• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

Suluhu ya Mgogoro kati ya Mwekezaji MWIBA Holdings na Wannachi Meatu yapatikana

Posted on: March 26th, 2017

Hatimaye suluhu ya mgogoro baina ya mwekezaji wa kampuni ya MWIBA Holdings na wananchi wa vijiji saba vinavyounda Jumuiya ya Hifadhi ya Wanyamapori (WMA) ya Makao wilayani Meatu, juu ya utata wa mkataba wa kumiliki ardhi, uanzishwaji wa ranchi ,mahusiano mabovu  na kusogezwa  kwa alama za mipaka katika makazi ya wananchi  imepatikana

Suluhu hiyo imepatikana baada ya kufanyika kikao cha pamoja wilayani Meatu kati ya Kamati ya Siasa ya CCM, Viongozi na Watendaji wa Serikali (Wilaya ya Meatu na Mkoa wa Simiyu), Mwakilishi wa Ofisi ya Waziri Mkuu, Watendaji wa Kampuni ya MWIBA Holdings na Viongozi wa Vijiji vinavyounda Jumuiya ya Hifadhi ya Wanyamapori ya Makao, ambacho kimeongozwa na Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka

Pande zote mbili (Mwekezaji na wananchi) zimekubaliana kuondoa kesi inayohusu mgogoro huo kwa Msuluhishi Jaji Mstaafu Thomas Mihayo na kurejea tena katika meza ya  maridhiano ili kujadili namna ya kuondoa tofauti na dosari zote zilizoonekana awali.

Mtaka ameipongeza Kampuni ya MWIBA Holdings kurejea katika meza ya mariadhiano na wananchi na ameagiza kufanyika mabadiliko katika Menejimenti ya Kampuni hiyo  kwa kuwa baadhi ya watendaji wametajwa kuwa chanzo cha migogoro ambayo imekuwa ikiwanufaisha wao wenyewe  huku ikichochea uhasama kati ya kampuni hiyo na wananchi

“....Nawaeleza Wakurugenzi, baadhi ya wasaidizi wenu wanawachafua sana, wanatengeneza migogoro na wananchi wetu kwa manufaa yao wenyewe; mkitaka kufanya kazi na sisi chukueni hatua kwa watumishi wenu, tunataka wawekezaji lakini hatuko tayari kuona wananchi wananyanyaswa kwa namna yoyote ile” alisema Mtaka.

Naye Mbunge wa Jimbo la Meatu Salum Khamis amesema  nia yake ni kuona wananchi hawabugudhiwi hivyo akatoa rai kuwa maridhiano yatakayofanyika kati ya pande hizo mbili yafanyike kwa umakini sana ili makubaliano yatakayofikiwa yalinde haki za wakazi wa Meatu na yasiwe chanzo cha migogoro.

Wakati huo huo baadhi ya wananchi wamesema mipaka waliyoshiriki kuweka wakati wa uanzishwaji wa Jumuiya ya Hifadhi ya Wanyamapori (WMA) ya Makao, ilitolewa kinyemela na watumishi wakiwemo viongozi wa Jumuiya hiyo kwa kushirikiana na mwekezaji huyo na kusogeza nyuma alama hizo kwa kilomita 10 kutoka eneo la hifadhi kuelekea eneo la makazi ya wananchi

Wananachi hao wamesema kuwa mipaka ambayo imekuwa ikileta migogoro ni mpaka ulioko katika kijiji cha Bulongoja kwenye bikoni namba 314, ambapo walisema kuwa bikoni hiyo iliondolewa na kusogezwa nyuma zaidi ya kilometa 10 kutoka ndani ya hifadhi kuelekea kwenye makazi yao.

Akitoa ufafanuzi wa suala hilo, Katibu Tawala Mkoa, Ndg.Jumanne Sagini amesema atatuma timu ya wataalam Ngazi ya Mkoa ambao watashirikiana na wataalam wa wilaya ya Meatu watakaokwenda kuhakiki mipaka hiyo  kwa kuzingatia ramani na kuirejesha ilipokuwa, huku akisisitiza wataalam hao kuzingatia weledi.

Kwa upande wake Mkurugenzi kutoka Makampuni ya Friedkin Game Tracker Safaries na Mwiba Holdings Company Abdulkadir Mohamed amekubali kumaliza mgogoro huo na kufanya mabadiliko ya menejimenti yake  ili waweze kufanya uwekezaji wa utalii na mazingira kwa uhuru.

Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Simiyu, Mhe.Dkt.Titus Kamani amewasa viongozi na watendaji wa Serikali mkoani humo kutekeleza wajibu wao katika kuwaletea wananchi maendeleo na wasiruhusu kwa namna yoyote migogoro ikachukua nafasi kubwa kuliko maendeleo ya wananchi.

Jumuiya Hifadhi ya wanyamapori Makao inaundwa na vijji saba ambavyo ni Makao, Sapa, Mwangudo, Mbushi, Iramba ndogo, Jinamo na Mwabagimu.

Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa