• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

Simiyu kufanya Majaribio ya Kufundisha kupitia Mtandao

Posted on: May 31st, 2017

Mkoa wa Simiyu unatarajia kufanya majaribio ya kufundisha wanafunzi kwa kutumia mtandao kupitia programu itakayotengenezwa na watalaam wa Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA).

Hayo yamesemwa na Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe.Anthony Mtaka katika Maadhimisho ya Wiki ya Elimu Mkoani humo yaliyofanyika kimkoa mjini Mwanhuzi Wilayani Meatu, chini ya Kauli Mbiu “TUWEKEZE KATIKA ELIMU KWA USTAWI WA JAMII YENYE UTAALAMU WA SAYANSI NA VIWANDA KUELEKEA UCHUMI WA KATI TANZANIA”

“Tunataka tufanye majaribio,  tuanze kwa kuunganisha shule zetu za mjini wataalamu wetu wa ICT (TEHAMA) watengeneze programu,baadhi ya madarasa kama darasa la saba  tuanze kufundisha kwa kutumia mtandao” amesema.

 Wakizungumza kwa nyakati tofauti baadhi ya wanafunzi walioshiriki katika maadhimisho ya wiki ya elimu wamesema iwapo teknolojia hiyo itafanikiwa kutumika itawasaidia katika masomo yenye upungufu wa walimu hususani wa sayansi, ambapo wameiomba Serikali kuendelea kutatua changamoto ya upungufu wa vyumba vya madarasa na vifaa vya maabara ili kuwawezesha kujifunza vema masomo hayo kwa nadharia na vitendo.

 

Kwa upande wake Afisa Elimu wa Mkoa wa Simiyu, Julius Nestory amesema maadhimisho ya wiki ya Elimu yaliyoanza Mei 24 ni moja ya tathmini ya malengo yaliyowekwa Mei 2016 na miongoni mwa mafanikio ya malengo hayo ni ujenzi wa vyumba vya madarasa zaidi ya 180 chakula cha mchana kutolewa katika shule za kutwa lililotekelewa kwa asilimia 43.

Katika hatua nyingine Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe Anthony Mtaka amesema Serikali imepanga kupitia Watalaam hao wa TEHAMA pia kwa kutumia teknolojia nyepesi, itengenezwe programu itakayosaidia kutoa taarifa za uwepo wa watumishi mahala pa kazi.

Aidha ameongeza kuwa katika kipindi hiki ambacho Serikali Mkoani Simiyu imejipanga kufanya mapinduzi ya Viwanda, imedhamiria kuwatumia Watalaam wa TEHAMA kutengeneza mfumo wa taarifa na takwimu sahihi za kila sekta zikiwemo za kilimo, mifugo, elimu ili mtu akitaka taarifa yoyote ya Simiyu azipate kwa urahisi (awe nazo mkononi).

“Miaka minne ijayo hatutakuwa na Simiyu mnayoiona leo, kama kuna mtu anafikiri ni maneno atupe muda; tunataka tuwapunguzie Watanzania kufanya rejea nchi nyingine waje kwenye mkoa wetu. Tarehe 09/05/2017 Maswa wanapokea hundi ya shilingi Bilioni 1.5 kwa ajili ya ujenzi wa kiwanda cha chaki Maswa, Meatu upembuzi yakinifu unaanza tarehe 12/06/2017 ujenzi wa kiwanda cha maziwa” amesema.

Wakati huo huo Mkuu huyo wa Mkoa amesema Serikali inalitafutia ufumbuzi wa kudumu suala la bei ya pamba ambalo limekuwa likiwakatisha tamaa wakulima kwa kuwa wafanyabiashara wananunua pamba kwa bei ya chini kwa kigezo cha kuwa bei katika soko la dunia iko chini.

Mtaka amesema Simiyu inaoongoza kwa kulima pamba lakini Halmashauri na wananchi hawanufaiki kwa kiwango kinacholingana na uzalishaji uliopo, hivyo watatafutwa watalaam ambao watachunguza bei ya pamba katika soko la dunia na akasisitiza kuwa mfanyabiashara yeyote atakayeona pamba haina faida kwake aache katika Msimu wa mwaka 2018 Halmashauri zitanunua.

Wiki ya Elimu huadhimishwa kila mwaka mwezi Mei ikiwa na lengo la kuwakutanisha wadau wa elimu, kuona shughuli mbalimali za elimu, kufanya tathmini ya mipango ya elimu ya mwaka uliopita na kuweka mipango ya mwaka mwingine.

Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa