• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

Simiyu Kuanzisha Mfumo wa Ukusanyaji, Utunzaji Takwimu za Wakulima wa Pamba

Posted on: October 19th, 2019

Mkoa wa Simiyu umeanzisha mfumo rasmi wa ukusanyaji takwimu na utunzaji wa kumbukumbu za wakulima wa pamba uitwao ‘Kilimo Maendeleo’ utakaowawezesha wakulima kusajiliwa katika Vyama vya msingi vya Ushirika (AMCOS), kuuza pamba yao kwa njia ya mtandao na kupata pembejeo zote kutoka kwa wauzaji wa pembejeo.

Akizungumza katika uzinduzi wa mafunzo juu ya mfumo huo, Meneja wa huduma za ugani kutoka GATSBY AFRICA, Bw. Sunday Mtaki amesema Mfumo huo utaanza kutekelezwa katika AMCOS 24 zilizoteuliwa kwa kuanzia.

“Katika utekelezaji wa mkakati wa miaka mitano ya mkoa wa Simiyu katika zao la pamba, eneo la usajili wa wakulima na matumizi ya TEHAMA kwenye kilimo ni muhimu sana, tumeileta kampuni inaitwa LITENGA ambayo ina mtandao unaitwa Kilimo Maendeleo kazi yake ni kuwaunganisha wakulima kupitia AMCOS na taarifa zote za mkulima zitapatikana kupitia simu za mkononi,” alisema Mtaki.

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu amesema mfumo huo ni sehemu ya utekelezaji wa mpango mkakati wa miaka mitano wa kilimo cha zao la pamba ulioandaliwa na Mkoa kwa kushirikiana na wadau, kwa lengo la kuboresha kilimo cha pamba, huku akiwataka Maafisa Kilimo na Maafisa ushirika kutimiza wajibu wao.

“Maafisa Kilimo na Maafisa Ushirika timizeni wajibu wenu msisubiri mgombane na mtu hii kazi ndiyo inayowapa heshima, Serikali ya Rais Magufuli imeweka mkakati wa kuhakikisha zao la pamba linakuwa zao muhimili kwenye nchi yetu, ndiyo maana sisi kama Mkoa tumeanza utekelezaji wa mkakati wa miaka mitano wa kilimo cha zao la pamba,” alisema Mtaka.

Aidha, Mtaka ameongeza kuwa dhamira ya mkoa ni kufanya mapinduzi katika kilimo cha pamba ili wakulima walime kilimo cha kisasa chenye tija na kuwa na ushirika imara, ambapo amesema viongozi wa AMCOS wasio waaminifu watachukuliwa hatua kwa mujibu wa sheria ikiwa ni pamoja na kuwavua nyadhifa zao.

Mwenyekiti wa Chama cha Ushirika cha Mkoa wa Simiyu (SIMCU), Bw. Charles Madata amewaonya viongozi wa AMCOS kuwa waaminifu na kuhakikisha  kila mmoja anakuwa na nidhamu ya fedha ili mali za wakulima ziweze kuwa salama.

Kwa upande wake Kaimu Mrajisi wa Vyama vya Ushirika Mkoa wa Simiyu, Bw. Ibrahimu Kadudu amesema viongozi wote wasio waaminifu watachukuliwa hatua, ambapo amebainisha kuwa takribani viongozi 107 wa AMCOS wilayani Maswa waliohusika na ubadhilifu wanatarajiwa kufikishwa mahakamani mara baada ya kukamilika kwa ukaguzi.

Naye Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu, Bw. Jumanne Sagini amesema kupitia mkakati wa miaka mitano ya mkoa wa Simiyu katika zao la pamba, mkoa wa huo unatarajia kuongeza tija ya uzalishaji wa pamba kutoka kilo 200 kwa ekari hadi kufikia kilo 600 hadi 1000 au zaidi kwa ekari.

MWISHO

KUPATA PICHA ZAIDI FUNGUA KIUNGANISHI HIKI:-https://simiyuregion.blogspot.com/2019/10/simiyu-kuanzisha-mfumo-wa-ukusanyaji.html

Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa