• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

SIMIYU Wamtunuku Cheti Aliyekuwa RAS Kutambua Mchango Wake Katika Elimu

Posted on: August 24th, 2020

Uongozi wa Mkoa wa Simiyu umemtunuku cheti cha shukrani aliyekuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu, Bw. Jumanne Sagini ikiwa ni kutambua mchango wake katika kukuza sekta ya elimu katika Mkoa wa Simiyu wakati wa uongozi wake, kabla ya kuteuliwa na Halmashauri Kuu ya CCM kuwa Mgombe wa Ubunge katika Jimbo la Butiama mkoani  Mara.

Akimkabidhi cheti hicho Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu, Bi. Miriam Mmbaga amesema  uongozi umetoa  cheti hicho kama alama katika kushukuru na  kuthamini mchango wa Ndugu Sagini  katika maendeleo ya sekta ya elimu na mkoa wa Simiyu kwa ujumla.

“Tunakutakia kila la heri na tunaahidi kuwa tutaendelea kuishi ndoto na dhamira ulizoshiriki kuzitengeneza ukiwa na Mkuu wetu wa mkoa Mhe. Anthony Mtaka ili kuhakikisha elimu inasonga mbele na mkoa wa Simiyu unakuwa nambari moja katika kila eneo,” alisema Bi. Mmbaga.

Akipokea cheti hicho aliyekuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu, Bw. Jumanne Sagini amewashukuru viongozi wa mkoa kwa kutambua mchango wake huku akibainisha kuwa wakati wa uongozi wake kama msimamizi mkuu wa utekelezaji wa yale waliyokuwa wakikubaliana alipata ushirikiano kutoka kwa viongozi na watendaji kuanzia ngazi ya mkoa hadi wilaya.

“ Ninawashukuru sana viongozi wa mkoa mkiongozwa na kiongozi Mkuu Mhe. Mkuu wa Mkoa kwa kutambua mchango wangu, nimefarijika kuona mimi nilipotoka Simiyu kwenda kwenye shughuli za kisiasa, yale tuliyopanga kama mkoa yametimia maana mwaka juzi tulishika nafasi ya kumi, mwaka jana tukabaki hapo lakini mwaka huu nasikia mmeshika nafasi ya tatu hongereni sana, natamani lengo la kushika nafasi ya kwanza litimie,” alisema Sagini.

Aidha, Sagini ameomba Mkoa wa Simiyu ukubali kuwa marafiki wa Wilaya ya Butiama na Mkoa wa Mara kwa ujumla,  ili kuendeleza ushirikiano kati ya wilaya na mikoa jirani; huku akitoa wito kwa viongozi wa mkoa wa Simiyu kukubali na kutoa ushirikiano pale watu wa Butiama na Mara watakapohitaji kujifunza na kupata uzoefu kutoka kwao.

Jumanne Sagini aliteuliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli  kuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu mwishoni  mwa mwezi Aprili mwaka 2016 na aliachia nafasi hiyo Julai 03 mwaka huu baada ya kuanza kushiriki mchakato wa kugombea ubunge katika Jimbo la Butiama ambapo amepewa  ridhaa na Chama Cha Mapinduzi kupeperusha bendera ya Chama hicho katika Uchaguzi Mkuu mwaka 2020.

MWISHO

KUPATA PICHA ZAIDI FUNGUA KIUNGANISHI:-https://simiyuregion.blogspot.com/2020/08/simiyu-wamtunuku-cheti-aliyekuwa-ras.html

 

Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa