• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

RC Mtaka Awashauri Wachezaji na Viongozi wa Coastal Union kutumia Falsafa ya Michecho ni Ajira na Biashara Kama Njia ya Kuleta Mapinduzi ya Soka.

Posted on: January 14th, 2019

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Anthony Mtaka amewashauri wachezaji wa timu ya Coastal Union ya Tanga kutambua kuwa michezo ni biashara na pia ni ajira hivyo wanapaswa kujiwekea malengo ya muda mrefu na mfupi ili waweze kunufaika na matunda ya jitihada zao.

RC Mtaka ametoa kauli hiyo ofisini kwake mjini Bariadi alipotembelewa na kikosi cha timu hiyo na viongozi wake kilichokuwa kikitokea mkoani Mara kwenye mechi ya ligi kuu Tanzania Bara ambako ilipoteza mchezo huo kwa kufungwa magoli 3 -2 na biashara United.

Katika salamu zake kwa timu hiyo Mtaka amesema njia pekee ya mafanikio kwa timu hiyo na wachezaji wake inaanzia kwenye nidhamu ya wachezaji ndani na nje ya uwanja na pia uwepo wa viongozi makini wanaojitambua na wenye nia ya kuleta mapinduzi ya soka nchini.

“ Binafsi sikubaliani na zile kauli  mbiu za michezo ni afya au michezo ni burudani, naendelea kusisitiza michezo ni biashara halikadhalika michezo ni ajira hivyo kipaji chako ndio mtaji wako”.

“Mkitambua hilo mtafika mbali, tunayo mifano hai, hebu mtazameni mchezaji kama Mbwana Samatta, huyu alijitambua mapema, akajiwekea malengo na ndio maana ameweza kufikia hapo alipo,analipwa mshahara ambao watanzania wachache sana wanaupata”, aliongeza Mtaka.

“Kumbukeni nidhamu ndio muhimili mkubwa utakaowapeleka mbali,achaneni na ulimbukeni wa Usimba na Uyanga, na pia msikubali kuingia katika vishawishi vya kutumia dawa za kulevya, mkifanya hivyo kwa umri wenu huu nawahikikishia mtafika mbali kuliko mnavyotegemea”, alisisitiza RC Mtaka.

Aidha Mtaka pia aliwatolea mfano wachezaji wa zamani kama George Weah ambaye kwa sasa ni rais wa Liberia na golikipa wa zamani wa TP Mazembe Robert Kidiaba Muteba ambaye hivi karibuni amechaguliwa kuwa mbunge huko Congo DRC  kuwa ni kielelezo cha nidhamu bora michezoni akisema kuwa kama wangekuwa na sifa mbaya jamii isingeweza kukubali kuwapa nyadhifa kubwa za kisiasa.

Kuhusu uongozi wa vyama vya soka nchini, Mheshimiwa Mtaka amesema ipo haja ya kuvitazama kwa makini zaidi kwani kwa sehemu kubwa ya viongozi wake wanaendesha mambo kijanja kijanja hali inayodhoofisha jitihada za serikali za kuleta mapinduzi ya soka nchini.

“ Mara nyingi huwa najiuliza, hivi kuna haja gani ya kusajili mchezaji wa kigeni kwa mamilioni wakati kiwango chake ni cha chini kuliko wachezaji wetu wa ndani, hawa viongozi wana ajenda gani na soka letu mpaka kufikia maamuzi hayo”, alihoji Mtaka.

 RC Mtaka ameongeza kuwa njia pekee itakayosaidia kuleta mabadiliko ya soka nchini ni mabadiliko ya mitazamo ya viongozi wake ambapo amesema wanapaswa kuweka uzalendo mbele na kuiona michezo kama fursa inayoweza kutangaza utalii wetu kupitia wachezaji waliowahi kutamba au wale wanaogonga vichwa vya habari hivi sasa akitolea mfano wa nchi kama Uganda ambayo baadhi ya mitaa yake imepewa majina ya wachezaji maarufu.

Aidha mheshimiwa Mtaka ambaye pia ni rais wa chama cha riadha nchini amesema kumekuwa na tofauti kubwa ya kimaisha kati ya wanariadha waliopata mafanikio kimichezo miaka ya nyuma na wachezaji wa soka waliowahi kutamba miaka hiyo kutokana na mfumo wa uongozi wa michezo uliopo.

RC Mtaka amesema kutokana na hali hiyo wachezaji wengi wa soka wamejikuta wakiwa taabani kimaisha mara baada ya kustaafu kucheza soka hali ambayo amesema tiba yake itapatikana endapo viongozi na wadau wa soka wataamua kubadili mitazamo yao na kuingia katika medani za soka la kibiashara kama ilivyo kwa nchi nyingi zilizoendelea.

Kwa upande wake kocha mkuu wa Coastal Union Juma Mgunda amekiri kuwepo kwa dosari za kiuongozi katika usimamizi wa mipango ya soka nchini na kuahidi kuufanyia kazi ushauri wake pale ambapo umeigusa timu yake.

“ Mheshimiwa mkuu wa mkoa timu yetu ni timu kongwe na imepitia vipindi vingi vya mpito, lakini kama ulivyojionea kwa sasa hali ni tofauti, tuna vijana chipukizi wenye uwezo mkubwa wa kuleta matokeo yatakayo washangaza wengi, binafsi ninaamini tutafika mbali”, aliongeza Mgunda.

Aidha kuhusu ushiriki wa mchezaji wa timu hiyo ambaye pia ni mwanamuziki maarufu wa kizazi kipya Ali Kiba, Mgunda amesema mchezaji huyo ni hazina kubwa ya timu hiyo na kwamba hawawezi kumtumia kwenye mechi za ugenini ambazo mapato yanachukuliwa na timu mwenyeji.

“Ali Kiba ni brand ya Coastal Union, anapoingia uwanjani ni lazima watu wajae kutazama mechi, na sisi kwa kutambua umuhimu wake tutamtumia kwa mechi za nyumbani tu ili pato lote liingie mfukoni kwetu”. Alisisitiza Mgunda.

Timu ya Coastal Union tayari imeondoka mjini Bariadi kuelekea Dar es Salaam kuendelea na michezo yake ya ligi kuu.

Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa