kwa wananchi kuchangia mfuko wa kudhibiti UKIMWI kwani vita dhidi ya VVU/UKIMWI ni ya kila mmoja katika jamii.

Mfuko wa Udhamini wa kudhibiti ukimwi ulianzishwa Mwaka 2015, Kusudi la Mfuko huu ni kuchangia fedha kwa ajili ya kuboresha huduma za VVU na UKIMWI.

MWISHO

KUPATA PICHA ZAIDI FUNGUA KIUNGANISHI:-https://simiyuregion.blogspot.com/2020/07/tacaids-yakabidhi-masanduku-10-ya.html

Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa