• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

Simiyu Yajipanga Kimkakati Kuwasaidia Wafugaji Kufuga Kisasa

Posted on: July 28th, 2017

Serikali Mkoani Simiyu imejipanga  kuweka mkakati maalum utakaowasaidia wafugaji mkoani humo kutoka kwenye ufugaji wa kuhama hama na kufanya ufugaji wa kisasa wenye tija.

Hayo yamebainishwa na Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka katika kikao maalum cha viongozi wa Serikali, viongozi wa dini, wafugaji, wataalam na wadau mbalimbali wa mifugo kutoka ndani na nje ya mkoa  kilichofanyika katika Ukumbi wa Kanisa Katoliki mjini Bariadi.

Mtaka amesema Mkoa wake umedhamiria kuwatambua wafugaji na maeneo yao na kutoa elimu juu ya upimaji wa maeneo hayo ili yatumiwe kufuga kisasa na kuachana na ufugaji wa kuhama hama kufuata maji na malisho katika mikoa mingine.

“Hatuwezi kuwa Serikali ambayo ina majibu mepesi kwenye mambo ya msingi, lazima tupate majawabu ya wafugaji ndani ya mkoa wetu, tufike mahali ambapo mfugaji kutoka mkoa wa Simiyu hatapigwa faini kwenye mikoa mingine kwa sababu ya kutafuta maji na malisho”amesema Mtaka.

Aidha, Mkuu huyo wa Mkoa amesema Serikali kupitia Wataalam wa Kilimo na Mifugo watatoa elimu kwa Wafugaji watakaorasimisha maeneo yao, ili wayatumie kupata malisho ya mifugo na kuweka miundombinu muhimu ya mifugo kama vile malambo, majosho na visima katika kukabiliana na changamoto ya upungufu wa maji na malisho ya mifugo.

Ameongeza kuwa, Mkoa unaandaa utaratibu ambapo shule za Serikali zitakapokuwa zinafungwa, Idara ya Kilimo na Mifugo itatumia madarasa hayo kutoa elimu ya ufugaji na kilimo bora kwa wananchi.

Sanjali na hilo, Mkuu huyo wa Mkoa amesema zoezi la kupima maeneo ya wafugaji na kuweka miundombinu muhimu ya mifugo litakapokamilika Serikali imepanga kuweka mizani katika minada yote mkoani humo ili wafugaji wasidanganywe na kuibiwa wanapouza mifugo yao.

Kwa upande wake Padre John Kasembo ambaye ni Mwezeshaji na Mshauri katika Masuala ya Uongozi, Ujasiriamali na  Maendeleo ametoa wito kwa Wafugaji wa Mkoa wa Simiyu kukubali kufanya ufugaji wenye tija na waungane na Viongozi katika mipango inayoandaliwa kwa ajili ya kufikia ufugaji bora kwa manufaa yao.

Padre Kasembo amesema ili wafugaji wafuge kisasa wanapaswa kuwa na maeneo, miundombinu ya kisasa, malisho na kufuata sheria na taratibu, hivyo akawaasa wakubali kubadilika katika namna ya kufikiri, kutenda, kuweka vipaumbele na kushughulikia changamoto ili wapate matokeo chanya.

Daktari wa Mifugo wa Sekretarieti ya Mkoa wa Simiyu, Gamitwe Mahaza amesema Wafugaji wengi pia ni Wakulima, hivyo ni vema wakatumia masalia ya mazao kwa ajili ya malisho badala ya kuyaacha mashambani yakaharibika; akasisitiza juu ya urasimishaji wa maeneo yao ili miundombinu kama visima iwekwe kusaidia ukuaji wa malisho ya asili na upandaji wa malisho ya kisasa.

Naye Mtaalam wa Mifumo ya TEHAMA kutoka Tume ya Sayansi na Teknolojia (COSTEC), Mhandisi George Mulamula ameeleza kuwa upimaji katika maeneo ya wafugaji unaweza kufanyika kwa kutumia njia mbalimbali zikiwemo zinazotumia mifumo ya TEHAMA , kama vile matumizi ya satelite na ndege zisizotumia rubani (drones) ambazo zitasaidia zoezi hilo kufanyika kwa  usahihi mkubwa na haraka.

Pia Mhandisi Mulamula amesema kupitia Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) Wafugaji wataweza kupata mafunzo na taarifa mbalimbali za mifugo kupitia simu zao za mikononi, kujua bei na soko la mifugo na kutambua mifugo yao hivyo kupunguza wizi wa mifugo.

Viongozi wa Wafugaji na Wafugaji kwa pamoja wameshukuru Uongozi wa Mkoa kuona umuhimu wa kushughulikia changamoto zao ambapo wamesema kwa kuwa wana maeneo ambayo hayajapimwa wameiomba Serikali kupitia Idara ya Ardhi kupima maeneo hayo na Idara ya Mifugo iendelee kutoa elimu ya ufugaji bora.

“Tunaushukuru sana uongozi wa Mkoa kwa kuliona hili, mimi naomba maeneo yetu yapimwe na sisi wafugaji tuelimishwe kufuga kisasa, wafugaji wengi tuna maeneo ila ng’ombe tumewapeleka mikoa mingine kwa sababu hatujui tunayatumiaje maeneo yetu, wataalam watuelimishe namna ya kuyatumia” amesema Yohana Mnyumba, Mfugaji kutoka Wilaya ya Bariadi.

 Mkoa wa Simiyu ni moja ya Mikoa inayoongoza kwa kuwa na mifugo mingi hapa nchini, hali inayopelekea baadhi ya Wafugaji kuhamia maeneo mengine ili kutafuta malisho, hivyo Serikali imedhamiria kuona wafugaji Mkoani humo wanaondokana na ufugaji wa mazoea na kuingia kwenye ufugaji wa kisasa wenye tija

Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa