• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

Siku ya Wakunga Duniani Kitaifa mwaka 2019 Kufanyika Simiyu

Posted on: May 4th, 2019

Maadhimisho ya Siku ya Wakunga Duniani Kitaifa mwaka 2019 yanatarajiwa kufanyika kesho katika Uwanja wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi Mkoani Simiyu, ambapo Mgeni rasmi atakuwa Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia,Wazee na Watoto, Dkt. Faustine Ndugulile akimwakilisha Makamu wa Rais wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake, Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka amewakaribisha wakunga wote hapa nchini na kuwahakikishia kuwa Mkoa umefanya maandalizi ya kutosha ili maadhimisho hayo yaweze kufana.

"Nitumie nafasi hii kama Mkuu wa Mkoa kuwaalika familia ya Wakunga wote Tanzania ambao wameanza safari kuja kwenye shughuli yao ya Kitaifa ndani ya mkoa wetu, niwahakikishie kuwa tumefanya maandalizi ya kutosha kuhakikisha shughuli yao inaenda vizuri" alisema Mtaka

Katika hatua nyingine Mtaka amelishukuru Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Idadi ya watu Duniani (UNFPA) kuwa sehemu ya kuwezesha Maadhimisho hayo Kitaifa kufanyika Mkoani Simiyu,  pamoja na  mchango mkubwa wa Shirika hilo na wadau wengine katika sekta ya afya ndani ya Mkoa.

Naye Makamu Mwakilishi Mkaazi wa UNFPA hapa nchini, Dkt.Hashina Begum amesema Kauli Mbiu ya Siku ya Wakunga Duniani mwaka 2019 inayosema"Wakunga ni Watetezi wa Haki za Wanawake" inakumbusha umuhimu wa wakunga katika kuwatetea kina mama wakati wa ujauzito, wakati wa kujifungua na baada ya kujifungua.

Ameongeza kuwa UNFPA imeendelea kushirikiana na Serikali katika ukarabati wa vituo 38 vya afya, wodi za wazazi na vyumba vya upasuaji, ununuzi wa vifaa na mashine za kumwezesha Mkunga kutoa huduma ya mama na mtoto kwa urahisi na kuwajengea uwezo wakunga 90 kutoka vituo vilivyokarabatiwa kutoa huduma za dharura kwa mama na mtoto.

Naye Rais Chama Cha Wakunga Tanzania (TAMA), Feddy Mwanga amesema TAMA inafanya kazi na Mkoa wa Simiyu kutoka mwaka 2016 kuwaelimisha Wakunga, ili waweze kutoa huduma za dharura kwa mama na mtoto hususani katika vituo vya pembezoni, huku akiishukuru UNFPA kwa mchango wake kifedha na utaalamu kuwezesha mafunzo hayo.

Ameongeza kuwa Dira ya TAMA ni kuona kuwa kila mama mjamzito anayejifungua na watoto wachanga wanahudumiwa na Wakunga wataalam na wanapata huduma bora, huku akitoa wito wananchi wa Simiyu kujitokeza kwa wingi katika Maadhimisho hayo ili waweze kupata huduma za upimaji bila malipo.

MWISHO.

KUPATA PICHA ZAIDI FUNGUA TAFADHALI KIUNGANISHI HIKI:-https://simiyuregion.blogspot.com/2019/05/siku-ya-wakunga-duniani-kitaifa.html

Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa