• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

Simiyu Kufanya Majaribio Kutumia Vyeti vya Vyuo Vikuu Kudhamini Mikopo

Posted on: November 16th, 2020

Katika kukabiliana na changamoto ya ajira kwa vijana mkoa wa Simiyu umejipanga kufanya majaribio ya kutumia vyeti vya taaluma kwa wahitimu wa vyuo vikuu kama dhamana ya mikopo ili kuwawezesha  kupata mitaji na kujiajiri kupitia sekta ya kilimo na viwanda.

Hayo yamebainishwa na Mkuu wa Mkoa wa Simiyu alipokutana na baadhi ya vijana jana Novemba 15, 2020 mjini Bariadi kwenye mjadala wa ukosefu wa ajira kwa vijana na mapendekezo ya suluhisho la changamoto hiyo ambao ulihudhuriwa pia na wadau wa maendeleo akiwemo  Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Maendeleo ya Umoja wa Mataifa(UNDP), Bibi. Christine Musisi.

“Tunataka (tu pilot) tufanye majaribio na tutakuwa (number one) wa kwanza, tutawafuata wadau (UNDP) kuwaeleza kuwa tumekuja na namna ya kuwasaidia vijana waliomaliza vyuo vikuu ili tuone kama vyeti vyao vinaweza kusimama kama dhamana badala ya vyumba na viwanja ambavyo wao hawana,”

“Tutawaambia vijana hao wenye maandiko ya miradi  wawasilishe iwe ni kwa mtu binafsi au kikundi, tutajadiliana tuone ‘risk’ zikoje,” alisema Mtaka.

Mwakilishi Mkazi wa UNDP hapa nchini, Bibi. Christine Musisi ametoa wito kwa vijana kuhamasika kubadili mitazamo kutoka kwenye mawazo tegemezi kwenda katika mawazo ya kujitegemea wenyewe na kwenda mbele zaidi kwa kutumia rasilimali zinazowazunguka, huku akiahidi kuwa UNDP itaendelea kushirikiana na Mkoa wa Simiyu kama mdau wa maendeleo.

Baadhi ya vijana wametoa mapendekezo mbalimbali ambayo yakifanyiwa kazi na serikali, vijana wenyewe na wadau wengine yataweza kuchangia kuleta ufumbuzi wa tatizo la ajira kwa vijana.

“Tunaomba Serikali ituboreshee miundombinu ya kilimo tutoke kwenye kilimo cha kutegemea mvua twende kwenye kilimo cha umwagiliaji ili tuzalishe malighafi ya kupeleka viwandani,” alisema Adrian Paul.

“Njia nyingine ya kuongeza ajira kwa vijana na Serikali kufufua viwanda vilivyokufa na kuanzisha viwanda vipya ili iweze kuzalisha ajira kwa rika zote wakiwemo vijana,” alisema Afisa Vijana Itilima

“Elimu ya kujitegemea irudishwe na ianze kufundisha mashuleni ili kuwaanda watoto tangu wakiwa wadogo kujitegemea ili hata atakapomaliza masomo akakasa ajira aweze kujiajiri mwenye na kujitegemea,” alisema Asia Kimaro kutoka Wilayani Maswa.

Mkurugenzi wa Miradi kutoka UNDP, Bw. Amon Manyama ameahidi kushirikiana na mkoa wa Simiyu katika maandiko ya miradi huku akitoa wito kwa vijana kujituma na kutokuridhika kwa kufanya kazi moja badala yake kila mmoja aone umuhimu wa kuwa kazi zaidi ya mbili.

MWISHO

KUPATA PICHA ZAIDI FUNGUA KIUNGANISHI HIKI:-https://simiyuregion.blogspot.com/2020/11/mkuu-wa-mkoawa-simiyu-mhe.html

Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa