• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

Simiyu Kuanza Kuwaandaa Wanafunzi wa Darasa la Saba, Kidato cha Nne wa Mwaka 2019 sasa

Posted on: April 24th, 2018

Mkoa wa Simiyu umejipanga kuanza kuwaandaa Wanafunzi wa Darasa la Saba na Kidato cha Nne wa mwaka 2019 kuanzia mwezi Agosti, mwaka huu 2018 ili kufikia malengo ya kuongeza ufaulu katika mitihani yote ya Taifa.

Hayo yamebainishwa na Mkuu wa Mkoa huo Mhe. Anthony Mtaka katika Hafla fupi ya kuwapongeza walimu wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi kwa kuongeza ufaulu kwa Shule za Msingi na Sekondari kipindi cha miaka miwili mfululizo, iliyofanyika Ukumbi wa Bariadi Alliance Mjini hapa.

Mtaka amesema kutakuwa na mitihani kwa wanafunzi wa darasa la sita na kidato cha tatu mwezi Agosti 2018 ili kupata wanafunzi wenye ufaulu mzuri watakaounda darasa maalumu la darasa la saba na kidato cha nne mwaka 2019 ( special class).

"Tunaanza maandalizi ya darasa la saba na kidato cha nne wa mwakani kuanzia mwezi Agosti mwaka huu, ili tuchuje bila kupendelea mtihani ni chujio zuri, matokeo hayo yatabandikwa na wazazi wote wataona" alisema Mtaka.

Aidha, Mkuu huyo wa Mkoa amesema baada ya kumaliza kambi ya kitaaluma kwa kidato cha sita mwezi huu, Mkoa umepanga kufanya kambi za kitaaluma kwa kidato cha nne na darasa la saba ambazo zitafunguliwa rasmi tarehe 06 Juni, 2018.

Wakati huo huo amesema Serikali inaendelea kuwajengea uwezo walimu mahiri na makini ili waweze kuwasaidia wanafunzi wa madarasa maalumu kufanya vizuri lengo likiwa ni kuongeza ufaulu kwa shule za msingi na kufuta daraja la nne na sifuri kwa shule za sekondari.

Kuhusu ujenzi wa Shule ya Sekondari ya Mkoa, Mtaka amesema Mkoa utajenga shule ya Mkoa Mjini Bariadi (Makao Makuu ya mkoa) ambayo itatambulika kama Shule ya Sekondari Simiyu na itakuwa na uwezo wa kuchukua wanafunzi 1000 huku ikiwa na miundombinu mingine muhimu kama maabara, vyumba vya kompyuta na mkongo wa Taifa.

Pia amesema pamoja na kujenga Shule hiyo ya Mkoa, Serikali imedhamiria kwa kushirikiana na wananchi kujenga shule mbili maalumu kwa ajili ya wasichana na wavulana (Simiyu Girls na Simiyu Boy's) ambazo zitabeba taswira ya Mkoa na kutambulisha Mkoa huo tofauti na ilivyo sasa ambapo shule nyingi zilizopo katika Makao makuu ya Mkoa ni zile za Kata.

Katika hatua nyingine Mkuu huyo wa Mkoa amewaruhusu walimu mkoani humo kufundisha masomo ya ziada (tuition) hususani wakati wa likizo na mapumziko ili wanafunzi waendelee kujifunza badala ya kusubiri kufundishwa darasani pekee.

Akizungumza kwa niaba ya walimu wa Halmashauri ya Mji, Mwl. Travel Ndimangwa kutoka Shule ya Msingi Somanda A amepongeza utaratibu wa kuwaandaa wanafunzi wa madarasa ya mitihani pamoja na kuruhusiwa kuwafundisha wanafunzi masomo ya ziada mambo ambayo amesema yatachangia kuongeza ufaulu kwa wanafunzi.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi, Mhe. Robert Lweyo ametoa wito kwa walimu wa Halmashauri hiyo kufanya kazi kwa bidii na weledi ili kupandisha ufaulu ambapo mwaka 2017 ilishika nafasi ya 22 Kitaifa katika mtihani wa Kidato cha Nne kutoka nafasi ya 44 mwaka 2016

PICHA ZAIDI KUHUSU HABARI HII FUNGUA HAPA:-.https://simiyuregion.blogspot.com/2018/04/simiyu-kuanza-kuwaandaa-wanafunzi-wa_24.html

Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa