• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

Simiyu Yajipanga Kuongeza Upatikanaji wa Huduma za Ugani Kuongeza Tija Kwenye Uzalishaji wa Pamba

Posted on: July 18th, 2020

Katika kutekeleza mpango Mkakati wa Mapinduzi ya Kilimo cha Pamba wa miaka mitano (2019-2024) wa Mkoa wa Simiyu, mkoa unakusudia kuongeza hali ya upatikanaji wa huduma za ugani kwa lengo la kuongeza tija katika uzalishaji kutoka kilo 175 kufikia kilo 600 kwa ekari ifikapo mwaka 2024.

Hayo yamebainishwa na Katibu Tawala msaidizi sehemu ya mipango na uratibu Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Bw. Donatus Weginah wakati akitoa mada katika mafunzo ya maafisa ugani, maafisa ushirika na viongozi waandamizi wa wilaya na Halmashauri juu utekelezaji wa mpango mkakati huo yaliyofanyika Julai 18, 2020 Mjini Bariadi.

Weginah amesema kutokana na upungufu wa maafisa ugani wapatao 200 katika mkoa wa Simiyu, mkoa unatarajia kutoa mafunzo ya muda mfupi ya kilimo bora cha pamba kwa baadhi ya vijana ili waweze kuwasaidia wakulima kulima kilimo chenye tija hususani katika maeneo ambayo hakuna maafisa ugani.

“Tunataka kuongeza uzalishaji kutoka wastani wa kilo 175 zinazozalishwa sasa hivi mpaka kufikia kilo 600 kwa ekari ifikapo mwaka 2024, ili tuweze kufikia hapo ni lazima tuhakikishe huduma za ugani ambazo ni changamoto zinapatikana, tutatumia vijana ambao watapa mafunzo ya muda mfupi ili waweze kuwapatia elimu wakulima wetu huko vijijini,” alisema Weginah.

Aidha, Weginah amebainisha kuwa mafunzo yataanza kwa vijana wataohudumia Vyama vya Msingi vya Ushirika (AMCOS) 26 vilivyochaguliwa kuwa maeneo ya mfano ya kuanzia (pilot areas) kwa mwaka huu na baadaye kuanzia mwaka 2021 vijana hao watapelekwa katika mkoa mzima hususani katika maeneo yenye upungufu mkubwa wa maafisa ugani.

Afisa ugani wa kata ya Chinamili wilayani Itilima, Bw. Gaudence Mlay amesema vijana hao watakaopewa mafunzo pamoja na wakulima wawezeshaji watawasaidia maafisa ugani katika utoaji wa elimu kwa wakulima na watawafikia wakulima wengi zaidi kuliko ilivyo sasa ambapo katika baadhi ya maeneo afisa ugani mmoja anahudumia vijiji vitatu mpaka vinne.

Kwa upande wake Afisa Ushirika wa Halmashauri ya mji wa Bariadi, Bw. Billwater Mbilinyi amesema mkakati wa mapinduzi ya kilimo cha pamba umeanza kutekelezwa kwa kuwatambua wakulima, ukubwa wa maeneo wanayolima na mahitaji ya pembejeo jambo ambalo litasaidia wakulima kupata kiasi cha pembejeo kinachotakiwa  kwa wakati.

Wakati huo huo Mrajisi Msaidizi wa Vyama vya Ushirika mkoa wa Simiyu, Bw. Ibrahimu Kadudu amesema katika utekelezaji wa mkakati huo mkoa wa Simiyu utahakikisha unasimamia matumizi ya mizani za kidijitali ambazo zitatatua changamoto ya mizani kuchezewa hivyo mkulima atapata kile anachostahili kupata wakati anapouza pamba yake.

Awali akifungua mafunzo hayo Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Mhe. Festo Kiswaga amesema mpango mkakati huo umekuja katika kipindi muafaka huku akitoa wito kwa wananchi, viongozi wa serikali, iongozi wa dini na wadau wengine wa pamba kuunga mkono utekelezaji wa mkakati huu kwa manufaa ya mkoa na Taifa kwa ujumla.

Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu, Mhandisi, Mashaka Luhamba akifunga mafunzo hayo amewataka washiriki wote wa mafunzo hayo kila mmoja akatimize wajibu wake katika kutekeleza mkakati huo kwa lengo la kufikia matokeo yaliyotarajiwa ikiwa ni pamoja na kuongeza tija ya kilimo cha pamba  kwa wakulima.

Mkakati wa Mapinduzi ya Kilimo cha Pamba wa miaka mitano (2019-2024) wa Mkoa wa Simiyu ulizinduliwa rasmi tarehe 05  Machi 2020 na Naibu Waziri wa kilimo, Mhe. Hussein Bashe, ambapo utekelezaji wake umeanza na Vyama vya msingi vya ushirika (AMCOS)  26 na baadaye utatekelezwa katika mkoa wote wa Simiyu.

MWISHO

KUPATA PICHA ZAIDI FUNGUA KIUNGANISHI HIKI:-https://simiyuregion.blogspot.com/2020/07/simiyu-yajipanga-kuongeza-upatikanaji.html

Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa