• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

Simiyu Yakisiwa kutumia Shilingi 175,260,331 katika Bajeti ya Mwaka 2019/2020

Posted on: March 16th, 2019

Katibu Tawala Mkoa wa Simiyu, Bw. Jumanne Sagini amesema Sekretarieti ya Mkoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa Mkoani Simiyu zimekisia kutumia jumla ya shilingi 175,260,331/= kwa ajili ya miradi ya maendeleo, mishahara na matumizi mengineyo.

Sagini ameyasema hayo Machi 15, 2019  wakati akiwasilisha rasimu ya Mapendekezo ya Mpango wa Bajeti ya mwaka 2019/2020 katika kikao maalum cha Kamati ya Ushauri ya Mkoa(RCC) kilichofanyika Mjini Bariadi.

Amesema katika kiasi tajwa, shilingi 41,960,264,000/= zitatumika katika miradi ya maendeleo, shilingi 18,522,914,000/= kwa ajili ya matumizi mengineyo na shilingi 114,777,153,000/= kwa ajili ya mishahara.

Aidha, Sagini amesema Mamlaka za Serikali za Mitaa zimekadiria kukusanya jumla ya shilingi 13, 004,878,000/= kutokana na vyanzo vyake vya ndani, ambapo kati ya hizo shilingi 4,745,216,000/= sawa na asilimia 36.5 zitatumika katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo na shilingi 8,259,662,000/= zitatumika kwa ajili ya uendeshaji wa Mamlaka za Serikali za Mitaa.

Ameongeza kuwa mpango wa bajeti umezingatia masuala muhimu kwa mkoa ambayo ni kusimamia na kudumisha masuala ya amani na utulivu, kuimarisha utawala bora na uwajibikaji kwa kuhakikisha uchaguzi wa Serikali za Mitaa unafanyika kwa amani na utulivu, kujenga mazingira wezeshi kwa wawekezaji wa ndani na nje, kuimarisha upatikanaji wa huduma bora za afya, elimu na maji hususani kwa wananchi waishio vijijini.

Masuala mengine ni Kuzisimamia Halmashauri ili kubuni, kuandaa maandiko na kufuatilia utekelezajiwa miradi ya maendeleo ya kuongeza kipato cha halmashauri, kuimarisha mipango ya matumizi bora ya ardhi,kuendeleza ujenzi wa ofisi, nyumba za viongozi na hospitali za wilaya Itilima, Bariadi na Busega.

Pamoja na hayo mpango huu umezingatia kuimarisha upatikanaji wa huduma za kijamii na kiuchumi, kuimarisha usimamizi wa mapato ya ndani na kuibua vyanzo vipya, kuhuisha mipango mkakati ya mkoa na halmashauri na kuanza kutekeleza dhana ya kuimarisha utendaji wa kuongeza tija katika utekelezaji wa kazi na miradi ya kiuchumi.

Awali akifungua kikao cha Kamati ya Ushauri ya Mkoa, Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt.John Magufuli kwa kutoa fedha kwa ajili ya ujenzi wa majengo ya Hospitali ya Rufaa ya Mkoa na Hospitali tatu za Wilaya mkoani hapa.

“Tunamshukuru Mhe. Rais kwa kutoa fedha kwa ajili ya ujenzi wa majengo ya Hospitali ya Rufaa ya  Mkoa na pia tumepata shilingi bilioni 4.5 kwa ajili ya ujenzi wa Hospitali za Wilaya ya Bariadi, Busega na Itilima” alisema  Mtaka .

Katika hatua nyingine Mtaka  amewapongeza Wabunge wa Mkoa huu kwa namna wanavyoshiriki katika kuhimiza shughuli za maendeleo huku akiwataka viongozi wote kuwaunga mkono ikiwa ni pamoja na Wakurugenzi wa Halmashauri zote mkoani humo kujipambanua katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo ambayo itawasaidia kuongeza kipato, huku ikiipongeza wilaya ya Maswa kwa kuanza utekelezaji wa ujenzi wa kiwanda cha vifungashio na upanuzi wa kiwanda cha chaki miradi ambayo itakuwa chanzo cha uhakika cha mapato kwa Halmashauri.

Wajumbe mbalimbali waliohudhuria katika kikao cha Kamati ya Ushauri ya Mkoa waliunga mkono mapendekezo ya bajeti ya mwaka 2019/2020 huku wakisisitiza Halmashauri kuwa na miradi ya kimkakati ili ziweze kupata vyanzo vipya vya mapato na wananchi kujiunga na bima ya afya ili kujihakikishia huduma za matibabu.

“Ninashauri Halmashauri ziwe na mradi ya kimkakati itakayoziongezea mapato yao ya ndani kama ilivyofanya Maswa ambayo inaenda kuwa na viwanda vikubwa viwili cha chaki na kiwanda cha vifungashio,  tena hasa nashauri kasi iongezeke hapa Bariadi ambapo ndiyo sura ya Mkoa”alisema Gungu Silanga Mjumbe wa Halmashauri kuu ya CCM Taifa,kupitia Simiyu.

“Mhe. Mkuu wa Mkoa naunga mkono suala la kuhamasisha wananchi wetu kujiunga na Bima ya Afya tena natoa wito kwa viongozi wenzangu tuwe mabalozi kwa wananchi wetu tuwaelimishe na kuwahamasisha kujiunga na Bima ya Afya ili wawe na uhakika wa kupata matibabu”alisema Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Meatu, Mhe. Pius Machungwa.

MWISHO

KUPATA PICHA ZAIDI FUNGUA KIUNGANISHI HIKI:-https://simiyuregion.blogspot.com/2019/03/simiyu-yakisiwa-kutumia-shilingi.html

Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa