• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

RC Mtaka Awahakikishia Ushirikiano wa Serikali Waumini, Viongozi wa Madhehebu wa Dini

Posted on: May 31st, 2019

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka amewahakikishia waumini na viongozi wa madhehebu ya dini mkoani hapa kuwa viongozi wa serikali wako pamoja nao na wataendelea kushirikiana na kila watakapo wahitaji .

Mtaka ameyasema hayo jana Mei 30, 2019 katika futari aliyoiandaa kwa waumini na viongozi wa madhehebu ya Kiislam katika Viwanja vya Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mjini Bariadi.

“Ndugu zangu waislam mliopo hapa naomba muamini kabisa kwamba viongozi wa mkoa na viongozi wote wa Serikali kwenye maeneo yetu  ndani ya mkoa wa Simiyu wako pamoja na ninyi; kwa jambo lolote, eneo lolote ambalo mngehitaji ushirikiano kwenye mkoa wetu sisi tuko tayari kuunga mkono” alisema Mtaka.

Aidha, ameshauri viongozi wa BAKWATA Mkoa wa Simiyu kuomba kuandaa tukio moja kubwa la Kitaifa kufanyika Mkoani Simiyu kama ambavyo yamekuwa yakifanyika katika mikoa mingine na akaahidi kushirikiana na viongozi hao endapo watakuwa tayari kuandaa tukio lolote.

Katika hatua nyingine Mtaka ametoa wito pia kwa viongozi wa Madhehebu ya Kiislam kutengeneza mazingira mazuri kwa vijana na kuwafundisha ikiwa ni njia moja wapo ya kuwaandaa kushiriki katika mashindano ya kuhifadhi Quran ili Mkoa wa Simiyu na nchi kwa ujumla iweze kuwakilishwa vema katika mashindano hayo.

Sambamba na hilo amewashukuru viongozi wa dini kwa kuendelea kuiombea nchi, viongozi wake, kuombea amani, umoja na mshikamano miongoni mwa Watanzania ambapo amebainisha kuwa Serikali inatambua mchango wa Taasisi za dini katika nchi na kwa namna viongozi wa dini wanavyoshirikiana na Serikali katika masuala na mtukio mbalimbali.

Kwa upande wake Sheikh Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mahamoud Kalokola amemshukuru Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka kwa namna anavyoenzi waislam na akatoa wito kwa watu wengine kuiga mfano wake kwa kuwa kila anyefanya hivyo anapata thawabu yake kwa Mwenyezi Mungu.

Ameongeza kuwa tendo hilo la kufuturisha linawakusanya watu pamoja walio waislam na wasio waislam jambo ambalo linadumisha umoja, upendo, ushirikiano na mshikamano kwa wote bila kujali tofauti ya dini zao.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Mhe. Festo Kiswaga amempongeza Mkuu wa mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka ambao nao watajipanga kufanya jambo hili ili nao waweze kupata baraka za Mwenyezi Mungu.

Huu umekuwa ni utaratibu kwa Mkuu wa mkoa wa Simiyu, kuandaa furati kwa waumini viongozi wa madhehebu ya dini ya Kiisla, ambayo pia huwahusisha viongozi wengine wa chama na Serikali wakati wa mfungo wa mwezi Mtukufu wa Ramadhani.

MWISHO

KUPATA PICHA ZAIDI FUNGUA KIUNGANISHI HIKI:-https://simiyuregion.blogspot.com/2019/05/mkuuwa-mkoa-wa-simiyu-mhe.html

Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa