• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

Serikali yatoa Shilingi Bilioni 2.2 Kujenga Jengo la Mama na Mtoto Hospitali ya Rufaa Simiyu

Posted on: July 17th, 2019

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe. Ummy Mwalimu amesema Serikali imetoa jumla ya shilingi bilioni 2.2 kwa ajili ya kujenga jengo la wodi ya mama na mtoto katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Simiyu, ili hospitali hiyo iweze kutoa huduma za kulaza wanawake na watoto.

Waziri Ummy ameyasema hayo Julai 16, 2019 wakati akiwa katika ziara ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa jengo la maabara, jengo la upasuaji ambalo pia litakuwa na huduma za mionzi katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Simiyu Mjini Bariadi.

Amesema wagonjwa wengi ni wanawake na watoto wadogo hivyo ni vema wakajengewa wodi  huku akibainisha pia kuwa Serikali imeshatoa shilingi bilioni 5.7 kwa ajili ya ujenzi wa jengo la maabara na jengo la upasuaji ambalo pia litakuwa na huduma za mionzi unaotarajia kukamilika mwezi Oktoba 2019.

“Tulianza na ujenzi wa jengo la OPD, na awamu ya pili namshukuru Mhe. Rais ametoa shilingi bilioni 5.7 kwa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Simiyu kwa ajili ya ujenzi wa jengo la maabara, jengo la upasuaji ambalo pia litakuwa na huduma za mionzi”

“Sasa hivi tuna shilingi bilioni 2.2 kwenye akaunti ya Hospitali na tutaanza kujenga jengo la mama na mtoto, ili tuanze kulaza wagonjwa maana hata ukiangalia wagonjwa wengi  ni wanawake na watoto wadogo, hili la wodi za watu wengine nalo pia tunalibeba” alisema Waziri Ummy.

Aidha, Mhe. Waziri amepongeza wakala wa Majengo TBA mkoa wa Simiyu kwa kutekeleza miradi kwa wakati na kwa ubora unaotakiwa huku akimtaka Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya kurejesha fedha zilizokatwa kodi(withholding tax) wakati akilipa TBA gharama za ujenzi, ili zifanye kazi ya ujenzi maana TBA kama Taasisi ya Umma haipaswi kukatwa fedha hizo.

Naye Meneja wa TBA Mkoa wa Simiyu, Mhandisi. Likimaitare Naunga amesema ikiwa fedha kiasi cha zaidi ya shilingi milioni 204 zilizokatwa kama kodi “Withholding Tax” zikirejeshwa zitasaidia kununua vifaa vya kukamilishia majengo hayo.

Kwa upande wake mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe. Anthony Mtaka ameishukuru Serikali kwa kwa kuendelea kutoa fedha kwa ajili ya ujenzi wa majengo hayo katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Simiyu, ambayo yataendelea kuboresha huduma kwa wananchi, ambapo pia ameishukuru wizara ya afya kwa kuendelea kusimamia kwa karibu ujenzi wa majengo hayo.

Naye Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Simiyu, Mhe. Enock Yakobo amesema CCM kama wasimamizi wa utekelezaji wa Ilani wanashukuru kwa namna Serikali inavyotekeleza ilani katika kuboresha huduma za afya Mkoani Simiyu na ameahidi kuwa wataendela kufuatilia  na kusimamia  kwa karibu ili kuhakikisha huduma bora zinatolewa.

MWISHO

KUPATA PICHA ZAIDI FUNGUA KIUNGANISHI HIKI:-https://simiyuregion.blogspot.com/2019/07/serikali-yatoa-shilingi-bilioni-22.html

Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa