• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

Simiyu yawahakikishia Wadau Upatikanaji wa Miundombinu Uwanja wa Nanenane

Posted on: May 13th, 2018

Mkoa wa Simiyu umewahakikishia wadau wote wa Maonesho ya Nanenane upatikanaji wa miundombinu yote muhimu hususani  miundombinu ya maji, umeme na barabara katika Uwanja wa Maonesho ya Nanenane Kanda ya Ziwa Mashariki uliopo eneo la Nyakabindi Mjini Bariadi, ambapo Mkoa huo utakuwa mwenyeji wa Maonesho hayo Kitaifa mwaka 2018.

Hayo yamebainishwa na Katibu Tawala Mkoa wa Simiyu, Ndg. Jumanne Sagini alipokutana na Kamati ya Maadalizi ya Maonesho Nanenane kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi, ambao walitembelea uwanja huo na kupewa eneo ambalo litatumika na wizara hiyo kuonesha shughuli zake.

Sagini amesema viongozi wa Mkoa kwa kushirikiana na viongozi wa Taasisi nyingine za Serikali wameshafanya mazungumzo na kuweka mipango ya namna kila Taasisi itakavyoshiriki katika kuhakikisha miondombinu ya maji, umeme na barabara inawekwa vizuri ili kufanikisha Maonesho hayo

“Tumeshazungumza na TANESCO na wako tayari kuteremsha Transifoma kwenye eneo lile ili tupate umeme, tumezungumza na Mamlaka za Maji ili tupate fedha za kuchimba kisima kirefu cha maji ya kutosheleza wadau wetu na kuhusu barabara tumezungumza na TANROADS na TARURA, tunatarajia wiki mbili zijazo mambo yatakuwa tofauti pale” alisema Sagini.

Aidha, Sagini amesema pamoja na kushughulikia miundombinu, Mikoa ya Simiyu, Mara na Shinyanga ambayo inaunda Kanda ya Nanenane ya Ziwa Mashariki, imeshafanya vikao vya wataalam na kuweka mipango mbalimbali ya kufanikisha maonesho hayo na akabainisha kuwa Mei 17,  kitafanyika kikao kikuu cha maamuzi kwa lengo la kufikia maamuzi ya nini kinafanyika kwa wakati gani na nani atakayefanya.

Wakizungumza mara baada ya kutembelea eneo la Uwanja wa Nanenane  Kanda ya Ziwa Mashariki,  wawakilishi wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi  pamoja na kupongeza uongozi wa mkoa kwa juhudi zinazofanyika, kuridhishwa na hali ya maandalizi ya uwanja wameshauri kasi ya maandalizi iongezeke ili kuendana na muda uliobaki kuelekea maonesho.

“Viwanja tumeviona viko mahali pazuri na eneo tumepewa, kwa muda uliobaki tunashauri waongeze speed(kasi) wameshaanza kugawa maeneo kwa wadau na wameshaanza kuyasafisha, lakini waharakishe kuweka miundombinu ya maji,barabara na umeme” alisema Merry Yongolo Mratibu wa Maonesho ya Nanenane Wizara ya Mifugo na Uvuvi.

“Natoa pongezi kwa Mkoa wa Simiyu kwa kukubali kuwa mwenyeji wa Nanenane mwaka huu hii ni fursa waitumie, sisi kama wizara pia tunaona hii ni fursa hasa katika kukutana na wafugaji na wavuvi na kutatua changamoto zinazowakabili; ili tuweze kufanikisha maonesho haya maandalizi ya mapema ni muhimu sana alisema Dkt. Khamis Mkuli kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi.

Naye  Mkurugenzi wa shughuli za utafiti Kanda ya Ziwa Moses Ngendelo amesema katika maonesho hayo wanatarajia kuonesha teknolojia mpya ambazo zitawasaidia wafugaji, wakulima na wavuvi kuongeza tija katika uzalishaji, hivyo akatoa wito kwa wakulima, wafugaji na wavuvi kushiriki maonesho hayo ili waweze kuona teknolojia hizo.

Hivi karibuni Wizara ya kilimo imetangaza Kanda Mpya ya Maonesho ya Nanenane ijulikanayo kama Kanda ya Ziwa Mashariki, ambayo inajumuisha mikoa ya Simiyu, Mara na Shinyanga na Uwanja utakaotumika kwa ajili ya Maonesho hayo uko Eneo la Nyakabindi Mjini Bariadi Mkoani Simiyu.

MWISHO

KUPATA PICHA ZAIDI FUNGUA KIUNGANISHI HIKI HAPA:-https://simiyuregion.blogspot.com/2018/05/simiyu-yawahakikishia-wadau-upatikanaji.html

Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa