• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

SUA Yaahidi Kusaidia Kuanzisha Kituo cha Kupima Kifua Kikuu kwa Kutumia Panya Simiyu

Posted on: August 27th, 2020

Chuo Kikuu cha Kilimo Sokoine (SUA) kimeahidi kuwa kiko tayari  kuanzisha kituo cha kupima  makohozi  kwa kutumia panya waliofundishwa kubaini vijidudu vya Ugonjwa wa Kifua Kikuu ambao wanaweza kupima sampuli nyingi kwa wakati mmoja ikilinganishwa na vipimo vya maabara.

Hayo yamebainishwa jana na Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu, Bi. Mmbaga kikao kazi cha tathmini ya utekelezaji wa mradi wa kudhibiti kifua kikuu ngazi ya jamii uliokuwa ukitekelezwa  na mkoa wa Simiyu kwa kushirikiana  na shirika lisilo la  Kiserikali la Management and Development for Health (MDH),  kwa miaka mitatu  kuanzia Januari 2018 na unatarajiwa kuhitimishwa Desemba 2020, ambacho kilifanyika jana Mjini Bariadi.

“Tumeona ni muhimu tukaangalia tunavyoweza kutumia teknolojia nyingine kufanya  upimaji wa Ugonjwa wa Kifua Kikuu, kwa mfano tumepata fursa ya kushirikiana na wenzetu wa SUA kipindi cha nanenane mwaka huu  wamesema wako tayari kutusaidia kuanzisha kituo cha upimaji wa makohozi kwa kutumia panya waliofundishwa,” alisema Mmbaga.

Aidha, Mmbaga amesema mkoa wa Simiyu umeonekana kufanya vizuri katika kuwafikia wagonjwa wa Kifua kikuu ikilinganishwa na mikoa mingine saba ambayo yote inatekeleza mradi wa kudhibiti kifua kikuu ngazi ya jamii chini ya shirika lisilo la  Kiserikali la Management and Development for Health (MDH) ambapo umevuka lengo na kuwafikia wananchi kwa asilimia 102.

Pamoja na mafanikio hayo Mmbaga ameelekeza wataalam wafanye tathmini ya malengo yao na waweke malengo mapya yatakayokusudia kuwafikia wananchi wengi wenye uhitaji, ili kupata jamii yenye afya itakayotekeleza kwa vitendo azma na dira ya mkoa ya kuwa mkoa wenye uchumi shindani kwa kutumia rasilimali na fursa zilizopo.

Kwa upande wake Mratibu wa Huduma za kudhibiti Kifua kikuu na Ukoma, Dkt. Emmanuel John amesema kwa mwaka 2019 Mkoa wa Simiyu ulikuwa na lengo la kuwafikia wagonjwa wa Kifua Kikuu 1631 ambapo mpaka kufikia mwezi Desemba 2019 wagonjwa takribani  1673 walikuwa wamefikiwa sawa na asilimia 102 ya lengo.

Dkt. John ameongeza kuwa katika wagonjwa waliokuwa wameanzishiwa matibabu kwa mwaka 2018/2019  asilimia 72 waliweza kupona kabisa, huku akibainisha kuwa katika asilimia 28  baadhi yao walifariki, baadhi walipotea katika mifumo ya matibabu (watoro); huku akiweka bayana kuwa kwa mwaka 2020,  lengo la Mkoa ni kuwafikia wagonjwa 1779.

Naye Kaimu Mganga Mkuu wa Simiyu, Dkt. Khamis Kulemba amesema kuwa wataalam wa afya ngazi ya mkoa na halmashauri watahakikisha wanafanya marejeo ya malengo yao yaweze kuakisi hali halisi ya mahitaji ya jamii ili wananchi wengi waweze kufikiwa na huduma za upimaji na matibabu ya Kifua Kikuu.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Shirika lisilo la Kiserikali la Management and Development for Health (MDH), Bw. Eliamin Busara amesema katika awamu ijayo shirika hilo linatarajia kujikita zaidi katika mpango wa Kifua Kikuu na uboreshaji wa huduma za mama na mtoto hususani katika kuzuia maambukizi ya Virusi vya UKIMWI.

Wakati huo huo Busara ametoa wito kwa Serikali kupitia halmashauri kuwa na mipango ya namna ya kuendeleza huduma zilizokuwa zikitolewa kwa wananchi kupitia mradi huo ili huduma za afya zisitetereke hususani katika upimaji na matibabu ya Kifua Kikuu.

MWISHO

KUPATA PICHA ZAIDI FUNGUA KIUNGANISHI HIKI:-http://simiyuregion.blogspot.com/2020/08/blog-post_5.html

Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa