• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

RITA Kusajili na Kutoa Vyeti Vya Kuzaliwa kwa Zaidi ya Wanafunzi 60,000 Wilayani Bariadi

Posted on: August 29th, 2018

Wakala wa Usajili, Udhamini na Ufilisi (RITA) unatarajia kusajili na kutoa vyeti vya kuzaliwa kwa wanafunzi 60,000 wa shule za Msingi za Sekondari wilayani Bariadi mkoani Simiyu, kupitia Mpango wa Usajili na kutoa vyeti vya kuzaliwa kwa watoto wa miaka 06 hadi 18.

Hayo yamebainishwa na Kaimu Afisa Mtendaji Mkuu RITA Bw. Charles Salyeem wakati wa ufunguzi wa mafunzo kwa Waratibu Elimu Kata na Maafisa Watendaji Kata  kuhusu Mpango wa Usajili na kutoa vyeti vya kuzaliwa kwa wanafunzi wa shule za msingi na Sekondari wilaya ya Bariadi mkoani Simiyu, Agosti 28, 2018  mjini Bariadi.

Salyeem amesema mpango huo utahusisha usajili na kutoa vyeti vya kuzaliwa kwa wanafunzi wenye umri wa kuanzia miaka 06 hadi 18 kwa ushirikiano kati ya RITA na Ofisi za Wakurugenzi wa Halmashauri kupitia Idara za Elimu ambapo wanafunzi watasajiliwa na kupata vyeti vya kuzaliwa katika shule zao.

Ameongeza kuwa watoto wa umri wa miaka 06 hadi 18 ambao si wanafunzi watapata fursa ya kusajiliwa katika Ofisi za Watendaji wa Kata, huku akibainisha kuwa watapaswa kuwa na viambatisho vya msingi vinavyotakiwa kwa maelekezo watakayopewa na Watendaji wa Kata kwenye maeneo yao.

Aidha, Salyeem amesema wazazi na walezi wa watoto wenye umri huo watahitajika kuchangia gharama kwa ajili ya usajili na kupata vyeti vya kuzaliwa kwa watoto wao  ili fedha zitakazopatikana  ziwezeshe kupeleka mpango huu katika maeneo mengine.

Awali akifungua mafunzo kwa Waratibu Elimu Kata kuhusu mpango huo kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka, Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Mhe. Festo Kiswaga amewatakaWaratibu Elimu Kata na Maafisa Watendaji Kata kuzingatia maelekezo watakayopewa na kufanya kazi kwa uadilifu wakitanguliza uzalendo na siyo maslahi binafsi.

Aidha,Kiswaga amesema cheti cha kuzaliwa ni moja ya nyaraka muhimu kwa wanafunzi wanaotoka hatua moja ya masomo kuingia nyingine hivyo akawataka viongozi na watendaji kujipanga ili kuvuka lengo la RITA la kusajili wanafunzi 60,000 kwa kuhakikisha kila fomu inayochukuliwa kwa ajili ya kuomba usajili inarudishwa na cheti cha kuzaliwa kinachukuliwa.

“RITA imejiwekea lengo la kusajili wanafunzi 60,000 kati ya zaidi ya 156,769 waliopo wilayani Bariadi, wanafunzi wasio na vyeti ni wengi, hivyo basi tujipange tuweze kuvuka lengo, tutumie viongozi kuhamasisha wazazi na kuhakikisha zoezi hili linafanikiwa” alisema.

Afisa Mtendaji wa Kata ya Ihusi, Kasimili Ngusa amesema mpango huu utawarahisishia wanafunzi wengi wa umri wa miaka 06 hadi 18 kwa kupata vyeti vya kuzaliwa shuleni walipo, tofauti na ilivyokuwa awali ambapo iliwalazimu wazazi na walezi kufuata huduma ya usajili na kupata vyeti vya kuzaliwa Ofisi za Mkuu wa Wilaya.

Naye Mratibu wa Elimu Kata ya Isanga, Sophia Kitobelo ametoa wito kwa wazazi na walezi kutumia fursa hiyo ya kusajili na kuchukua vyeti vya kuzaliwa shuleni na katika Ofisi za kata, kuhakikisha kuwa watoto wao wanapata vyeti vya kuzaliwa ambavyo ni miongoni mwa nyaraka muhimu kwa Watanzania.

Mkakati huu wa Usajili wa Wanafunzi wa shule za msingi na sekondari wenye umri wa miaka 06 hadi 18 umefunguliwa rasmi katika Wilaya ya Bariadi na baadaye utaendelea katika wilaya nyingine za Mkoa wa Simiyu; hadi sasa umeanza kutekelezwa katika wilaya kumi na moja za Mikoa miwili ya Dar es Salaam, Mara na Njombe.

MWISHO

 KUPATA PICHA ZAIDI KUHUSU HABARI HII FUNGUA KIUNGANISHI HIKI:-https://simiyuregion.blogspot.com/2018/08/rita-kusajili-na-kutoa-vyeti-vya.html

 

 

Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa