• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

Simiyu yaidhinishiwa Bilioni 13 Matengenezo ya Barabara, Miradi ya Maendeleo

Posted on: December 15th, 2018

Mkoa wa Simiyu umeidhinishiwa jumla ya shilingi bilioni 13.1 kwa ajili ya matengenezo ya barabara na  miradi ya maendeleo katika bajeti ya mwaka 2018/2019.

Hayo yamebainishwa na Meneja wa Wakala wa Barabara (TANROADS)'Mkoa wa Simiyu, Mhandisi. Albert Kent wakati akiwasilisha taarifa katika Kikao cha Bodi ya Barabara ya Mkoa, kilichofanyika Desemba 14, 2018 Mjini Bariadi.

Kent amesema kati ya fedha hizo shilingi bilioni 11.461 zimeidhinishwa kwa ajili ya matengenezo ya barabara kutoka katika mfuko wa barabara na shilingi bilioni 1.595 utekelezaji wa miradi 12 ya maendeleo  yenye urefu wa kilometa 78.2.

Aidha, Kent amezungumzia maendeleo ya ujenzi wa daraja la mto Sibiti na kubainisha kuwa ujenzi wake umefikia asilimia 85 na jitihada zinaendelea kufanyika, ili ifikapo mwezi Machi, 2019 liwe limekamilika kama ilivyoelekezwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. John Pombe Magufuli mwezi Septemba, 2018 wakati akiweka jiwe la msingi la ujenzi wa daraja hilo.

Naye Mratibu wa Wakala wa Barabara Mijini na Vijijini (TARURA), Mhandisi. Salvatory Yambi amesema katika bajeti ya mwaka 2018/2019 Mkoa wa Simiyu umeidhinishiwa jumla ya shilingi bilioni 5.4 na kubainisha kuwa hadi sasa TARURA inaendelea kutekeleza miradi 29 yenye thamani ya zaidi ya shilingi bilioni 3.6 ambayo ipo katika hatua mbalimbali za utekelezaji.

Awali akifungua kikao cha Bodi ya Barabara kwa niaba ya Mwenyekiti wa kikao hicho na Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka, Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Mhe. Festo Kiswaga amepongeza TANROADS na TARURA kwa kazi kubwa wanayoifanya mkoani humo, hususani katika kusimamia ujenzi na matengenezo barabara hali iliyochangia kuufungua mkoa na kuchochea kukua kwa uchumi.

Akichangia hoja katika kikao hicho, Mbunge wa Bariadi, Mhe. Andrew Chenge ameshauri kuwepo na uhusiano wa karibu kati ya TARURA na Halmashauri hususani katika maandalizi ya Bajeti, ili vipaumbele vya TARURA vizingatie vipaumbele vya Halmashauri ambao ndio wanaokutana na wananchi moja kwa moja na kujua mahitaji yao.

Naye Katibu Tawala wa Mkoa Simiyu, Jumanne Sagini ametoa wito kwa Wakurugenzi wa halamshauri kutenga fedha kwa ajili ya matengenezo ya barabara ambazo haziko chini ya TARURA hususani katika kipindi hiki cha maandalizi ya bajeti.

Katika kikao hiki pia wajumbe mbalimbali walipata nafasi ya kuchangia hoja ambazo zililenga kuboresha miundombinu ya barabara na madaraja, masuala yote ambayo Mhandisi Kent alieleza kuwa yatafanyiwa kazi na yanayohitaji hatua zaidi kutoka katika wizara yenye dhamana yatafikishwa.

"Nashauri wananchi washirikishwe katika zoezi la uwekaji wa alama za vivuko wakati barabara ya Maswa-Bariadi itakapokamilika ili viwekwe mahali penye uhitaji" Mkuu wa Wilaya ya Maswa, Mhe. Dkt. Seif Shekalaghe

"Ili daraja la Sibiti liweze kuleta tija zaidi tunaomba TANROADS iandae mpango wa dharura wa kujenga daraja la Mto Itembe ili kuwaondolea adha wananchi  waweze kuvuka kutoka eneo moja kwenda kwingine pindi mvua zinaponyesha." Mhe. Leah Komanya, Mbunge wa Viti Maalum CCM.

Mwenyekiti Halmashauri ya Mji wa Bariadi, Mhe. Robert Lweyo ameshauri  ijengwe  round about (mzunguko) Mjini Bariadi katika makutano ya barabara ya Ngulyati-Bariadi, Lamadi- Bariadi na Maswa-Bariadi, jambo ambalo Mhandisi Kent aliahidi kuliandikia barua na na kuliwasilisha katika wizara yenye dhamana na ujenzi.

MWISHO

KUPATA PICHA ZAIDI KUHUSU HABARI HII FUNGUA KIUNGANISHI HIKI:-https://simiyuregion.blogspot.com/2018/12/simiyu-yaidhinishiwa-bilioni-13.html

Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa