• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

Serikali kuzindua Mfuko wa Watu Wenye Ulemavu

Posted on: February 27th, 2019

Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia watu wenye ulemavu, Mhe. Stella Ikupa amesema Serikali inatarajia kuzindua rasmi mfuko wa watu wenye ulemavu ambao utakuwa ukishughulikia masuala mbalimbali ya watu wenye ulemavu ikiwemo kutoa ruzuku kwa vyama vya watu wenye ulemavu.

Mhe. Ikupa ameyasema hayo wakati akizungumza na viongozi na watendaji wa Serikali na  watu wenye ulemavu wakati akiwa katika ziara ya kikazi wilayani humo, Februari 26,2019.

Amesema taratibu zote zimekamilika na sasa iko katika hatua za mwisho ili mfuko huo uweze kuzinduliwa huku akibainisha kuwa Baraza la Ushauri kwa watu wenye Ulemavu Taifa nalo litazinduliwa hivi karibuni kwa kuwa tayari Mwenyekiti wa Baraza hilo ameshateuliwa na Rais wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli.

“Tayari tumeshapata Mwenyekiti wa lile Baraza la Ushauri kwa watu wenye ulemavu ambaye ameteuliwa na Mhe. Rais na tunaamini muda si mrefu lile baraza litazinduliwa na litaendelea kufanya kazi kwa mujibu wa sheria” alisema Naibu Waziri Ikupa.

Katika hatua nyingine Mhe. Ikupa amepongeza viongozi wa Wilaya ya Meatu kwa namna wanavyoshughulikia masuala ya watu wenye ulemavu na wakati huo huo akawapongeza watu wenye ulemavu wilayani humo kutumia vema fedha za mikopo wanazopata kutokana asilimia mbili za mapato ya ndani ya Halmashauri kwa kuanzisha shughuli za ujasiriamali.

Aidha, ametoa wito kwa watu wenye ulemavu kujitokeza kwa wingi kuomba mikopo hiyo ambayo haina riba ili waweze kuanzisha shughuli za ujasiriamali zitakazowasaidia kujikwamua kiuchumi na kuondokana na utegemezi.

Mkuu wa Wilaya ya Meatu, Dkt. Joseph Chilongani amesema Halmashauri ya Wilaya hiyo imetenga takribani shilingi milioni Sabini kwa ajili ya kuwawezesha kiuchumi watu wenye ulemavu na akatoa wito kwao kujitokeza kuomba mikopo ili iwasaidie kuanzisha shughuli za kuwaingizia kipato.

Kwa upande wao watu wenye ulemavu wameiomba Serikali kwa kushirikiana na wadau mbalimbali kusaidia katika utatuzi wa changamoto mbalimbali zinazowakabili ikiwa ni pamoja na ukosefu vifaa saidizi kwa watu wenye ulemavu na kutengeneza mazingira wezeshi shuleni kwa wanafunzi wenye ulemavu.

“ Tunaomba Serikali yetu kwa kushirikiana na wadau itusaidie kupata nyenzo saidizi kama fimbo nyeupe kwa wasioona, viungo bandia na baiskeli za miguu mitatu kwa walemavu wa viungo” alisema Ndimila Luyoja Katibu wa SHIVYAWATA wilaya ya Meatu.

“ Tunaomba vifaa saidizi vya kukuza maandishi kwa wanafunzi  wenye ualbino na pia walimu wawape nafasi ya kukaa mbele madarasani ili waweze kuona vizuri kama wanafunzi wengine kwa sababu wasipopata nafasi hiyo watashindwa kuona vizuri ubaoni kutokana na wao kuwa na uoni hafifu”Mwenyekiti wa Chama cha Watu wenye ualbino Meatu.

Naye Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Festo Kiswaga amesema Serikali mkoani humo itaendelea kutoa kipaumbele kwa watu wenye uelemavu ambapo amesema wataendelea kujumuishwa katika agenda ya ujenzi wa uchumi wa viwanda kufikia uchumi wa kati mkoani humo.

Akiwa Wilayani Meatu, Mhe. Naibu Waziri amezungumza na viongozi, watu wenye ulemavu, kuona kazi mbalimbali za watu wenye ulemavu na kutembelea mradi wa Kitalu nyumba ili kujionea utekelezaji wake.

MWISHO

KUPATA PICHA ZAIDI FUNGUA KIUNGANISHI :-https://simiyuregion.blogspot.com/2019/02/serikali-kuzindua-mfuko-wa-watu-wenye.html

Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa