• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

Simiyu Itaendelea Kushirikiana na Walemavu Kuhakikisha Wanapata Huduma kwa wakati: DC Kiswaga

Posted on: June 14th, 2019

Mkuu wa Wilaya ya Bariadi Mhe. Festo Kiswaga amesema Serikali mkoani Simiyu itaendelea kufanya kazi kwa kushirikiana na watu wenye ulemavu wa makundi yote  bila kubagua na kuhakikisha wanapata huduma kwa wakati katika taasisi za Serikali wanapoenda kupata huduma.

Kiswaga ameyasema hayo Juni 13, 2019 wakati wa alipofungua kikao cha uboreshaji huduma kwa jamii ya viziwi Mkoa wa Simiyu, kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka, kilichofanyika Mjini Bariadi.

Amesema watu wenye ulemavu wana haki sawa na watu wengine hivyo akatoa wito kwa vyombo vya ulinzi na usalama pamoja na maeneo mengine ya kutoa huduma za jamii mkoani Simiyu kufanya utaratibu wa kuweka wataalam maalum wenye uelewa wa lugha ya alama ili kuondoa changamoto ya mawasiliano kwa watu wenye ulemavu hususani viziwi.

“Vyombo vya ulinzi na usalama vihakikishe vina mtu au watu kwa ajili ya kuwasaidia viziwi kuondoa changamoto ya mawasiliano pamoja na watu wenye ulemavu kwa ujumla wanaohitaji huduma, si lazima kuajiri kwa sasa kwa kuwa suala la ajira linaweza kuchukua muda; lakini wahakikishe wana mtu wa kutoa msaada viziwi wapate huduma” alisema Kiswaga.

Aidha, Kiswaga amesisitiza umuhimu wa kutoa elimu kwa viziwi kuhusu maeneo yaliyozuiwa kama vile katika vyombo vya ulinzi (majeshi) na kushauri kuwa ikiwa wanapaswa kwenda katika maeneo hayo waombe msaada kwa watu wenye uwezo wa kuzungumza ili kuepuka watu hao kuonekana kuwa wamevunja sheria kwa kukusudia kwenda maeneo hayo.

 

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Chama cha Viziwi Tanzania(CHAVITA) Mkoa wa Simiyu, Mhandi Zephania amesema viziwi wanakabiliwa na changamoto ya mawasiliano wanapoenda kupata huduma mbalimbali hivyo chama hicho kinaendelea kutoa elimu ya lugha ya alama kwa watumishi wa maeneo mbalimbali ya kutolea huduma ili kukabiliana na changamoto hiyo.

Naye Mkalimani wa lugha ya alama Bw. Jonathan Livingstone amesema Wizara ya Elimu imekubali kupokea jukumu la kusanifisha lugha ya alama iingizwe katika mitaala ifundishwe katika shule za msingi, sekondari na vyuo.

Katika hatua nyingine Kamanda wa Wilaya ya Maswa, Jonas Nyaoga amesema Jeshi la polisi limejipanga kuwahudumia viziwi kwa namna ambayo wakiwa wanahitaji huduma wanasaidiwa kwa kuhakikisha kuwa kila wanapowahoji viziwi wanatafuta watu wanaofahamu lugha ya alama ili waweze kuwatafsiria.

Kikao cha kujadili uboreshaji wa huduma za jamii kwa viziwi mkoani Simiyu kilijumuisha viongozi wa Chama cha Viziwi(CHAVITA) Mkoa wa Simiyu, Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa na Kamati za Ulinzi na Usalama za Wilaya zote tano za Mkoa wa Simiyu.

MWISHO

KUPATA HABARI KAMILI FUNGUA KIUNGANISHI HIKI:-https://simiyuregion.blogspot.com/2019/06/serikali-mkoani-simiyu-itaendelea.html

Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa