• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

RC Mtaka: Simiyu Tutaendelea Kufanya Kazi kwa Kuheshimiana na Kusikilizana

Posted on: May 1st, 2019

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe. Anthony Mtaka amesema  Viongozi  Mkoani Simiyu wataendelea  kufanya kazi  na kuwahudumia wananchi  kwa kuzingatia utawala bora, utawala unaofuata sheria na uongozi wa kuheshimiana na kusikilizana.

Mtaka ameyasema hayo Mei Mosi, 2019 wakati alipokuwa akizungumza na wafanyakazi na wananchi mkoani humo katika Maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Kimkoa, yaliyofanyika katika Uwanja wa Nguzonane Wilayani Maswa.

“Tungependa tujenge utumishi ambao ni wa kipekee sana kwenye mkoa na kila mtumishi aliye kwenye mkoa huu ajisikie fahari kufanya kazi Simiyu; ahadi yangu kwenu ni kwamba tutaendelea kufanya kazi kwa kuheshimiana,kusikilizana na kutiana moyo katikati ya changamoto ambazo watumishi wanazipitia” alisema

Aidha, amewashukuru wafanyakazi kwa namna walivyojitoa kwa hali na mali  kuhakikisha kwamba malengo ya Serikali ya kuwahudumia wananchi yanatekelezeka  na kusisitiza kuwa mkoa utaendelea kufanya kazi kwa ushirikiano na Vyama vyote vya wafanyakazi na kuwataka waajiri wote wathamini vipaji vya watumishi wao.

Kwa upande wake Katibu wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Mkoa wa Simiyu, Bw. Said Mselem ameomba Serikali kushughulikia suala la upandaji wa mishahara na madaraja kwa watumishi ili kuwaongezea ari na motisha katika kazi.

Katika hatua nyingine Mselem ameiomba Serikali kuu kuona uwezekano wa kuwabadilishia mfumo wa malipo ya mshahara watumishi wanaolipwa kupitia mapato ya ndani na kuanza kuwalipa kupitia HAZINA, ili wawe na uhakika wa kupata mishahara yao na michango yao ya mifuko ya hifadhi ya jamii iwasilishwe kwa wakati.

Nao baadhi ya wafanyakazi  kutoka vyama tofauti vya wafanyakazi wamesema Wafanyakazi Mkoani Simiyu wanapenda kazi zao na wanafanya kazi kwa uadilifu, hivyo wameiomba  Serikali iendelee kuboresha mazingira na kuwasaidia kutatua changamtozao ili waweze kufanya kazi wa uhuru na kujituma zaidi.

‘Watumishi tunapenda kazi zetu na tunafanya kwa bidii na uadilifu, tunajua wapo wachache wanaotuangusha lakini tunaendelea kuwahimiza wawajibike kutimiza azma ya kuwatumikia wananchi, ombi letu kwa Serikali itukumbuke kwenye kupanda madaraja wapo ambao hawajapanda toka mwaka 2015” alisema Mwenyekiti CWT Itilima Mwl. Rehema Shalali.

“Watumishi wanaolipwa kwa mapato ya ndani wanakutana na changamoto ya mafao yao wanapostaafu, mafao hayaendi kwenye mifuko ya hifadhi ya jamii kwa kuwa wakati maana hawalipwi mishahara kwa wakati tunamwomba Mhe. Rais aliangalie hili, ili watumishi hao nao waweze kulipwa na HAZINA moja kwa moja” alisema Sara Kiyuga Mjumbe wa Baraza Kuu TALGWU Taifa.

Maadhimisho ya Mei Mosi kwa mwaka 2019 yamebebwa na Kauli Mbiu “ TANZANIA YA UCHUMI WA KATI INAWEZEKANA, WAKATI WA MISHAHARA NA MASLAHI BORA KWA WAFANYAKAZI NI SASA”  ambapo yamefanyika kwa mara ya saba sasa Kimkoa tangu mkoa wa Simiyu kuanziswa mwezi Machi, 2012.

MWISHO

KUPATA PICHA ZAIDI KUHUSU HABARI HII TAFADHALI  FUNGUA KIUNGANISHI HIKI:-https://simiyuregion.blogspot.com/2019/05/rc-mtaka-simiyu-tutaendelea-kufanya.html

Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa