• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

Simiyu Yafanikiwa Kusajili na Kutoa Vyeti vya Kuzaliwa kwa Watoto 337,662

Posted on: July 11th, 2018

Mkoa wa Simiyu umeweza kusajili jumla ya watoto 337,662 kwa kipindi cha miezi mitatu iliyopita sawa na asilimia 91.7 ya watoto waliotarajiwa kusajiliwa, chini ya mpango wa Usajili wa watoto wa umri chini ya miaka mitano, unaotekelezwa kwa ushirikiano wa Wizara ya Katiba na Sheria (RITA), Wizara ya Afya, Ofisi ya Rais TAMISEMI pamoja na wadau wengine..

Akizungumza katika  kikao cha Tathmini  kuhusu utekelezaji wa mpango wa usajili wa vizazi kwa watoto wa umri  chini ya miaka mitano, Kaimu Afisa Mtendaji Mkuu wa RITA Bi.  Emmy Hudson amesema kabla ya mpango huo Mkoa wa Simiyu ulikuwa na usajili wa chini kwa asilimia 5

“Kwa mujibu wa takwimu mpaka sasa Mpango huu katika Mkoa wa Simiyu umeweza kusajili watoto 337,662 ambao ni sawa na asilimia 91.7 ya watoto wote waliotarajiwa kusajiliwa...hii ni dhahiri kuwa ni mafanikio makubwa kwani kabla ya kuanza kwa mpango kulikuwa na asilimia 5 tu ya watoto waliokuwa wamesajiliwa na kupata vyeti vya kuzaliwa”...Alisema

Aidha, Hudson alisema kuwa mbali na mafanikio hayo yaliyopatikana  ni lazima kila Halmashauri kuendeleza mpango huo  kwani bila hivyo watakuwa wanarudisha  nyuma jitihada za serikali la kufikia usajili wa watoto wa miaka mitano kuwa asilimia 100.

Akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka, Katibu Tawala wa Mkoa huo, Bw.  Jumanne Sagini  alisema kuwa pamoja na mkoa huo kufikia asilimia hiyo 91 ,ni vema sasa halmashauri zikajitahidi kufikisha lengo la usajili kwa asilimia 100.

Sagini pia alizitaka Halmashauri zote ziweke mipango mikakati ya namna ya kuendeleza usajili huo wa watoto chini ya miaka mitano na kuweka katika mipango ya bajeti kwani hazitaweza kufadhiliwa miaka yote.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Mhe. Festo Kiswaga amesema kuwa zoezi la usajili katika wilaya yake liliendeshwa vizuri ingawa kulikuwa na changamoto kadhaa ambazo zilitatuliwa kwa kadri zoezi la usajili lilivyokuwa likiendelea na kuiwezesha wilaya hiyo kufanya vizuri pia.

Kiswaga ameeleza kuwa kupitia matokeo hayo ya mpango wa usajili ndani ya miezi mitatu utasaidia kuchochea maendeleo ya Mkoa  na Taifa kwa ujumla, kutokana na kuwepo kwa takwimu na taarifa za watoto wa chini ya mikaa mitano zitakazotumika kupanga mipango ijayo ya maendeleo ngazi zote.

Aidha, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Meatu, Bw. Fabian Manoza amewapongeza RITA kwa kusimamia mpango huo ambao utasaidia kuboresha na kupanga mikakati ya Serikali hususani katika sekta ya afya kwa kuwezesha upatikanaji wa takwimu za watoto wenye umri chini ya miaka mitano .

“Naamini kuwa kwa sasa tutaweza kupanga mipango yetu vema kwani mwanzoni tulikuwa tunapata shida sana  wakati wa kupanga mipango ya afya, hususani katika ugawaji wa chanjo kwa watoto, kutokana na kukosa takwimu sahihi za watoto...”Alisema Manoza

Aliongeza kuwa katika kipindi hicho cha miezi mitatu walikusudia kuwafikia watoto 68,000  lakini waliofikiwa ni 63,000 kutokana na changamoto mbalimbali ikiwemo mvua ambayo ilisababisha baadhi ya maeneo kutokufikika, huku akibainisha mkakati wa kuendeleza usajili na kuongeza wigo wa kuwafikia wananchi kwa karibu kupitia Ofisi za Vijiji.

Mpango wa Usajili na kutoa vyeti vya kuzaliwa kwa watoto wa umri chini ya miaka mitano ulianza kutekelezwa Mwezi Machi 14 mwaka huu mkoani Simiyu,  ambapo kwa mikoa ya Mara na Simiyu, ulizinduliwa rasmi na Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Prof. Palamagamba Kabudi Mjini Musoma Mkoani Mara Machi 20, 2018.

MWISHO

 KUPATA PICHA ZAIDI ZA KIKAO HIKI FUGUA KIUNGANISHI HIKI:-https://simiyuregion.blogspot.com/2018/07/simiyu-yafanikiwa-kusajili-na-kutoa.html

Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa