• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
OFISI YA MKUU WA MKOA WA SIMIYU
OFISI YA MKUU WA MKOA WA SIMIYU

.JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA .OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA OFISI YA MKUU WA MKOA WA SIMIYU

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Media Centre
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

SIMIYU WAPIGA HATUA MAPAMBANO DHIDI YA VVU NA UKIMWI, NI KATIKA UTEKELEZAJI WA MALENGO MATATU YA KIMATAIFA YA 95:95:95

Posted on: February 7th, 2024


Bariadi.

Mkoa wa Simiyu umepiga hatua kubwa katika utekelezaji wa malengo matatu ya kimataifa ya 95:95:95 katika mapambano dhidi ya VVU na UKIMWI ambayo ni kuhakikisha Wananchi wenye maambukizi ya VVU wanatambua hali zao,utoaji wa dawa za kufubaza makali ya VVU kwa waliobainika kuwa na maambukizi, pamoja na utoaji hamasa kwa waliobainika kuwa na maambukizi kutumia Dawa.

Hayo yamebainishwa na  kaimu  Katibu Tawala Mkoa wa Simiyu Wakili Mwanahamisi Kawega   alipofungua  mkutano wa  Tathmini ya robo ya kwanza ya mwaka wa mradi  wa Afya Thabiti, wenye lengo la kupokea taarifa ya utendaji kwa kipindi cha robo ya kwanza (October-December 2023) uliofanyika katika ukumbi wa Mikutano wa Bariadi Comference lengo likiwa ni  kujadili mafanikio, changamoto na mafunzo yaliyopatikana wakati wa  utekelezaji wa mradi wa Afya Thabiti wenye lengo la kutoa huduma za  VVU/UKIMWI katika mikoa ya Simiyu na Mara.

“Lengo la kwanza la kuhakikisha wananchi wenye maambukizi ya VVU wanatambua hali zao limefikiwa kwa asilimia 100.4%, ikilinganishwa na lengo la asilimia 95%. Lengo la pili la kuwapa dawa wenye VVU limefikiwa kwa asilimia 96.7%, na lengo la tatu la kuwahimiza watu hao kutumia dawa ili kufubaza virusi vya UKIMWI limefikiwa kwa asilimia 97.4%, ikilinganishwa na lengo la asilimia 95%.” Alisema Wakili Kawega.

Aidha Wakili Kawega amewapongeza Wataalamu wa Afya Mkoani Simiyu kwa mafanikio yaliyopatikana katika utekelezaji wa malengo matatu ya kimataifa ya 95:95:95 katika mapambano dhidi ya VVU na UKIMWI ambapo amewataka kuweka mikakati madhubuti ya kuhakikisha kundi la Vijana kuanzia miaka 0-24 linafikiwa na kupatiwa hamasa ya kutosha ili waweze kujitambua na kupima Afya zao kusudi wale watakaobainika waweze kuanza matumizi ya Dawa za kufubaza makali ya VVU.

Ernest Kisandu, Mwakilishi kutoka Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) amesema Wizara itaendelea kutoa ushirkiano kwa Wadau mbalimbali wa kupambana na VVU na UKIMWI Nchini  kusudi malengo mahsusi ya kutokomeza VVU yaweze kutimia.

Kwa upande wake Mganga Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Dkt.Boniface Marwa amesema Pamoja na mafanikio hayo ipo changamoto kwa kundi la Vijana wenye umri wa  kuanzia 0 hadi 24  ambalo bado halijafikia viwango vya kutambua hali zao za VVU na kutumia dawa ambapo mkoa unajipanga kwa kushirikiana na wadau kuhakikisha kuwa kundi hilo linafikiwa.

.

Matangazo

  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 01, 2025
  • Fungua

Habari Mpya

  • SIMIYU RS WAHAMIA JENGO JIPYA LA UTAWALA NYAUMATA

    June 03, 2024
  • RC NAWANDA ARIDHISHWA NA UJENZI MRADI WA MAJI MWABUMA/MWASHATA MEATU.

    May 30, 2024
  • RC SIMIYU ARIDHISHWA NA MAENDELEO UJENZI WA MRADI WA USAMBAZAJI MAJI WA VIJIJI VYA SUNZULA, MWAMNEMA NA NGESHA WILAYANI ITILIMA,

    May 29, 2024
  • SHULE 8 ZA MSINGI ZAPATIWA VIFAA VYA TEHAMA SIMIYU.

    April 20, 2024
  • Fungua

Video

MIAKA MINNE YA RAIS DKT.SAMIA SULUHU HASSAN MKOANI SIMIYU
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • TUME YA RAIS UKUSANYAJI MAONI MABORESHO YA KODI YATUA SIMIYU
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii
  • SIMIYU- RS TV

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani
    • Video

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa